Sauti ya Wanavunjo bajeti ya TAMISEMI bungeni

Sauti ya Wanavunjo bajeti ya TAMISEMI bungeni

MTANZANIA620

Member
Joined
Jun 20, 2023
Posts
65
Reaction score
81
Mbunge wa Jimbo la Vunjo Dkt. Charles Stephen Kimei amekuwa miongoni mwa wabunge waliochangia katika mjadala wa bajeti ya wizara ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ambapo ameeleza mambo kadhaa ikiwemo:-

Dkt. Kimei ameishukuru serikali na kumpongeza kwa wingi wa miradi katika jimbo la vunjo na kumhakikishia shukrani za wanavunjo ataanza kuziona kupitia ushindi wa kishindo uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.

Aidha Dkt. Kimei aikumbusha serikali utekelezaji wa ahadi zilizosalia za viongozi wakuu na ahadi za ilani ya uchaguzi ya ccm 2020-2025

Aomba bajeti hii itenge fedha Barabara za Nyerere (Kilema Pofo - Mandaka - Kilema); Chekereni - Kahe - Mabogini - TPC; Uchira - Kisomachi - Kolarie; Himo - Sokoni - Lotima pamoja na kufungwa taa mji wa himo

Aomba kituo cha afya mwika msae kipate fedha za kuongeza majengo ya mama na mtoto, maabara, wadi nk

Hakika hii ni sauti yetu, tunaamini serikali sikivu ya awamu ya sita chini ya mhe rais dkt samia suluhu hassan itaisikia

Mtaa unasema hakika tulichagua mwakilishi muaminifu anayeyajua mahitaji yetu

#VunjoTumechagua
#CCMTeamMaendeleo
#MaendeleoKwaVitendo
#KaziIendelee

 
Ww ndio mbunge wa vunjo Nini, kwani rais anategemea kura au mbeleko ya vyombo vya Dola?
 
Tunaelekea kwenye chaguzi mbalimbali.Kila mmoja ameshateua chawa wa "kumuongea vema" kwa umma.
 
Back
Top Bottom