Scania buses na Cummins buses ( Zhoungtong climber, yutong ect)

Juzi hapa nilisafiri na huyu mnyama freightliner hatari sana,kwanza masaa machache ya kwanza ya safari ndani ya gari nilikua na eargasm za kutosha . Sijawahi ona gari ambayo inajibu gears kama hii, nilikua natamani Mimi ndiye niwe dereva wa hii mashine .Gearbox ni Eaton Fuller heshima kwao.Bahati mbaya video imegoma ku-upload.View attachment 1197146
 
Unaposema, "inajibu gears" unamaanisha nini?
 
Unaposema, "inajibu gears" unamaanisha nini?
Kwa mfano truck za kisasa kama Scania ziko kimya sana kama gari ndogo,gia zinaingia kimya .Hiyo truck inapiga chafya mpaka kwenye gia lever,anavo change gia kuna sauti maalum inatoka kwenye eidha engine au Gearbox. Natumai maelezo yamejitosheleza kidogo.
 
Sema unapenda yale makelele.
 
Hahahaha kumbe kucheua? Automation iko sambamba na umeme ndio maana gari nyingi zimeachana na kucheua, kucheua kuna baki kwenye mabreki tu
 
Unanikumbusha coaster moja box ilikua inaenda ikwiriri,imeandikwa Chelsea nyuma..dah haifai ile chuma...
 
Yeah ni kweli ila mwisho wa siku ni utunzaji tu check yutong f12 & f12+ za abood Bado mbichi kabisa
Mbichi zinaenda wapi mkuu?....hivi kuna Cumming yeyote inavuka boda? Mana naona kampuni karibia zoote za masafa marefu zinatumia scania.
 
Truck nyingi za mchina zinatumia engine za Cummins.
Mbichi zinaenda wapi mkuu?....hivi kuna Cumming yeyote inavuka boda? Mana naona kampuni karibia zoote za masafa marefu zinatumia scania.
 
Si kwamba ninakukosoa.....ila naomba urudi kisoma tena kitu kinaitwa gear ratio....

Waliotengeneza magari makubwa na madogo walitumia physics na hisabati za hali ya juu...

Hapa kinachotokea ni nini...
Kwa mfano Scania ikiwa 50kph na Passo ikiwa 50kph, haya magari mawili hayataachana kwa kwa mendo. tofauti itakuwa kwenye mzunguko wa gear box na matairi..

Ni dhahiri kuwa gear box ya gari kubwa itakuwa na mzunguko medogo kwa sababu ina matairi makubwa na gear box ya gari ndogo itakuwa na mzunguko mkubwa ili kufanya katairi kadogo kazunguke sana ili ku... maintain speed iliyopo..

Kwa hiyo, kwa mfano tairi la gari kubwa likizunguka mizunguko 2 ili kupata speed 50, tairi la gari mdogo linaweza kuzunguka mizunguko 3....

Hapa ni swala la namna gear zilivyotengenezwa...

Kwa hiyo si kweli kama watu wanavyopotoshana vijiweni kuwa basi likiwa mf 100kph, passo iwe 120kph eti ndiyo ziwe sambamba,......ni upotoshaji..

Gari kubwa na ndogo yote yataenda sawa kama yapo speed 100 tofauti itakuwa kwenye idadi ya mizunguko ya tairi na gear ratio...

Kuna mambo machache yanayoweza kuathiri speed halisi ya gari na ndiyo maana kwenye tochi wameweka balansi ya zile points 5.....yaani ukiwa speed 50.5 kurudi chini huandikiwi faidi....

Kwa mfano gari ndogo kama ilitoka na tairi size 175/70 r15, ukaja ukabadilisha ukaweka 195/70 r14....hapa utapata badiliko la speed bila wewe kujua....ndani kwenye dash utaona mshale unasoma 50 lakini actual speed kwa nje ukipihwa tochi inaweza kuwa 50.2 mpka 50.3 hivi....kwa ninj..? kwa sababu umebadilisha ukubwa wa tairi uliopimwa kulingana na gear ratios za gari husika na kuweka tairi kubwa........

Nawasilisha.
 
Hili napingana na wewe...80kph ya vitz haiwezi kuwa sawa na 80kph ya bus ...atakupita tu hata iweje
Mungu baba...
Kasome kwanza kitu kinaitwa gear ratios na tire size...ndiyo uje ubishe...

Vitz ukiwa 80, ni sawa na basi likiwa 80..
 
Mbichi zinaenda wapi mkuu?....hivi kuna Cumming yeyote inavuka boda? Mana naona kampuni karibia zoote za masafa marefu zinatumia scania.
Kama kigezo ni kuvuka boda darlux, tahmeed, modern coast, trinity wote hao wanamichina inavuka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…