Sehemu ya kuanikia nguo huwa inasahaulika katika ramani na ujenzi wa nyumba

Sehemu ya kuanikia nguo huwa inasahaulika katika ramani na ujenzi wa nyumba

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Usafi wa nguo hufanyika kila mara na hii inategemea ukubwa wa familia au wingi wa wakazi. Kuna wanaofua kila siku, kila baada ya siku au mara moja kwa wiki. Wengine Hufua kwa mashine na kukausha kwa dryer, hawa siwaongelei hapa kwani ni wachache sana.

Nguo kuanikwa hovyo hovyo kunapoteza uzuri wa nyumba. Unakuta ni nyumba nzuri barazani kuna nguo zimeanikwa. Zile za community ndiyo balaa, nguo kuonekana kambani ni sehemu ya maisha.

Kusema ukweli kutegemea nishati ya jua kukaushia nguo ni rahisi na unaokoa pesa pia mazingira. Kutumia umeme kukaushia nguo ni wakati tuna jua la ziada ni matumizi mabaya ya nishati.

Kama unajenga nyumba ni mihimu kufahamu idadi ya watu watakaoishi humo pia huduma zao kama kuanika nguo zitakuaje. Ni nyumba chache za community unakuta kuna makaro ya kufulia na miti na kamba za kuanikia nguo hasa nyuma ya nyumba. Pia unaweza kuvuta bati hasa lile transparent uweke eneo la kuanikia nguo siku za mvua.

Huwa ninakereka kuona maghorofa mazuri mjini lakini barazani nguo zimeanikwa. Uzuri wa nyumba unapotea ghafla.
 
Ata sehemu ya kuhifadhi/kutupa taka, kuna ndugu yangu kaweka bonge la garden kuzunguka nyumba ila taka zinamtesa
Hili la taka kuna tozo la serikali ya mtaa unalipia lakini ukusanyaji wao ni mbovu pia hakuna vyombo maalum vya kukusanyia taka. Ni muhimu kuwe na kitengo cha kukusanya taka kubwa kama kitanda, kabati au fridge isiyo hitajika.
 
Ulaya nguo hazianikwi nje ila kuna mashine za kufua na kukamua😅 zikitoka hapo zinakula pasi! Huwez kuta watu wameanika nguo nje ila kwa sisi wazee wa mapokeo tumeiga ramani zile zile bila kujua tunahitaji mazingira yakuanika nguo
 
Ulaya nguo hazianikwi nje ila kuna mashine za kufua na kukamua😅 zikitoka hapo zinakula pasi! Huwez kuta watu wameanika nguo nje ila kwa sisi wazee wa mapokeo tumeiga ramani zile zile bila kujua tunahitaji mazingira yakuanika nguo
Wakati wa ukoloni nyumba walizojenga waliweka sehemu ya kufulia na meza ya pasi tena walichonga ya mbao. Nje waliweka kamba tena mara nyingi zinakua chini ya miti ili nguo zisioteze rangi katika jua kali.
 
Asante kwa bandiko nzuri asubuhi hii, imekua vyema kuweka ukumbusho kwa sisi tunaondea kuwa na makazi.

Nisindikize uzi wako huu kwa picha.

nguo.jpg
6p5.jpg


KUANIKA%2BNGUO%2BGHOROFANI.JPG

KUANIKA%2BNGUO%2BGHOROFANI.JPG
 
Ulaya nguo hazianikwi nje ila kuna mashine za kufua na kukamua😅 zikitoka hapo zinakula pasi! Huwez kuta watu wameanika nguo nje ila kwa sisi wazee wa mapokeo tumeiga ramani zile zile bila kujua tunahitaji mazingira yakuanika nguo
Ulaya mkuu miezi minne au zaidi ni barafu kila sehemu na hauoni jua kabisa. Binafsi mashine za kufulia zipo, lakini baraka ya Mungu ya jua Africa naitumia ipasavyo.
 
Ata sehemu ya kuhifadhi/kutupa taka, kuna ndugu yangu kaweka bonge la garden kuzunguka nyumba ila taka zinamtesa
Na tanuru zuri la kuchomea taka flani au majani pia linatakiwa liwemo.
 
Taabu sio kusahaulika tuu .... pia aina ya nguo zianikwazo apoo

Upite mahali ukute mtu ameanika zile nguo nyeupee/pink/red etc kamba nzimaaa apo mwanaume macho kodooo 🍿
🍿
 
Siku hizi nyumba hazina hata store Wala garage wala sehemu ya kufulia na kunyooshea.

Tunakwama wapi?
Nilibahatika kusoma shule ya RC, ilikua ni wasichana watupu hivyo pichu tulianika kwenye kamba lakini walijenga laundry room, ilikua na makaro na meza za kupigia pasi. Kusema ukweli utaratibu ulikua mzuri sana, pasi zilikua za kutosha na kama hutaki vurugu weekend unawahi mapema laundry.
 
Nilibahatika kusoma shule ya RC, ilikua ni wasichana watupu hivyo pichu tulianika kwenye kamba lakini walijenga laundry room, ilikua na makaro na meza za kupigia pasi. Kusema ukweli utaratibu ulikua mzuri sana, pasi zilikua za kutosha na kama hutaki vurugu weekend unawahi mapema laundry.
MZJ au Kifungilo? Nimevuta picha our schools were so organized and in order.
 
Back
Top Bottom