KERO Sehemu ya kusubiria boti Zanzibar inatia aibu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mamlaka ya bandari Zanzibar sidhani kama haioni hali ya sehemu ya kusubiria boti kwenye bandari yao. Wateja wengi wa boti hupanda economy class ambayo watu wengi husubiria huku kwenye viti vya plastic.

Safari inamtaka mtu afike pale walau lisaa limoja kabla. Hivyo hutumia viti akisubiria safari.

Lakini kwa viti hivi, nadhani mtu atatoka akiwa analia kuhusu makalio yake.

Zanzibar inachukua watalii wengi sana, ni muhimu sehemu ya kusubiri kuvutia kwa kuwa wapo watalii hutumia economy class pia. Hali hii ya kutoboresha huduma nafhani inatuhatibia kama taifa, sifhani kama vile viti ni makumbusho pia.

 
Kwa muonekano hivyo viti vilivunjwa na vitu vigumu kama jiwe/chuma.
Sasa sijui wenzetu huko wana makalio ya ainagani hadi yanavunja plastic ngumu ama fiber
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…