Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,662
- 6,888
Ni vyema tusijadili sera mpya ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 kabla ya kuisoma na kuielewa. Mfano kwenye lugha ya kufundishia, sera imeshindwa kuchagua lugha ya Kiswahili pekee kuwa ya kufundishia and kujifundishia. Badala yake sera imeweka lugha zote mbili - Kiswahili na Kiingereza kuwa za kufundishia na kujifundishia katika ngazi zote za elimu na mafunzo (angalia attachment ukurasa kati ya 35 n 38)
Pia sera imeonesha umuhimu wa lugha zote mbili na kusema wazi ili kuingia kwenye anga za kimataifa English ni muhimu. Halafu eti Kiswahili na chenyewe kinaenea kwenye mabara.
Cha kushangaza ni kuwa sera imeshindwa kutoa uelekeo katika hili, nafikiri inaziachia taasisi husika za elimu kuamua kama ilivyo sasa kwa baadhi ya pre-primary and primary kutumia lugha ya Kiingereza kama medium of instruction!
Pia sera imeonesha umuhimu wa lugha zote mbili na kusema wazi ili kuingia kwenye anga za kimataifa English ni muhimu. Halafu eti Kiswahili na chenyewe kinaenea kwenye mabara.
Cha kushangaza ni kuwa sera imeshindwa kutoa uelekeo katika hili, nafikiri inaziachia taasisi husika za elimu kuamua kama ilivyo sasa kwa baadhi ya pre-primary and primary kutumia lugha ya Kiingereza kama medium of instruction!