SAUT na Vyuo vingine, Shule za kanisa havina malengo ya kweli kumkomboa mtoto wa maskini wa TZ.

SAUT na Vyuo vingine, Shule za kanisa havina malengo ya kweli kumkomboa mtoto wa maskini wa TZ.

jembe la kigoma

Senior Member
Joined
Mar 23, 2012
Posts
119
Reaction score
19
Ni kwa mda mrefu sasa shule,vyuo na taasisi nyingine zinazotoa huduma kwa jamii huku zikimilikiwa na makanisa hasa kanisa katoliki yamekuwa yakijidadavua kuwa na malengo ya kuwasaidia watoto na watu wasiojiweza kupata huduma wanazozitoa kwa gharama nafuu,lakini kinyume chake zimekuwa hazina tofauti na shule na vyuo vingine vinavyomilikiwa na taasisisi na watu binafsi wenye malengo ya kupata faida tu,kwa mfano kwa sasa wanafunzi wa chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino(SAUT)Wapo kwenye maandalizi ya mitihani ya kumaliza mhula(semister)ili ufanye mtihani ni lazima uwe na kadi ya mtihani,na ili upewe kadi hiyo haupaswi kuwa unadaiwa hata shilingi 500 kati ya ada ya shilingi (MILIONI MOJA,LAKIMBILI NA ELFU 32)tabu inakujakwa wale wanafunzi wanaotokea familia za kawaida,maskini na wasio na uwezo wa kuwasomesha na kugharamia gharama zingine kwa mwanafunzi,hivyo kupelekea mwanachuo kujisomesha na kuendesha maisha yake kwa kutegemea mkopo kutoka bodi ili alipe Ada,stationary nyumba na chakula,hivyo uwezekano wa kulipa ada yote bila kuacha madeni haupo,hivyo kuwanyima vibali vya kuketi chumba cha mtihani ni kuwaonea na kuwanyima haki ya msingi ya kupata elimu,kuwaambia kama haujamaliza ada wasubiri mwezi wa 9 kufanya mitihani maalumu (special)ni kwenda kinyume na lengo la kanisa kuwasaidia watoto wa maskini,hii ndo inapelekea watoto wa kike kujiuza na kupata maradhi,kama haitoshi akichelewa kulipa anapigwa faini(penati) ya shilingi laki 1,wakati huohuo chuo kinatambua kwa jinsi gani bodi ya mikopo hawaleti fedha kwa wakati hivyo kupelekea wanachuo kuishi kwa kukopakopa,wito Kama askofu mkuu Pengo alivyosema taasisi za dini zikumbuke lengo kuu la kanisa kufungua vyuo,shule na hospitali na kuwasaidia wananchi na si ufanya biashara.
 
Mleta mada,SAUT ni kati ya vyuo vya private ambavyo bado ada iko chini,kujiunga hapo maana yake unakubaliana nao,uzuri umesema kuna special exam,hivyo mjipange ili mfanye hiyo september.
 
Kaka unataka usome bure halafu upate elimu gani? Au walimu wawe wanajitolea tu?
 
Nenda kasome Morogoro kwenye kile chuo kilikuwa cha Tanesco Mkapa akawapa Waislamu pale hawalipi ada
 
Fee structure ya UDSM:
attachment.php

attachment.php


Source : http://www.udsm.ac.tz/sites/default...c_for_degree_advert_for_equivalents_11_12.pdf p. 10 -11



  1. Pamoja na structure hii ya fee ya UDSM, chuo hakihusiki na kulipa mishahara, na bado kuna fedha zinapelekwa chuoni kwa ajili ya OC. SAUT inategemea ada tu kulipa mishahara na gharama zote za uendeshaji.
  2. Gharama za ukarabati na ujenzi kwa vyuo vya serikali hazitegemei hiyo ada wakati vyuo binafsi (ikiwemo SAUT) vinatumia hizo hizo kwa ukarabati.
  3. Vyuo binafsi ni lazima vihakikishe vinaweza kujiendesha kutokana na ada zake, hakuna anayetoa fedha za ziada kwa ajili ya kusaidia kuendesha chuo.
  4. Wasipowabana wakati wa mitihani fedha hazilipwi
  5. Kwa watu wenye shida za dhati, kuna mpango wa kusaidiwa kama kuna vithibitisho (Mwone DVCAF, wakati unajiunga na chuo)
  6. SAUT ada yake iko chini hata ya hivyo vya serikali kwa programmes nyingi. Hakuna chuo kingine cha binafsi chenye ada za chini kama SAUT.


