Sekeseke la 'impeachment' limeibuka tena! 25th amendment kutumika?

Sekeseke la 'impeachment' limeibuka tena! 25th amendment kutumika?

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
5,500
Reaction score
8,060
Habari!

Shinikizo jipya sambamba na mashitaka ya kumuondoa madarakani Rais wa Marekani Donald Trump vimeibuka upya na kushika kasi baada ya vurugu zilizozuka hivi karibuni bungeni, Washington DC, ambazo Trump analaumiwa na kushutumiwa kwazo.

Huku hayo yakiendelea, kumekuwa pia na mjadala kuhusu kutumika kwa kifungu cha 25 cha marekebisho ya katiba ya Marekani (25th amendment) dhidi ya Trump, kifungu ambacho kinaweka wazi jinsi Makamu wa Rais na wingi wa mawaziri wanavyoweza kumuondoa rais madarakani pale atakaposhindwa kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa katiba.

Democrats wamekuwa mstari wa mbele kushinikiza kuondolewa kwa Trump madarakani kabla ya muda wake kuisha siku chache zijazo. Baadhi ya viongozi na wanachama wa chama cha Republican nao pia wameonekana kuunga mkono hilo na pia kulaani vikali kitendo cha uvamizi wa bunge.

Mmoja wa viongozi ni Spika wa Baraza la Wawakilishi, Bi Nancy Pelosi, ambaye ofisi yake ilivamiwa na waandamanaji (wahuni), amesema (nanukuu):
Trump has committed an assault on our nation and our people. Pence must remove him and invoke the 25th amendment. If they fail to act, we may be prepared to move forward with impeachment. Justice will be done to those who carried out these acts of sedition and cowardice.
(mwisho wa kunukuu)

Vurumai lililozuka bungeni, Washington DC, hapo jana pia limeondoka na maafisa kadhaa wa serikali ya Trump ambapo baadhi tayari wamekwisha kuachia ngazi huku wengineo kadhaa nao wakitegemewa kufanya hivyo katika wakati ujao.

Msako mkali dhidi ya wale wote waliohusika katika vurugu na uvamizi umeanza ambapo tayari watu kadhaa wamekwisha kukamatwa huku pia shirika la upelelezi la FBI likitoa wito kwa raia wa kuwasilisha taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa wahusika wengine.

Jaribio hili kwa mara nyingine la kumuondoa Trump madarakani kabla ya muda wake kuisha litafanikiwa?

Jawabu la kitendawili hiki tutalipata hapo baadaye na mengine zaidi ya haya tutaendelea kujuzana. So long!
 
Ana siku 13 zimebaki ili aondoke hivyo suala la impeachment halileti tija.

Wakitumia hicho kifungu cha 25 bado Trump anaweza kukipinga kwa kutumia decree hivyo tegemeo lao ni makamu wake bwana Pence ambae anatakiwa aunge mkono juhudi hizo za kumuondoa Trump jambo ambalo Pence hawezi kufanya.

Kichatotakiwa kufanywa kwa sasa ni kwa FBI na ofisi ya AG kutafuta ushahidi wa Trump kuhusika moja kwa moja kuandaa hizo furugu.

Kisha kuwatafuta wahusika wengine wakuu ambao waliratibu furugu hizo ambazo kiusalama ni hatari kwa vile waliingia ofisi Capitol ofisi kubwa ya demokrasia ya Wamarekani na wengine kutinga ofisini kwa bibi Nancy Pelosi.

Huwezi fahamu kama baadhi ya nyaraka muhimu za siri pia zimekuwa compromised.

Hivyo ni vyombo vya ulinzi na usalama kutekeleza kazi yao kwa ueledi uleule badala ya kuzembea kama walivyofanya.
 
Ana siku 13 zimebaki ili aondoke hivyo suala la impeachment halileti tija.

Wakitumia hicho kifungu cha 25 bado Trump anaweza kukipinga kwa kutumia decree hivyo tegemeo lao ni makamu wake bwana Pence ambae anatakiwa aunge mkono juhudi hizo za kumuondoa Trump jambo ambalo Pence hawezi kufanya.

Kichatotakiwa kufanywa kwa sasa ni kwa FBI na ofisi ya AG kutafuta ushahidi wa Trump kuhusika moja kwa kuandaa hizo furugu.

Kisha kuwatafuta wahusika wengine wakuu ambao waliratibu furugu hizo ambazo kiusalama ni hatari kwa vile waliingia ofisi Capitol ofisi kubwa ya demokrasia ya Wamarekani na wengine kutinga ofisini kwa bibi Nancy Pelosi.

Huwezi fahamu kama baadhi ya nyaraka muhimu za siri pia zimekuwa compromised.

Hivyo ni vyombo vya ulinzi na usalama kutekeleza kazi yao kwa ueledi uleule badala ya kuzembea kama walivyofanya.
Umeandika vyema lakini mimi najaribu kuliangalia kwa upande wa pili, Wameamerica waliharibu sana kutumulika kuwa hatuna uhuru wa kutoa maoni, kuandamana ni haki wananchi waachwe waandamane na wakipigwa wanatushutumu kuwa tulimia nguvu sana na wanakaa vikao kutujadili lakini wao jana wamepiga watu risasi ambao hawakuwa wanatumia bunduki
 
Ana siku 13 zimebaki ili aondoke hivyo suala la impeachment halileti tija.

Wakitumia hicho kifungu cha 25 bado Trump anaweza kukipinga kwa kutumia decree hivyo tegemeo lao ni makamu wake bwana Pence ambae anatakiwa aunge mkono juhudi hizo za kumuondoa Trump jambo ambalo Pence hawezi kufanya.

