Segerea

Kirikou Wa Kwanza

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2013
Posts
3,564
Reaction score
1,991
Kuna jamaa alikamatwa na kupelekwa Segerea wakati
anaingia wafungwa wa mule ndani wote wakaanza
kuimba "Mwalii mwalii
mwalii mwalii!."
Jamaa kusikia anaitwa mwali akaona hili balaa akijilegeza tu watamgeuza mke wao! Jamaa akabidi
kujikaza kisabuni akakunja sura.
Mfungwa mmoja akamuuliza kwa
kumfokea "Umeletwa Segerea kwa
kosa gani?"
Jamaa akajua hii ndiyo chance kwa ujasiri akajibu "Nimeua watu wanne" Wale wafungwa waliposikia hivyo hakuna aliyemgusa.
Asubuhi ndugu zake na jamaa wakaja
kumtoa, polisi akamfata akamwambia "We mwizi wa mifugo
toka nje ndugu zako wanakungoja." Hayaa wafungwa waliobaki ndani kusikia hivyo wakabaki na masikitiko wengine wakisema "Ana bahati tumemkosa."
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…