Scania buses na Cummins buses ( Zhoungtong climber, yutong ect)

Shukurani sana brother! Nimekuelewa vizuri sana
 
Nilibanana kidogo nikashindwa kukuuliza yafuatayo;

Hiyo technology imeanzia kwenye kizazi cha tano pekee? Maana kuna 16L ya kizazi cha nne unaizungumziaje?

Halafu kwanini R470 ilionekana ni bora zaidi mpaka ikachukua tuzo 2010 na siyo R500
 
Endeleeni tu kufananisha mchina na scania
Inaitwa bulldog
 
Kilo ya mawe na kilo moja ya pamba nn kizito?
Unatafuta ulinganifu kwenye vitu visivyo lingana! Naona unalazimisha tubishane, umesema ila sio pikipiki za kichina sasa kwani speed inategemea na mtengenezaji? Maana mchina nae ameandika pikipiki yake inaenda speed 120... Ngoja niache ushinde wewe kwenye hili ila ukija kuendesha gari ndogo ukiwa speed 130 na ukapitwa na scania ambayo top speed kwenye dash ni 120kph utakumbuka kauli yangu
 
Nilibanana kidogo nikashindwa kukuuliza yafuatayo;

Hiyo technology imeanzia kwenye kizazi cha tano pekee? Maana kuna 16L ya kizazi cha nne unaizungumziaje?

Halafu kwanini R470 ilionekana ni bora zaidi mpaka ikachukua tuzo 2010 na siyo R500
Low Rev ilianzia kwenye series 4 miaka ya 2000, wakati huo kulikuwa na 164 480 @2300Nm na 164 580@ 2700Nm lakini hizi zote zilikuwa ni euro3, hizi pia ni nzuri ila zimepitwa tu na wakati

R500 euro4 ili ingia kuanzia 2005, ingawa kuna matoleo mengi Sana hadi euro 6, ingawa kuanzia mwaka 2016, R500 ni straight six sio v8 tena.

R470 turbocompound ilikuwa truck of the year 2010 southern Africa sio duniani, Ni Moja ya engine sumbufu Sana ikichoka na ulaji wake wa mafuta sio economical
 
Hapa tz scania ataendelea kupeta sana matajiri wananunua michina engine zikifa wanatia scania maisha yanaendelea....ile michina ya osaka iliyoandikwa mberesero the great yote mashine zake scania.....na wengine wamefika mbali kwa kununua bodi za kichina wanatia engine ya scaniA....
Livelong msweden
 
Swali langu lina msingi wa hesabu darasa la tatu miaka ya 1980 na 90. Kama ulibahatika kusoma kipindi icho nazani ulikutana nalo. Logic ya ilo swali ni kujua kipimo. Kwenye spidi ya gari kipimo ni kph au mph. Unapoendesha pikipiki yenye uzito mfano honda (baja) yenye cc 250 za ukweli kwenda spidi 120 ni kitu cha kawaida na mwendeshaji huwezi feel iyo spidi ila ukiendesha spidi iyo kwa boxer kila mahali utavibrate

Nikuibie siri hizo scania unazodai top speed yake ni 120 huwa zinakimbia speed kubwa kuliko iliyoandikwa kwenye speed mita yake. Kwa kukanyaga exletor speed itacheza kwenye hiyo 120 kutokana na kuwa na gavanor ila unapohitaji ikimbie zaidi unachomoa fuse ya speedmeter na kuruhusu velocity ifanye kazi yake...
 
Hapa uliposema R470 ilikuwa truck of the year kwa nchi za kusini mwa Africa umenichanganya kidogo, nijuavyo hiyo tuzo hushindanisha trucks kwa kufuata criteria walizoweka kama fuel economy, carbon emissions n.k. ambapo mwaka huu FORD ndiyo mshindi.

Naomba unitofautishie hiyo tuzo ya kusini mwa Africa na hiyo ya dunia kwa ujumla
 
Umeniwahi mkuu! Mbali na kwamba zile chombo zinaamsha lakini wale drivers kweli wamevurugwa!
Ile scania hakuna Golden deer wala Newforce anayofaita hiyo mashine afu dereva ndo kavurugwa
 
Umeniwahi mkuu! Mbali na kwamba zile chombo zinaamsha lakini wale drivers kweli wamevurugwa!
Yule tall wa sauli sio binadamu yule hana kona wala mteremko(kitonga) anashusha kama tambarare afu mashine inaita afu uje ufananishe na mchina hapana
 
Hata usipochomoa fuse kama haijafungwa itakimbia zaidi na utaona ile speed meter inajigonga tu na mwisho huwa inakufa kabisa utakuta haisomi, ndo maana yangu ilipo maana kuna mtu alisema scania haiwezi kuikuta zhongtong kisa imeandikwa 140kph wakati scania ni 120kph hilo ndo nilikuwa napinga coz mara nyingi tu kabla ving'amuzi havijaanza nilikuwa nawakata humu barabarani wenye michina yao kama wamesimama... Na kuna siku nilikuwa na noah nilikuwa eneo la mafinga maenda Makambako nikiwa speed 140 nilipitwa na abood zile marcopolo hadi nikaishia kucheka tu... Na pia niliwahi kukaa lock up Iringa wiki nzima mwaka 2011 kwakuwa nimekamatwa speed 147 kwenye 50kph halafu mtu anasema scania ina top speed 120 tu??
 
Duh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…