autorun255, kusema kuwa Korea Kaskazini hawana hata timu ni kulikosea heshima Taifa hilo TUKUFU, kuukosea heshima umma wa wanasoka, umma wa wajamaa, kumkosea heshima Kim Jong-un, Kiongozi Mkuu wa Korea DPR, Chama cha Wafanyakazi cha Korea DPR, ambacho Kim ni Katibu wake, Jeshi la Watu wa Korea DPR, ambalo Kim ni Amiri Jeshi wake Mkuu, Chama cha Kikomunisti cha Korea DPR, ambacho Kim ni Mwenyekiti wake, Chama cha Soka cha nchini humo, wachezaji 23 wa sasa wanaounda timu ya taifa (ambayo kwa mujibu wako haipo) pamoja na dawati lao la ufundi.
Naomba utumie nguvu ile ile uliyotumia kutufedhehesha kututaka radhi wadau wa humu mchezoni, ututake radhi wajamaa na ulitake radhi taifa Tukufu la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Korea, au Korea Kaskazini kama unavyowaita.
Naomba umtake radhi Kiongozi wa Taifa hili, Kim Jong-un, yeye pamoja na Serikali yake kwa udhalilishaji huu uliouleta humu kuhusu soka la nchini mwake.
Zaidi ya yote ningependa ukitake radhi Chama cha Wafanyakazi cha Korea DPR, ambaco Kim ni Katibu wake, Ulitake radhi Jeshi la Watu wa Korea DPR, ambalo Kim ni Amiri Jeshi wake Mkuu, ukitake radhi Chama cha Kikomunisti cha Korea DPR, ambacho Kim ni Mwenyekiti wake, Chama cha Soka cha nchini humo, wachezaji 23 wa sasa wanaounda timu ya taifa (ambayo kwa mujibu wako haipo) pamoja na dawati lao la ufundi.
Mwisho kabisa ukiri udhaifu wako wa kutegemea taarifa za kupewa na mabeberu, na uwe tayari kuanza hatua nyingine ya kufunguliwa mawazo.
Nasubiri mrejesho wako!
Waione,
Gang Chomba,
Makoye Matale,
mwangalingimungu