Sekretarieti ya Ajira, mnayajua haya?

Sekretarieti ya Ajira, mnayajua haya?

maiyanga1

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
1,340
Reaction score
1,832
Nimesikitika sana baada ya kusikia kwamba pamoja na ajira zote za umma, ukiacha waalimu, kusimamiwa na tume ya ajira, eti kuna taasisi za umma ambazo usaili ukifanywa na tume ya ajira, bado nazo zinakuwa na vigezo vyake kuwachukua waliopita katika usaili wa tume ya ajira.

Hili likoje?
Mtu anatajiwa vigezo vya kupata ajira, anavitimiza, anafanyiwa usaili, anafaulu kisha akishafika kwenye taasisi anaambiwa hana vigezo vya taasisi.

Mfano, kuna watu walifaulu usaili wa tume ya ajira kufanya kazi TRA/NSSSF mwezi wa pili, wakapelekwa mafunzo miezi mitatu makao makuu, baada ya kupelekwa mikoani wanaambiwa hawana vigezo.

Matokeo yake:
1. Serikali inakuwa imepoteza pesa kumfanyia mtu mafunzo ambayo hatayafanyia kazi
2. Kwenye hizo taasisi watu wanaingiza watoto/jamaa zao ambao aidha walifeli usaili au hawakufanya kabisa.

Wengi wa wanaofanyiwa hivyo ni watoto wa walala hoi ambao hawana mahali pa kukimbilia.

Ndio tulipofikia watanzania.

TUME YA AJIRA MNAYAJUA HAYA?
 
Mkuu, isijekuwa kuna tukio specific unajaribu kulizungumzia, kwamba kuna mtu unayemfahamu alifanyiwa, kama ndivyo kwa nini usiliweke hadharani ili apate msaada kwa wenye mamlaka au umemaanisha inawatokea wengi?

Endapo inawatokea wengi, hebu tugusie baadhi ya vigezo ambavyo taasisi husika huvitumia kuwaondoa sifa waliofanikiwa kupata nafasi kwao.
 
Cha msingi ni labda angetoa taarifa kamili jee huyo mtu alitolewa kwa sababu zipi alivyohoji,,,? nijuavyo mimi HR Ni lazima akukague vyeti na ajilizishe mara nyingi huwa vinatumwa necta,,TCU taarifa za vyeti vyako wakileta mrejesho ndiyo HR anaendelea na hatua inayofuata,,,Je huyo mtu alitolewa katika hatua ipi nadhani huendi semina elekezi bila HR kujilizisha tupe taarifa jee ana cheque no huyo na sababu ni ipi
 
Huwaga kunamakosa hutokea utumishi wanatoa tangazo la Kazi Fulani uwe na certificate baadae wanakupeleka kutokea database unapelekwa sector nyingine uwe na diploma kumbe mtu huyo aliishia certificate

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Cha msingi ni labda angetoa taarifa kamili jee huyo mtu alitolewa kwa sababu zipi alivyohoji,,,? nijuavyo mimi HR Ni lazima akukague vyeti na ajilizishe mara nyingi huwa vinatumwa necta,,TCU taarifa za vyeti vyako wakileta mrejesho ndiyo HR anaendelea na hatua inayofuata,,,Je huyo mtu alitolewa katika hatua ipi nadhani huendi semina elekezi bila HR kujilizisha tupe taarifa jee ana cheque no huyo na sababu ni ipi
Kwa hiyo jamaa huenda walikataliwa coz ya vyeti feki?
 
Nimesikitika sana baada ya kusikia kwamba pamoja na ajira zote za umma, ukiacha waalimu, kusimamiwa na tume ya ajira, eti kuna taasisi za umma ambazo usaili ukifanywa na tume ya ajira, bado nazo zinakuwa na vigezo vyake kuwachukua waliopita katika usaili wa tume ya ajira.

Hili likoje?
Mtu anatajiwa vigezo vya kupata ajira, anavitimiza, anafanyiwa usaili, anafaulu kisha akishafika kwenye taasisi anaambiwa hana vigezo vya taasisi.

Mfano, kuna watu walifaulu usaili wa tume ya ajira kufanya kazi TRA/NSSSF mwezi wa pili, wakapelekwa mafunzo miezi mitatu makao makuu, baada ya kupelekwa mikoani wanaambiwa hawana vigezo.

Matokeo yake:
1. Serikali inakuwa imepoteza pesa kumfanyia mtu mafunzo ambayo hatayafanyia kazi
2. Kwenye hizo taasisi watu wanaingiza watoto/jamaa zao ambao aidha walifeli usaili au hawakufanya kabisa.

Wengi wa wanaofanyiwa hivyo ni watoto wa walala hoi ambao hawana mahali pa kukimbilia.

Ndio tulipofikia watanzania.

TUME YA AJIRA MNAYAJUA HAYA?
Nsssf HV ajira zao ni kama za kupeana tangazo Lao cjawai ona
 
Huwaga kunamakosa hutokea utumishi wanatoa tangazo la Kazi Fulani uwe na certificate baadae wanakupeleka kutokea database unapelekwa sector nyingine uwe na diploma kumbe mtu huyo aliishia certificate

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Kwel limenikuta hilo kwenye ajira za manispaa ya wilaya ya kinondon walitaka mtu mwenye certificate lakin baadae wakageuka kwenye kuitwa kwenye usail sikuitwa nimeletewa sababu pale kwamba chet hakiendan na tangazo la ajira
 
Kwel limenikuta hilo kwenye ajira za manispaa ya wilaya ya kinondon walitaka mtu mwenye certificate lakin baadae wakageuka kwenye kuitwa kwenye usail sikuitwa nimeletewa sababu pale kwamba chet hakiendan na tangazo la ajira
Kuna NTA 4 na NTA 5 hiyo ishu ilishamtokea ndugu yangu ..tangazo liliandika tu wanataka certificate hawakuspecify yeye akaenda na Leve4 akaambiwa chet hakiendan n tangazo wanatakqma level 5
 
Kuna NTA 4 na NTA 5 hiyo ishu ilishamtokea ndugu yangu ..tangazo liliandika tu wanataka certificate hawakuspecify yeye akaenda na Leve4 akaambiwa chet hakiendan n tangazo wanatakqma level 5
Ukiwa na NTA 4 hii inakuwa haijakamilika uwezi ajiriwa popote , NTA 4 ni kama cheti cha msingi kinachokuwazesha au kukupa sifa ya kusoma NTA 5. Hivyo ili kuweze kuajirika lazima uwe na NTA 5 (CERTIFICATE) , au NTA 6 (DIPLOMA) na NTA7 (DIGRII) ukiishia NTA 4 unapewa cheki lakini hakitambuliki kwenye ajira

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom