Sergio Aguero: Man City striker charged with violent conduct over Winston Reid elbow

Sergio Aguero: Man City striker charged with violent conduct over Winston Reid elbow

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Manchester City striker Sergio Aguero has been charged with violent conduct by the Football Association for elbowing West Ham's Winston Reid.

Aguero could face a three-match ban, including City's Premier League games with Manchester United on 10 September and Bournemouth on 17 September.

The 28-year-old would also miss the EFL Cup third-round game against Swansea.

Aguero is out of Argentina's two World Cup 2018 qualifiers next month with a calf injury.

Referee Andre Marriner did not see the 76th-minute incident during City's 3-1 win on Sunday and the FA has decided to take retrospective action after reviewing television footage.

Aguero has until 18:00 BST on Wednesday, 31 August to respond.
 
Mshambuliaji wa Man City Sergio Kun Aguero afungiwa, kuikosa Man United
sergio-aguero-manchester-city_3002134.jpg

Sergio Aguero


MANCHESTER, ENGLAND

NYOTA wa klabu ya Manchester City, Sergio Aguero, ameanza msimu vibaya baada ya usiku wa juzi kuamkia jana kupewa adhabu na Chama cha Soka nchini England (FA).

Mshambuliaji huyo hatari ambaye amekuwa akitoa mchango mkubwa hasa katika michezo miwili ya awali ya Ligi Kuu kwa kuifungia jumla ya mabao matatu, lakini mchezo huo wa juzi ulikuwa mgumu kwake katika dakika ya 75 baada ya kumchezea vibaya nyota wa West Ham, Winston Reid.

Kupitia mikanda ya video, Aguero alionekana akimpiga kiwiko beki huyo wa klabu ya West Ham wakati akiwania mpira katika mchezo ambao ulimalizika kwa Manchester City kushinda mabao 3-1.

Kutokana na kusambaa kwa video hiyo, chama cha soka nchini England kimeamua kumfungia mchezaji huyo michezo mitatu kwa madai ya utovu wa nidhamu uwanjani.

Mwamuzi wa mchezo huo, Andre Marriner, amedai kuwa hakuwa mbali na eneo la tukio lakini hakukiona kiwiko hicho ila aliona kuwa Aguero amemchezea vibaya mpinzani wake na kupigwa mpira wa adhabu.

Kutokana na hali hiyo ya Aguero kufungiwa michezo mitatu, ina maana nyota huyo ataukosa mchezo muhimu dhidi ya wapinzani wao, Manchester United kwenye uwanja wa Old Trafford, Septemba 10 mwaka huu.

Michezo mingine miwili ambayo ataikosa mchezaji huyo ni pamoja na Bournemouth, kabla ya kwenda kwenye uwanja wa Liberty kuvaana na Swansea City.

Hata hivyo, kocha wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola, amedai kuwa tukio ambalo amelifanya mshambuliaji wake katika mchezo huo hakuliona, hivyo anashindwa kulizungumzia.

“Sikuona chochote alichokifanya Aguero, hivyo siwezi kuelezea lolote, nadhani hakuna ambacho alikifanya, lakini kama kweli kuna kitu kibaya amefanya basi lazima tukubali.

“Hata kama tutamkosa Aguero katika mchezo dhidi ya wapinzani wetu Manchester United, lakini ushindi ni pale pale, akili yangu kwa sasa inawaza mchezo huo hivyo sina wasiwasi kumkosa Aguero,” alisema Guardiola.

Hata hivyo, kwa upande wa kocha wa West Ham, Slaven Bilic, amedai kuwa hata yeye hakuliona vizuri tukio hilo na suala la kumtoa mchezaji wake lilikuwepo kabla ya tukio lenyewe.

“Sikuamua kumbadilisha Winston Reid kutokana na kuchezewa vibaya, nilifanya hivyo kwa kuwa ulikuwa ni wakati sahihi wa kufanya hivyo,” alisema Bilic.

Kocha huyo amedai kuwa wapinzani wake walistahili kushinda kutokana na soka ambalo wameonesha kwa kuwa waliweza kufika kila wakati katika lango.

"Hii inaonekana kwa mashabiki wa upande wa pili na timu yao kwa ujumla imekuwa ahuweni kwao" kwa sababu Mshambuliaji hatari hatokuwepo hiyo siku watakapokutana, hivyo "wamejihakikishia ushindi ni lazima"

Ahsanteni.
 
Pole sana Aguero, Nakweli imekua ahuweni, washindwe wenyewe sasa, tena nasikia huko uingereza wamefanya na pati.
 
Bado ana nafasi ya kujitetea na hukumu bado haijatolewa

Hiyo haeding yako mkuu dah
 
Back
Top Bottom