Scholarship ipi ni nzuri kwa Doctor of Medicine, na chuo gani?

Msafiri Kasian

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2011
Posts
2,133
Reaction score
661
Nina mdogo wangu anasoma form six, natafuta scholarship ya kusoma doctor of medicine baada ya kumaliza masomo yake ya secondary.nimajaribu kutembelea tovuti mbalimbali nimeshindwa kujua nichuo gani kingeweza kumfaaa na utaratibu wa kufuatwa ili kupat nafasi hiyo. Hivyo basi ninaomba msaada kwa wenye uzoefu ili nipate kumsaidia.Ninapenda kutanguliza shukurani zangu za dhati.
 
Kuna kozi za MD zinatolewa Tanzania kwa udhamini wa bodi ya mikopo (HESLB). Hivyo wala usiwe na presha, presha iwe kwake kufaulu sana ili apate admission. Vyuo vizuri kwa sasa ni Muhimbili (competition kubwa kupata), zikifuatiwa na KCMC na Bugando. Ukiwa na sifa na ukapata nafasi huko utapata ushamini wa bure toka bodi ya mikopo.
Kuna scholarships za kusomea degree hizo hizo nchini China, Urusi, Uturuki na Algeria. Sijui kama Misri na Cuba kama wanatoa. Ulizia Wizarani kwa Kawambwa na balozi za nchi tajwa.
Ukiacha Misri, ni bora mdogo wako asome hapa hapa Tanzania, kwani ukipelekwa katika hizo nchi tajwa utasajiliwa kwenye vyuo vidogo na mara nyingi graduate huwa hayuko vizuri kitaaluma.
BTW: Huyo dogo anataka kusoma Medicine au wewe ndio wataka asomee Medicine? Vichwa vingi sana vipo kusoma PCM na PCB, galafu vinafikiria engineering tu na Medicine. Wenzenu mnaowaona mazezeta sasa bdio wanakuja kuwatengenezea policies na hata pia kuwapangia mishahara. Ukisoma na kufaulu vizuri PCB na PCM si lazima usome Medicine au Engineering. Kuna course nyingine nzuri kama Bcom, Bpharm, Economics n.k.
 
Mkuu nashukuru sana kwa ushauri, dogo aliniambia yeye mwenyewe anaomba nimsaidie kutafutia,na anatamani kwenda kusoma medicine nikaona ni vyema niulize kwanza kwa watu wenye uzoefu. Hata hivyo ushauri wako utafanyiwa kazi. Asante
 

Sio kweli kuwa wanaosoma MD nje wanapelekwa kwenye vyuo vidogo ukiacha Misri...Nina experience na Algeria ambako nimesomea MD na vyuo tulichagua wenyewe baada ya mwaka wa lugha. Kwa kifupi wanafunzi wageni wana wigo mpana wa kuchagua vyuo wenyewe tatizo siku hizi hawatoi nafasi zaidi ya mbili za MD kwa mwaka kwa kila taifa geni lenye wanafunzi algeria pia ukija huku ukubali kupoteza miaka si chini ya nane (mmoja wa lugha ya kifaransa, sita ya shule, mmoja wa internship ya lazima). Halafu kwa algeria hamna tofauti kubwa ya vyuo vya udaktari maana vyote ni vya serikali. Ni hayo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…