Separatus Fella awaasa Watumishi wa Umma kuhusu Ulevi na Rushwa

Separatus Fella awaasa Watumishi wa Umma kuhusu Ulevi na Rushwa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-10-16 at 13.50.38_26f8db83.jpg

Separatus Fella

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imetoa Mafunzo Elekezi ya Awali kwa Watumishi wapya 80 ambao wameajiriwa hivi karibuni ikiwa ni Mpango unaoandaliwa na Idara ya Utawala na Rasilimaliwatu katika kuwaandaa waajiriwa wapya kuendana na Misingi ya Maadili ya Utendaji kazi katika Utumishi wa Umma.

Akifungua Mafunzo hayo huku akimwakilisha Katibu Mkuu, Katibu wa Sekretarieti ya Kuzuia na Kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu, Separatus Fella amewataka watumishi hao wapya kujiepusha na masuala ya kupokea rushwa na Tabia Za Kilevi ambazo ni kinyume na maadili ya utumishi wa umma.

Mafunzo hayo ya siku nne yanafanyika Jijini Dodoma huku mada mbalimbali ikiwemo elimu ya afya, elimu ya ustaafu,utoaji huduma na muundo wa Serikali na jinsi inavyofanya kazi kufikisha huduma kwa wananchi.

WhatsApp Image 2024-10-16 at 13.50.41_66c4e25e.jpg

WhatsApp Image 2024-10-16 at 13.50.39_1776ac13.jpg

WhatsApp Image 2024-10-16 at 13.50.40_d221b4ea.jpg

WhatsApp Image 2024-10-16 at 13.50.42_8dc8a9ae.jpg
 
Hiv kilá watumishi wapya pamoja na walimu wanafanyiwa hivi au hizi ni Special kada?
 
Back
Top Bottom