Angalia hapa mfano wa ada za Tumaini University

attachment.php

Source: http://www.tumaini.ac.tz/docs/joining.pdf

Ulitegemea waite watu waende kusoma bure ndio ujue kuwa wanamkomboa mtoto wa maskini?

If you think education is expensive try ignorance.
 

Attachments

  • fee.PNG
    fee.PNG
    24.4 KB · Views: 903
  • fee1.PNG
    fee1.PNG
    32.3 KB · Views: 897
  • fee2.PNG
    fee2.PNG
    9.6 KB · Views: 880
Hii haina tofauti na chuki binafsi dhidi ya makanisa!!
 
Nenda kasome Morogoro kwenye kile chuo kilikuwa cha Tanesco Mkapa akawapa Waislamu pale hawalipi ada

Mleta uzi asipende kudanganya watu kila chuo kina utaratibu huo wa kuwabana wasiolipa ada.Kwa kuwa lengo lake ni kuonyesha kuwa eti vyuo vya kanisa vinanyonya watanzania eti kwa gharama kubwa atupe ulinganisho na vyuo vingine.Mwisho nimfahamishe kuwa hata MUM morogoro wanatoa vibali vya mtihani kwa wanachuo wasiodaiwa km anabisha aende kuwauliza wanachuo wa pale
 
Jembe la kigoma huna hoja hapa. Kama loans board inachelewa kuwapa fedha, kailaumu serikali na si chuo. Unatarajia chuo kijiendeshe vipi bila ada? Mishahara ya watumishi, stationaries na gharama nyingine zinazokuwezesha usome zitalipwaje? Kama vyuo vya serikali ambavyo vina ruzuku bado vinazuia wasiomaliza ada kufanya mitihani, unatarajia nini kwa chuo binafsi kisicho na ruzuku???
 
We una lako jambo na SAUT, its the cheapest university in Tz halafu unasema hakina nia ya kumkomboa Mt wa kawaida? Hakuna chuo kinachoweza kuruhusu mwanafunzi afanye mtihani kama anadaiwa hata kama ni tshs 5.
 
Hata mimi ni graduant frm SAUT, hakuna chuo private Tanzania ambacho kina gharama reasonable kama SAUT. Jaribu kuulizia vyuo private vingine kama TUMAINI uone mziki wake.
 
Fee structure ya UDSM:
attachment.php

attachment.php


Source : http://www.udsm.ac.tz/sites/default...c_for_degree_advert_for_equivalents_11_12.pdf p. 10 -11



  1. Pamoja na structure hii ya fee ya UDSM, chuo hakihusiki na kulipa mishahara, na bado kuna fedha zinapelekwa chuoni kwa ajili ya OC. SAUT inategemea ada tu kulipa mishahara na gharama zote za uendeshaji.
  2. Gharama za ukarabati na ujenzi kwa vyuo vya serikali hazitegemei hiyo ada wakati vyuo binafsi (ikiwemo SAUT) vinatumia hizo hizo kwa ukarabati.
  3. Vyuo binafsi ni lazima vihakikishe vinaweza kujiendesha kutokana na ada zake, hakuna anayetoa fedha za ziada kwa ajili ya kusaidia kuendesha chuo.
  4. Wasipowabana wakati wa mitihani fedha hazilipwi
  5. Kwa watu wenye shida za dhati, kuna mpango wa kusaidiwa kama kuna vithibitisho (Mwone DVCAF, wakati unajiunga na chuo)
  6. SAUT ada yake iko chini hata ya hivyo vya serikali kwa programmes nyingi. Hakuna chuo kingine cha binafsi chenye ada za chini kama SAUT.


Angalia hapa mfano wa ada za Tumaini University

attachment.php

Source: http://www.tumaini.ac.tz/docs/joining.pdf

Ulitegemea waite watu waende kusoma bure ndio ujue kuwa wanamkomboa mtoto wa maskini?

