Serekali haikusanyi kodi ipasavyo

Serekali haikusanyi kodi ipasavyo

Ngolombwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2013
Posts
267
Reaction score
76
Ndugu zangu wanajukwaa, kwanza nawapa pole sana kwa majukumu mengi na magumu ya kulijenga Taifa Letu, ambalo mpaka leo linaitwa Taifa changa.
Pamoja na hayo yote, tumezidi kushuhudia jinsi nchi yetu inavyokosa kuhudumia raia wake ipasavyo kwa kisingizio cha kukosa fedha. Huduma za muhimu kama maji, barabara, afya na nyinginezo hazipatikani na kama kuna juhudi basi tunaambiwa serekali imekopa kwa wahisani au tumepewa misaada na wafadhili, Rais wetu amekuwa msafiri mashuhuri akizunguka kuomba hiyo mikopo na ufadhili wa miradi ambayo, ambayo hata baada ya kuipata kuisimamia ili iwanufaishi wananchi inakuwa shida kubwa. Tumekuwa tukishhudia mkaguzi wa mahesabu ya serekali akitoa taarifa ya wizi wa mabilioni kila mwaka na hakuna hatua za kuridhisha zunazochukuliwa, wanasiasa wetu waliopo serekalini wamekuwa wakitueleza jinsi wanavyojitahidi kupunguza tatizo hilo lakini mafanikio yake kama yapo basi ni kidogo mno.
Pamoja na hayo yote, serekali yetu haikusanyi kodi kwa umakini hata kidogo, nimeshuhudia kwa macho yangu wafanya biashara wengi wakikwepa kodi kwa kisingizio cha mashine ya tra imeharibika na mara nyingine hali hiyo inakuwa hata wiki mbili, mfano nzuri ni vituo vya mafuta (petrol stations ) nyingi hazitumii mashine hizi kwa maelezo kuwa zimeharibika, pia maduka ya spare za pikipiki, na magari pale kariakoo ama hupati kabisa hizo risiti za tra na au ukipewa basi gharama ya risiti hiyo hailingani na kiasi cha pesa ulicholipa. Sehemu nyingine ni mpaka uombe risiti ndipo unaambiwa kama unahitaji ni lazima uongeze pesa. Je serekali yenye kujali raia wake haijui haya yote? Au ndyo vile mwalimu Nyerere alivyosema kuwa serekali corrupt haikusanyi kodi!!! Badala yake inawaandama wamachinga tu?
Nawasilisha.
 
Hii hoja ni muhimu, tuijadili kwa kirefu. Ngolombwe ametoa mifano mizuri tu. Tungewasaidia TRA na serikali kama tungejikita katika kutoa mifano. Kwangu hoja kubwa ni je, makampuni makubwa (achana na ya madini kwa sasa) yanalipa kodi ipasavyo? Hao mabilionea wa Tanzania na Afrika kama walivyotangazwa na gazeti maarufu la Forbes, wanalipa? Kama ndiyo, wanalipa kulingana na mapato yao? Tatizo ni matakwa ya sheria kwamba mambo ya kodi ni kati ya mlipaji na mkusanyaji! Hoja yangu: Turekebishe sheria kuondoa usiri huo kwani ndio pia mwanya wa rushwa. Let tax payments be in the public domain; tujue nani analipa nini!
 
Hii hoja ni muhimu, tuijadili kwa kirefu. Ngolombwe ametoa mifano mizuri tu. Tungewasaidia TRA na serikali kama tungejikita katika kutoa mifano. Kwangu hoja kubwa ni je, makampuni makubwa (achana na ya madini kwa sasa) yanalipa kodi ipasavyo? Hao mabilionea wa Tanzania na Afrika kama walivyotangazwa na gazeti maarufu la Forbes, wanalipa? Kama ndiyo, wanalipa kulingana na mapato yao? Tatizo ni matakwa ya sheria kwamba mambo ya kodi ni kati ya mlipaji na mkusanyaji! Hoja yangu: Turekebishe sheria kuondoa usiri huo kwani ndio pia mwanya wa rushwa. Let tax payments be in the public domain; tujue nani analipa nini!

Sioni sababu ya mlipa kodi afanyiwe siri katika kodi anayolipa, uwazi kwenye kodi ni nyenzo muhimu ya kupiga vita rushwa, na hasa kwenye nchi ndogo makini zinazotaka kupiga hatua za maendeleo kwa haraka kama nchi yetu, lazima dubadili sheria zetu, lakini pia utamaduni wetu wa kulipa kodi ni lazima uendene na dhamira yetu ya maendeleo, na wakusanya kodi ni lazima wajue kuwa kodi si mali yao ni mali ya wananchi wote hivyo wana wajibu wa kufanya hivyo kwa uwazi na ukweli. Lakini pia wananchi tubadilike tudai risiti kwa malipo yetu halali, swala la msamaha wa kodi ni muhimu kulipitia upya ili sasa walipa kodi wote wajue kuwa hakuna msamaha wa kodi, na makampuni makubwa yawe wazi kwa biashara yao.
 
Back
Top Bottom