Eti kwamba 98% wa jf member wanaskilizaga nyimbo za kiingilish tu! Niko hapa nasikiliza "enokwe nu muya"
GENTAMYCINE
makorere
tata akanga
GENTAMYCINE kila nikiamka ni lazima nisikilize hizi Rhumba Kali za Wanamuziki wangu pendwa na Wakubwa Congo DR akina Ngiama Makanda Werrason, Koffi Olomide na JB Mpiana.
Asubuhi nikiamka tu nasikiliza Rhumba Kali la Werrason liitwalo
Nakokitee ambapo Werrason kafanya balaa Kubwa
Mchana baada ya Kula nasikiliza Rhumba Kali la Koffi Olomide liitwalo
Destination ambapo Koffi kamaliza huko
Usiku kabla sijalala nasikiliza Rhumba Kali la JB Mpiana ambalo kwa Rekodi za Congo DR hadi leo hakuna aliyevunja Rekodi kwa Kupendwa na Wakongo wote la
OMBA ambapo hapo JB Mpiana kalalamika sana hadi Kulia kwakuwa huu Wimbo ni Kisa cha Kweli ambapo JB Mpiana alikuwa akimlilia Mkewe aliyempenda hakuna mfano aitwae Amida ambaye katika huo Wimbo alimbatiza Jina hilo la
OMBA.
JB Mpiana aliporwa na Tajiri Mmoja Congo DR Vitara Kamere (kama sijakosea) na baadae Tajiri Vitara Kamere nae akaporwa huyo Mwanamke Mrembo
OMBA na aliyekuwa Rais wa Congo DR Mtoto wa Mikocheni Dar es Salaam na sasa yuko Mbezi Beach huku akiwa ameikarabati Hoteli yao ya Regency pale Msasani kwa Mwalimu Nyerere (sasa kaibadili Jina) Joseph Kabila.
Na mpaka hivi sasa naandika hivi tayari JB Mpiana amesharudiana rasmi na huyo Mkewe Kipenzi Amida Shatour (OMBA) aliyemzalia Watoto wawili ambao JB Mpiana hupenda kuwapaisha karibu katika Nyimbo zake zote waitwao Suraiya (wa Kike) na Junior (wa Kiume)