Septemba 03, 2021, Bondia Hassan Mwakinyo anataraji kupambana na Bondia kutoka Namibia Julius Munyelele Indongo

Septemba 03, 2021, Bondia Hassan Mwakinyo anataraji kupambana na Bondia kutoka Namibia Julius Munyelele Indongo

poposindege

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
453
Reaction score
175
Septemba 03, 2021, Bondia Hassan Mwakinyo anataraji kupambana na Bondia kutoka Namibia Julius Munyelele Indongo mwenye umri wa miaka 38 katika pambano la kugombea mkanda wa ABU (African Boxing Union) uzito wa Super Welter katika ukumbi wa Kilimanjaro Hall, Ubungo Plaza, Dar-Es-Salaam.

Rekodi ya Bondia Julius Indongo amepigana mapambano 26, ameshinda 23 na kupigwa 3 yote kwa KO na hana droo. Katika mapambano yake manne ya mwisho ameshinda moja kwa TKO na kupigwa matatu kwa KO.

Pambano lake la mwisho ni November 27, 2020 dhidi ya Daniyar Yeleussinov ambalo alipigwa kwa TKO.

Kumbukumbu zinaonesha mwaka 2015 Machi 20 alipigana na Bondia Ibrahim Class huko kwao Namibia katika ukumbi wa Ramatex Factory, Windhoek na akashinda kwa pointi kwa kupewa ushindi na majaji wote. Mcheza kwao hutunzwa. Nyumbani bondia anapoteza kwa KO sio Pointi.

Ni bondia anayetumia staili ya Southpow. Kwa uoni wangu ni Bondia mtelezo kama ganda la ndizi kwa Mwakinyo. Hamalizi Raundi Tano atakua ameshakalishwa chini. Tutafute mabondia wazuri zaidi wa kumchallenge bondia wetu.

Indongo-700x350.jpg
 
Mwakinyo na uongozi wake me ata siwaelewi, Tangu kijana wetu afanye vizuri lile pambano la kwa malkia kusema ukweli hakuna nia ya dhati ya wao kutaka Mwakinyo azidi kukua kimchezo, maana amekuwa anatafuta mabondia uchwara na kuwapiga ilhali hawampi faida yoyote kwenye career yake

Aliposhinda dhidi ya mwingereza ilitakiwa ndio iwe njia ya yeye kupanda duniani kwa kutafuta mapambano na maboxer walio bora, badala yake amekuwa mtu wa mipasho tu mara yeye ndio Tanzania one, mara ye ndo vile ilhali hakuna ata bondia mmoja aliepigana nae tena ambae yuko juu yake, analetewa mabondia wastaafu ili awapige azidi kuvimba kichwa

Laiti kama angeitumia vozuri ile nafasi aliyoipata mwanzo leo hii angekuwa anaongelewa na mapromota wakubwa duniani, na kwakuwa hataki kupigana na mabondia bora me naweza kusema kuwa kumpiga yule mwingereza ilikuwa ni kama fluke tu au mtaani wanaita ndondokela, Anyway naheshimu uwezo wake

Sent from my M2101K7AG using JamiiForums mobile app
 
Upo sahihi mkuu.

Kinachofanyika ni kumpa mapambano.

Ya kawaida ili kulinda status yake ya ushindi bila ya kuangalia kumpandisha zaidi kuwa bora na ghali zaidi.

Yule promota/meneja aliye kuwa nae wakati wa ushindi kule UK. Ni mjanja angemsaidia sana kupenya Ulaya na America.

Baada ya ushindi akawa anatafsiri sivyo maneno ya Mwakinyo kwamba anamtaka bondia fulani (sikumbuki jina) ili acheze nae.

Alikua anataka kumpeleka mbele ili awe bondia mwenye thamani wapige pesa ndefu zaidi.
 
Upo sahihi mkuu.

Kinachofanyika ni kumpa mapambano
Ya kawaida ili kulinda status yake ya ushindi bila ya kuangalia kumpandisha zaidi kuwa bora na ghali zaidi.

Yule promota/meneja aliye kuwa nae wakati wa ushindi kule UK. Ni mjanja angemsaidia sana kupenya Ulaya na America.

Baada ya ushindi akawa anatafsiri sivyo maneno ya Mwakinyo kwamba anamtaka bondia fulani (sikumbuki jina) ili acheze nae.

Alikua anataka kumpeleka mbele ili awe bondia mwenye thamani wapige pesa ndefu zaidi.
Wanakosea sana, watabaki kujigamba tu kuwa yeye ni bondia bora kwa sasa Tanzani, bondia anaelipwa vizuri Tanzania ila akiwa hana CV yoyote kubwa duniani.

Sent from my M2101K7AG using JamiiForums mobile app
 
Mwakinyo anapigana uzito wa Super Welter na Ibra Class uzito wa Super feather
Na kisheria wanaweza kukutana?maana Mwakinyo anaenda kupambana na mtu aliyepigana na Ibra Class
 
Hii tabia ya kuleta vinyozi haitamsaidia bondia huyu kujua
 
Na kisheria wanaweza kukutana?maana Mwakinyo anaenda kupambana na mtu aliyepigana na Ibra Class
Ndo kawaida ya Mwakinyo, dhaifu, undersize na wazee na wapinzani wake.
 
Na kisheria wanaweza kukutana?maana Mwakinyo anaenda kupambana na mtu aliyepigana na Ibra Class
Super feather ni uzito wa kg 57 mpaka 59 na super Welter ni uzito wa kg 67.

Wanaweza kupambana iwapo mmoja atakwenda kwenye uzito wa mwenzie.


Vinginevyo ngumu kupambana mabondia wa uzito tofauti.
 
Back
Top Bottom