Asha Abdala
JF-Expert Member
- Mar 21, 2007
- 1,130
- 45
Ameongea point,ila sijajua kama kweli hiyo sera inaweza kupandikizwa ktk muda huu na katika chama ambacho hakina sera kama hizo.
Pia tukiangalia pemba utakuta hakuna matawi au hakuna influenceya CHADEMA.Sasa hiyo sera wata-impliment vipi?
Ameongea point,ila sijajua kama kweli hiyo sera inaweza kupandikizwa ktk muda huu na katika chama ambacho hakina sera kama hizo.
Pia tukiangalia pemba utakuta hakuna matawi au hakuna influenceya CHADEMA.Sasa hiyo sera wata-impliment vipi?
1. Suala la Mfumo Mpya wa Utawala ni suala la Kikatiba ambalo linaamuliwa kwa mabadiliko ya Katiba. Hakuna eneo moja la nchi pekee lenye uamuzi wa mwisho kuhusu katiba ya nchi.
2. Chama cha siasa hakina hatimiliki dhidi ya sera, yoyote yule aliyeko madarakani anaweza kutekeleza sera yoyote.
Cha msingi tu cha kujadili nini matakwa ya umma na nini maono ya viongozi- na hatima ya yote ni nini makubaliano ya pamoja(ama wakati mwingine ya wengi) kuhusu muundo na mwelekeo wa Taifa
JJ
1. Suala la Mfumo Mpya wa Utawala ni suala la Kikatiba ambalo linaamuliwa kwa mabadiliko ya Katiba. Hakuna eneo moja la nchi pekee lenye uamuzi wa mwisho kuhusu katiba ya nchi.
2. Chama cha siasa hakina hatimiliki dhidi ya sera, yoyote yule aliyeko madarakani anaweza kutekeleza sera yoyote.
Cha msingi tu cha kujadili nini matakwa ya umma na nini maono ya viongozi- na hatima ya yote ni nini makubaliano ya pamoja(ama wakati mwingine ya wengi) kuhusu muundo na mwelekeo wa Taifa
JJ
Zemarcopolo, je ni kwanini unaona sera ya majimbo haitekelezeki?
Je ni kwa visiwani tu au hata bara?
Haika,
Mfumo wanaoutaka CHADEMA wa majimbo hauelezei clearly nafasi ya Zanzibar katika mfumo huo, ila ukitaka kuona jinsi sera hii isivyotekelezeka angalia mfano huu:
Sera inataka kusiwe na cheo cha Rais wa Zanzibar na badala yake kuwe na mawaziri wakuu wawili, mmoja wa Unguja na mwingine wa Pemba.
Sasa fikiria, wakati wa uchaguzi mkuu tunachagua Rais wa Jamhuri na Rais wa Zanzibar then baada ya kuwaapisha tu Rais wa Jamhuri anakuja na agenda ya kuondoa cheo cha Rais wa Zanzibar ambaye ndio kwanza ameapishwa.
Kumbuka pia katika uchaguzi wa 2005 CHADEMA Zanzibar kura walizopata hazifi hata 0.5% ya kura zote! Kwa hiyo logical assumption will be that Rais wa Zanzibar atakuwa ametoka chama kingine, which means chama hicho urais wa Zanzibar ndio itakuwa ngome yake ya kushikilia angalau sehemu ya madaraka ya nchi baada ya urais wa Jamhuri kuchukuliwa na CHADEMA.Unaweza kuimagine response ya serikali ya Zanzibar na watu wake juu ya hili?Unaweza kuimagine kiasi cha muda na resourses nyingine zinazohitajika kushughulikia hili?
kumbuka kuwa CHADEMA hawana mkakati wowote wa kutawala nchi bila kuwepo mfumo wa majimbo, which means muda wote wa kutatua hili swala zima la kuunda serikali linakuwa linasubiri kwanza.
Ndio maana nasema sera hii haitekelezeki na CHADEMA kwa kuendelea kushikilia sera hii inadhihirisha kuwa haiko tayari kuongoza nchi.
Huo ni mfano mmoja tu, ila mapungufu ni mengi mno.na imedhihirika hapa kuwa CHADEMA wenyewe hawana mkakati wowote wa kushughulikia hili, ndio maana mjadala huu ukijitokeza viongozi wao hawatoi majibu ya maswali ya msingi. Jibu lao kila siku ni kubadilisha katiba, wanajua kuwa kubadilisha katiba hakuna guarantee.
Sasa iwapo ikishindikana kubadili katiba, why there is no plan B???Na wakati tunasubiri kubadili katiba nchi itaongozwa kwa mfumo gani na kwa muda gani?
Maswali haya ndani ya CHADEMA hayajapatiwa majibu.Ni vyema majibu hayo wayatafute mapema na kuyaweka hadharani la sivyo kila mtu atatafuta jibu lake mwenyewe, kwa mfano jibu nililojitafutia mimi ni kwamba CHADEMA ni wasanii ambao wanajua kuwa hawatapata nafasi ya kuongoza nchi kwa hiyo hawajisumbui kutafuta majibu ya maswali magumu juu ya kuongiza nchi.
Cha Msingi ni kujadili dhana ya federalism, ni aina gani ya ufiderali kwa muundo upi hilo ndio suala ambalo nimesema hapa ni la kikatiba.
Kwamba bila sera ya majimbo CHADEMA haitaweza kuongoza dola, hilo si kweli. Kumbuka kubadili mfumo wa utawala ni suala moja tu katika sera na za CHADEMA na hata katika ilani yake.
Kwa hiyo, hata bila ya mfumo wa majimbo CHADEMA itatekeleza ajenda zake za kisiasa ambazo zinakusudiwa katika kuleta mabadiliko katika taifa letu mathalani rejea http://www.chadema.net/maoni/ilani.php
Ila tunasisitiza kwamba mabadiliko ya kimfumo na kitaasisi kupitia katiba mpya, yatawezesha mabadiliko kufanyika kwa haraka na urahisi zaidi.
Kupitia misingi hii muhimu ambayo nakumbuka niliwahi kuichambua kidogo miaka kadhaa nyuma kupitia makala yangu haya: http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_18.html
Kilichowasilishwa Mwanza ni rasimu sifuri ya mawazo ya Timu maalum iliyofanya uchambuzi. Chama kama taasisi kinaendelea kuchukua maoni ya watu mbalimbali. Kwa hiyo endelea kutoa maoni yako tu. Siku chama kitakapofanya uzinduzi wa sera hii inayofanyiwa marejeo, mara baada ya kupitishwa na vikao vya kikatiba. Unaweza kutupima vizuri zaidi.
JJ