Kichatotakiwa kufanywa kwa sasa ni kwa FBI na ofisi ya AG kutafuta ushahidi wa Trump kuhusika moja kwa kuandaa hizo furugu.

Kisha kuwatafuta wahusika wengine wakuu ambao waliratibu furugu hizo ambazo kiusalama ni hatari kwa vile waliingia ofisi Capitol ofisi kubwa ya demokrasia ya Wamarekani na wengine kutinga ofisini kwa bibi Nancy Pelosi.

Huwezi fahamu kama baadhi ya nyaraka muhimu za siri pia zimekuwa compromised.

Hivyo ni vyombo vya ulinzi na usalama kutekeleza kazi yao kwa ueledi uleule badala ya kuzembea kama walivyofanya.
Trump ametoa speech saa kadhaa zimekwisha kupita na ameweka wazi kuhusu uwepo wa mabadiliko ya uongozi panapo Januari 20.

Maana yake ni kuwa, ameridhia kuondoka mamlakani, akidai kuanza mchakato wa makabidhiano ya madaraka. Pamoja na mengineyo pia ametoa wito wa kuwepo kwa maridhiano ya kitaifa.

Hili linaweza kutuliza zile hasira za wengi na kuzima mijadala ya wasiwasi juu ya uwepo wa mabadiliko ya uongozi. Hivyo, hizi siku chache zilizobaki kwa yeye kuendelea kuwepo mamlakani, pengine zinaweza zikavumilika.
 
Wameamerica waliharibu sana kutumulika kuwa hatuna uhuru wa kutoa maoni, kuandamana ni haki wananchi waachwe waandamane na wakipigwa wanatushutumu kuwa tulimia nguvu sana na wanakaa vikao kutujadili lakini wao jana wamepiga watu risasi ambao hawakuwa wanatumia bunduki
Uhuru wa kutoa maoni, maandamano na mikusanyiko [ya amani] ni haki ya kidemokrasia katika tawala za kidemokrasia.

Panapofanyika uchaguzi, demokrasia inahitaji ama inataka taasisi zenye dhamana na zenye kujitegemea (huru) kutekeleza majukumu yake kwa kuhakikisha maamuzi ya wananchi kupitia sanduku la kura yanasimamiwa ipasavyo. Hapa ndipo penye "uchaguzi huru na wa haki".

Inapotokea upande mmoja kutoridhika kwa kiasi cha kuleta vurugu au machafuko, ni tishio kwa demokrasia. Ndipo inapobidi taasisi yenye dhamana (vyombo vya ulinzi na usalama) kuingilia kati ili kuhakikisha maamuzi ya wanachi yanalindwa na kuheshimiwa na si kuingilia kati na kudhibiti ama kuvuruga uchaguzi.
 
Umeandika vyema lakini mimi najaribu kuliangalia kwa upande wa pili, Wameamerica waliharibu sana kutumulika kuwa hatuna uhuru wa kutoa maoni, kuandamana ni haki wananchi waachwe waandamane na wakipigwa wanatushutumu kuwa tulimia nguvu sana na wanakaa vikao kutujadili lakini wao jana wamepiga watu risasi ambao hawakuwa wanatumia bunduki
Ila mhalifu siku zote huwa hana amani.

Kwanini huwa mnapambana sana kutafuta UHALALI wa upuuzi mnaofanya ???
 
UPDATE: Pelosi says Democrats will move to impeach Trump if he does not 'willingly' resign

On Friday, Speaker Nancy Pelosi said that House Democrats will move to impeach President Trump if he does not "imminently and willingly" resign from office, according to The New York Times, Fox News and other reporters privy to a conference call between the lawmakers.
 
UPDATE: Vice President Mike Pence wants to 'preserve the option' of invoking the 25th Amendment to remove President Trump from office, according to a report from CNN.
 
UPDATE: House Democrats unveil article of impeachment against Trump

House Democrats introduced an article of impeachment against President Trump on Monday, accusing him of inciting insurrection at the Capitol building on January 6. Senate Majority Leader Mitch McConnell told GOP colleagues on Friday that the earliest a Senate trial could likely be held would be on January 19, according to a memo obtained by several news outlets.
 
UPDATE: Pence says he will not invoke the 25th Amendment

Vice President Mike Pence said he will not invoke the 25th Amendment to remove Trump from office, according to a letter sent to House Speaker Nancy Pelosi. A vote for impeachment is expected to take place on Wednesday morning.
 
UPDATE: Pence says he will not invoke the 25th Amendment

Vice President Mike Pence said he will not invoke the 25th Amendment to remove Trump from office, according to a letter sent to House Speaker Nancy Pelosi. A vote for impeachment is expected to take place on Wednesday morning.
Kwa maana hiyo jukumu sasa linabaki kwa congress ku-impeach na ikiwezekana kumuondoa madarakani Rais Donald Trump. Leo kura zinapigwa na house na hoja ikipita, itabidi Senate itoe hukumu. Hakuna aliye juu ya Katiba Marekani.
 
Kwa maana hiyo jukumu sasa linabaki kwa congress ku-impeach na ikiwezekana kumuondoa madarakani Rais Donald Trump. Leo kura zinapigwa na house na hoja ikipita, itabidi Senate itoe hukumu. Hakuna aliye juu ya Katiba Marekani.
Zoezi la kura ya kutokuwa na imani na rais kwa upande wa Baraza la Wawakilishi limekamilika.

Wabunge 232 wameipitisha kura dhidi ya wabunge 197 huku wabunge 10 wa Republican wakiunga mkono sambamba na Democrats katika kura ya kutokuwa na imani na Rais Trump.

On the record: Trump ni rais wa kwanza kuwa 'impeached' mara mbili katika historia ya Marekani.

Zoezi sasa linaelekea katika Bunge la Seneti.
 
Back
Top Bottom