If you think education is expensive try ignorance.

good annalysis. stay blessed
 
Kama shida yako ni kusoma bure, kuna taasisi zinazotoa misaada ya kulipia karo ila itahitajika uwe na sababu za kwa nini unadhani unastahili kusomeshwa bure.

Kwa uwiano bado ada ya sauti ni ndogo kulinganisha na vyuo vingine.

Katika uvivu wetu wa kufikiri na changanya na wazazi/ndugu zetu kukosa vipaumbele wengi wangetamani kusomeshwa bure, sasa chuo kitajiendeshaje?

Sielewi hii mada yako imelenga nini ila kama umekwenda shule sidhani kama hiyo elimu ndogo uliyopata imefanikiwa hata kukufuta ujinga!
 
Ndugu acha kuudanganya umma. SAUT ni chuo kinacho toza ada ya nafuu ambayo hata mtoto wa mkulima anaweza kusoma. Halafu unaposema mwanafunzi haruhusiwi kufanya mtihani mpaka akamilishe ada yote huo ni uongo kwani mpaka sasa zaid ya asilimia 60 ya wanafunzi wanaoanza mtihan j3 wenye vitambulisho hawajalipa ada yote. Mwanafunzi kufanya mtihani wa first semester anatakiwa awe amelipa sh 723,000 tu, sasa hii si ada ya sekondari ya private? Chini ya hapo hapewi kitambulisho cha mtihani but kama ana matatizo yanayoeleweka ana onana na DVCAA na anapewa ID ya mtihani. Ndugu jua unayoandika sio unakurupuka tu.
 
Kumbe MOU imesaidia sana, chuo cha kanisa ada yake haitofautiani na chuo cha serikali. Hongera Waheshimiwa Anne Makinda na Edward Lowassa kwa kuweka saini zenu kwenye MOU, matunda yake ni haya watu wengi zaidi wanapata elimu.
 
Ulitaka usome bure tu. We unawakwepa wanakushika kwenye paper
 
Mwanaukweli amemaliza hoja dhaifu isiyo na mantiki hata kidogo. Hivi mtu kama huyu katokea wapi mbio patapatapata kama bata kuleta hoja hii. Kutokufanya mtihani kwa kutolipa ada ndiyo kwanza umesikia leo? Ni lini mleta mada alipeleka sadaka kanisani na ukasema ni ya kuendeshea chuo ili watoto wa maskini wasome bure? Mbona mnalipa kodi ada za vyuo vya serikali ziko juu na bado mnachangishwa fedha za ujenzi, madawati, hostel nk. hamsemi? Chuki ulizolishwa hazifai
 
Ndugu acha kuudanganya umma. SAUT ni chuo kinacho toza ada ya nafuu ambayo hata mtoto wa mkulima anaweza kusoma. Halafu unaposema mwanafunzi haruhusiwi kufanya mtihani mpaka akamilishe ada yote huo ni uongo kwani mpaka sasa zaid ya asilimia 60 ya wanafunzi wanaoanza mtihan j3 wenye vitambulisho hawajalipa ada yote. Mwanafunzi kufanya mtihani wa first semester anatakiwa awe amelipa sh 723,000 tu, sasa hii si ada ya sekondari ya private? Chini ya hapo hapewi kitambulisho cha mtihani but kama ana matatizo yanayoeleweka ana onana na DVCAA na anapewa ID ya mtihani. Ndugu jua unayoandika sio unakurupuka tu.

Acha umbea, kuna rafk angu boom lake hadi sasa halijafika yupo ktk yale majina 215. Ameenda kwa DVCAA amemwambia aandike barua ya kufanya special. Chuo kina matatizo makubwa na wala msitetee upuuzi huu.
 
nimesoma saut sijawah kukutana na ulichokiandika,nijuavyo mimi hadi kufikia muda wa kufanya mitihani ya semesta ya kwanza unatakiwa uwe ushalipa nusu ya ada au angalau uwe umelipa laki 5,6 au 7,unafanya mtihani bila shida na unapata matokeo.
 
Back
Top Bottom