Sera ya Vyuo Vikuu kubakiza wahitimu wenye ufaulu wa juu badala ya kuajiri wasomi walio- practice unaathri ubora wa elimu inayotolewa vyuoni

Sera ya Vyuo Vikuu kubakiza wahitimu wenye ufaulu wa juu badala ya kuajiri wasomi walio- practice unaathri ubora wa elimu inayotolewa vyuoni

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Utaratibu huu ambao ndio kama sera ya vyuo vikuu vingi nchini kiliwemo Chuo Kikuu cha Dar -es-Salaam, sio tu umepitwa na wakati, bali pia haufai kwani unachangia vyuo kuwa na walimu ambao hawaja-practice katika field wanazofundisha na hivyo kuzalisha wasomi wenye kukosa maarifa na uzoefu kutoka kwa watu waliofanya kazi kwenye field husika.

Utaratibu huu ulifaa miaka ya nyuma ambapo wasomi walikuwa ni wachache lakini sio leo hii ambapo wasomi ni wengi wakiwemo waliofanya kazi katika field husika.

Mtu ambae amemaliza chuo na kupata first class kisha akaunganisha masters na baadae PhD ila hajafanya kazi katika field husika, sidhani kama anaweza kuwa mwalimu mzuri zaidi ya kubobea kwenye theory tu.

Pamoja na uwepo wa mafunzo kwa vitendo baada ya theory za darasani wakati wa likizo, bado kuna umuhimu mkubwa wa taaluma katika vyuo vyetu kutolewa na watu wenye sifa na moja ya sifa ya ziada ila muhimu ni walimu wawe walau wamefanya kazi katika field wanayofundisha.

Najua kwa baadhi ya field inaweza kuwa ni changamoto kupata na kuajiri wataalamu /wasomi wa kufundishia walioko katika field, ila vyuo bado vinaweza kutenga muda wa wataalamu hawa kuja kutoa mihadhara kwa utaratibu wa part- time vyuoni.

Tukikubali kutazama upya utaratibu huu na kuufanyia marekebisho kadri inavyowezekana, bila shaka tutakuwa na nafasi ya kuzalisha wasomi wazuri wanaoweza kushindana na wasomi kutoka katika mataifa mengine katika soko la ajira na hata katika kujiajiri.

Elimu yetu sehemu kubwa ni theory, na walimu wetu ambao nao ni zao la theory wanafundisha bila hata ku-practice field husika, halafu eti tunatarajia tuweze kuwa na wahitumu wenye viwango! Itawezekana kweli?

Tujitafakari.
 
Mkuu rejea kwenye msingi wa vyuo vikuu. Kazi ya vyuo vikuu sio kuandaa practioners bali critical thinkers! Haya ya practical yako vyuo vya kati.
Na ndio maana kwa sasa serikali inapeleka wahitimu wengi wa kidato cha nne wenye ufaulu wa kati mf. DIV 2 dhaifu na DIV 3 vyuo vya kati kusoma Diploma.

Huko ndio kwa kuzalisha fundi mchundo/ wasaidizi wa madaktari, mainjinia, wahasibu etc. Tatizo hapo kati tulidhani degree ni kwaajili ya kila mtu, sera ikawa kuongeza vyuo ili watu wapate degree. Hata wasio na uwezo wakaenda degree ya kwanza na ya pili ... wakasoma kwa shida kiasi lecturers wakaonekana wanawaonea.

WaTZ tumesahau kuwa mwanafunzi unatakiwa ku fit kwenye mfumo wa chuo lakini siyu chuo kijishushe ili kuendana na sifa za wanafunzi vilaza. Hao vilaza wetu wakaajiriwa maofisini wakashindwa ku perform, wengine hata kujenga hoja kwenye vikao hawawezi.

Angalia bungeni, wasomi waliotakiwa kuwa critical thinkers hawawezi hata kujenga hoja, hata huo ujasiri hawana. Hao ndio watu tuliowalazimisha wapate degree wakati hawakustahili
 
Mkuu rejea kwenye msingi wa vyuo vikuu. Kazi ya vyuo vikuu sio kuandaa practioners bali critical thinkers! Haya ya practical yako vyuo vya kati.
Unaikumbuka ile professorial rubbish?Unadhani moja ya chanzo cha report za aina ile ni nini?
 
Athari nyingine ni ku-recycle knowledge zile zile. Mtu kasomea UD undergraduate anarudi hapo kufundisha mwanafunzi, naye mwanafunzi wake anarudi tena kufundisha hapo hapo. Kama mwalimu wa kwanza kuna kitu kilikuwa kinamsumbua, unageuka ugonjwa wa kizazi, ni bora wangekuwa hata wana-exchange kati ya chuo na chuo
 
Wengi wanaenda nje kusoma PhD wakimaliza wanarudi humu nchini wanaendelea kufundisha.
Naona umefuta ule ujinga ulioandika mwanzoni, vizuri sana. Shida ni iko wapi kama hawa watu wanasoma huku wanafanya tafiti na kuandaa machapisho ??? Nadhani wewe unahisi kwamba utaalamu wa mwanazuoni unaangaliwa kwa kufundisha. HELL NO, tunampima mwanazuoni kwa uwezo wake binafsi wa kufanya tafiti na kuandaa machapisho.

Utaratibu wa TCU ni kwamba kila mwajiriwa ni lazima aandae machapisho kadhaa yaliyofanyiwa utafiti wa kutosha kisha kupitishwa ili yawekwe kwenye majarida ya kitaaluma (Academic Journals). Sasa unavyolalamika kwamba watu wanaenda kusoma nje PhD sikuelewi kabisa na nimekushangaa.

Kwasababu hata ukienda huko nje kusoma PhD hasa vyuo vya Magharibi utasaidia tu kufundisha aidha kwenye semina na kusimamia tafiti (Dissertations) za wanafunzi wa madaraja ya chini. Tena huko nje ndiyo kusikie tu, haukai tu unasoma muda wote. Utafanya workshops, consultancy, symposium, tutoring etc........
 
Ukutane nao darasani sasa walivyo na mbwembwe kumbe wazee wa kumeza, kuna walimu wangu pale Mlimani nna hasira nao mpaka kesho, japo nnapanga kurudi hapo kuongeza elimu sijui nikikutana nao itakuaje maana wengi wana Phd sasahivi
 
Back
Top Bottom