MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,675
- 33,583
Wakuu,
Senga na Pembe wanafahamika miaka mingi kwa umahiri wao wa vichekesho. Kwa miaka mingi ni kama walipotea na kuibuka kizazi kipya kilichofanya wengi kuwasahau.
Wakongwe hawa wameingia kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni na kujipatia followers wengi kwa haraka tofauti na matarajio ya wengi na bila promotion kubwa zaidi ya video zao za vichekesho kusambaa na kuwashtua watu uwepo wao.
Kiukweli hawa wakongwe uchekeshaji hawalazimishi na kuna kila dalili wamepata mwanzo mpya walau nao waonje matunda ya sanaa yao. Kwa uelekeo wao wa sasa naamini wamepata uongozi ambao umetambua namna ya kuyafufua madini haya ya kale.
Kupitia Senga na Pembe naamini pengine hata akina Mzee Jangala wamekosa muongozo tu lakini wangeweza kuburudisha hata kizazi hiki.
Nawatakia heri wakongwe hawa ambao ni kama walishapotea kwenye sanaa za vichekesho.
Senga na Pembe wanafahamika miaka mingi kwa umahiri wao wa vichekesho. Kwa miaka mingi ni kama walipotea na kuibuka kizazi kipya kilichofanya wengi kuwasahau.
Wakongwe hawa wameingia kwenye mitandao ya kijamii hivi karibuni na kujipatia followers wengi kwa haraka tofauti na matarajio ya wengi na bila promotion kubwa zaidi ya video zao za vichekesho kusambaa na kuwashtua watu uwepo wao.
Kiukweli hawa wakongwe uchekeshaji hawalazimishi na kuna kila dalili wamepata mwanzo mpya walau nao waonje matunda ya sanaa yao. Kwa uelekeo wao wa sasa naamini wamepata uongozi ambao umetambua namna ya kuyafufua madini haya ya kale.
Kupitia Senga na Pembe naamini pengine hata akina Mzee Jangala wamekosa muongozo tu lakini wangeweza kuburudisha hata kizazi hiki.
Nawatakia heri wakongwe hawa ambao ni kama walishapotea kwenye sanaa za vichekesho.