Sean 'Diddy' Akabiliwa na kesi mpya 120 za unyanyasaji wa kingono kabla ya kusikilizwa kwa kesi za awali

Sean 'Diddy' Akabiliwa na kesi mpya 120 za unyanyasaji wa kingono kabla ya kusikilizwa kwa kesi za awali

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
1727895912559.png

Hii achatuseme kwamba kazini kwa Diddy kuna kazi. Kesi zinazidi kumiminika zinazomuhusu yeye hadi sasa ni maumivu kwake na je atazishinda zote kesi hizi?

==================

Mkali wa Hip-Hop wa Marekani, Sean “Diddy” Combs anatuhumiwa kuhusishwa katika kesi mpya 120 za unyanyasaji wa kingono zinazotarajiwa kuwasilishwa mahakamani siku 30 zijazo kabla ya kesi zake za awali kuanza kusikilizwa.

Akiongea na waandishi wa habari jana Oktoba Mosi, wakili Tony Buzbee kutoka Texas ameweka wazi kuwa watu 120 wamewasilisha madai ya unyanyasaji wa kingono unaodaiwa kufanyika miaka 20 (miongo miwili) iliyopita huku akisema kuwa ana ushahidi wa picha na video.

Aidha wakili huyo alimtaja mhusika mmoja kuwa ni mtoto mwenye umri wa miaka tisa ambapo Diddy na wengine wanatuhumiwa kumnyanyasa kingono katika studio za Bad Boy Records huko New York.

Soma Pia:
Hata hivyo Diddy anapambana kujinasua kutoka kwenye mikono ya sheria baada ya kukusanya wanasheria mashuhuri kuhakikisha wanamtetea na kupata dhamana ya kutoka mahabusu zikiwa zimepita wiki mbili tangu alipotiwa nguvuni.
 
Mimi km shangazi wa bi harusi nahitaji diddy aninunulie tandale yote achukue mkewe.!! 😹
Haahah au sio hahah

Ila wazingua sana walipaswa tu kukaa kimya sasa yametokea kutokea ndio wanajifanya kusema sasa wabongo hawataki kuelewaa haahh
 
Kesi 120 mpya, vichupa 1000. Hapa naona idadi bado haijatimia kufikia usawa wa vichupa na watendwa au wengne wameona wakae kmya

babu tale na diamond
 
Ali Msomali aka Diddy aka Shemeji kesi yake itaanza kuunguruma 05 May 2025 kwa kipindi mpaka kuanza kwa kesi atabaki tu "nyuma ya nondo" aka segedansi aka Lupango aka inside aka ndichi.
 
Back
Top Bottom