Selemani Jaffo jiandae Kuulizwa uwe Waziri Mkuu 2020 hadi 2025 uchukue nafasi ya Kassim Majaliwa au uandaliwe kuwa Rais 2025 hadi 2035

Jafo bado mdogo ki umri kuwa PM! U PM unawafaa watu wenye umri mkubwa kidogo angalau kuanzia miaka 50 na kuendelea.

Ukishatumikia cheo cha PM, nafasi inayokufaa baada ya hapo ni Urais au makamu wa rais.

Nikiangalia umri wa SJ bado hajapata mikutuo mingi kwenye utumishi wake na anasafari ndefu ya kuitumikia nchi hii.

Waendelee kumpa uzoefu kwa kuongoza wizara mbalimbali ili apate changamoto zitakazo muimarisha kushika nafasi ya u PM kama wanataka awe PM hapo baadae.

PM wa sasa bado anafaa kutumikia nafasi yake, labda kama ana matatizo kwenye uongozi wake. Binafsi, bado namuona yupo vizuri na anaendana na kasi ya JPM

Nafasi ya uraisi SJ bado haiwezi, ni mwepesi mno! Uwaziri unamfaa. Kingwendu hamuwezi SJ, bado ana nafasi ya kushinda.

Huu ni mtazamo wangu na si vinginevyo!
 
Niliangalia hii habari jana..mbaya zaidi akamtishia kwamba apelekwe halmashauri za mbali kaka Kakonko huko..dah tunajisahau sana binadamu na haya madaraka.
 
Jafo na Hussen ni Presidential material wa baade. Ingawa HM ni mzoefu zaidi
 
Tundu Lissu ni Rais sasa hizo takataka zitashikaje madaraka?
 
MSISHANGAE , ANNA MGWIRA ANAKUWA PREMIER 2020 , AU KA UNA BISHA NJOO INBOX NIKUPE VIDEO CLIPS .
Anna mugwira ametangaza ni ya kugombea ubunge jimbo gani maana waziri mkuu lazima awe mbunge wa kuchaguliwa
 
Endelea Kujidanganya tu na ninakutaarifu hapa hapa kabisa kuwa Majaliwa ana 5% tu za Kurejea kuwa Premier 2020 lakini Jaffo ana zote 95%.
Achana na ramli chonganishi wewe
 
Magufuli katuonyesha CCM ina trouble shooters wengi baada ya kuteua watu tofauti na utaratibu wao ulivyokuwa promote wafia chama kwanza kitu ambacho kilikuwa kinafunika vijana wengine.

Kuna tofauti kubwa sana ya ufanyaji kazi wa mtu kama ‘Mwigulu au Simbachawene’ ambao wapo kiofisi ofisi zaidi; ukilinganisha na watu kama ‘Jaffo, Bashe au Biteko’ ambao ni ‘hands on’ maeneo waliyopewa kundi la pili unaona impact zao.

Vijana wanaojiona CCM mali yao wengi ovyo kweli kwenye uongozi ni watu wa majivuni hawana hari ya kujituma wala kuacha alama mwenye tofauti kidogo January but he lucks original ideas.

Binafsi ningependa kuona Dotto Biteko nayeye anapewa wizara yenye mikiki siku moja kama uchukuzi, maji au kokote kwenye kupambana na watendaji naamini serikalini huko ndio kwenye changamoto kubwa zaidi. Kwa wafanyabiashara na madini tushaona talent yake.
 
Jafo na Hussen ni Presidential material wa baade. Ingawa HM ni mzoefu zaidi
Hwafai,Jaffo alibariki wizi uchaguz serikali za mitaa.Ni wa Ovyo.Hussein Mwinyi is GOOOOD
 
Kuanzia sasa Ndugu Selemani Jaffo jiandae kuwa na Majibu Kamili juu ya hayo Mambo Mawili makubwa niliyokuambia katika headline yangu hapa.
kama unawaza magufuli kushinda uchaguzi huu basi ondoa mawazo hayo ya sijui waziri mkuu,sijui Jafo, Magufuli anaenda kuwa rais wa mileld nchi hii
 
Acheni kujaza watu upepo. Majaliwa bado yupo yupo sana
 
Kuanzia sasa Ndugu Selemani Jaffo jiandae kuwa na Majibu Kamili juu ya hayo Mambo Mawili makubwa niliyokuambia katika headline yangu hapa.

Umetumwa? Au anampumulia dadiyo!
 
Binafsi siwezi kuja huko Inbox Kwako kwa Mambo ya Kipuuzi ambayo yanatoka kwa Watu wa Vijiweni tu. Jaffo ni ama Premier au President period.
Marais wa nchi watakua wanatoka sehemu hizo hizo tu? Pwani na Kanda ya ziwa? Nchi hii yetu sote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…