Serikali amkeni, BASATA amkeni, RITA nao wanatuongopea?

Serikali amkeni, BASATA amkeni, RITA nao wanatuongopea?

MT255

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2012
Posts
3,606
Reaction score
4,914
Okay, Kuna watu wanataka ku-prove kuhusu hizo taarifa za umri wa Miss wetu fuata hizi steps, ni simple ingia https://i94.cbp.dhs.gov/, then chini chagua I agree, bofya proceed halafu ikifunguka jaza majina ya Miss wetu wa nguvu, weka passport number yake, chagua Tanzania then get travel history, utapata details zake.

Sisi Watanzania tunachotaka ni kuonyesha umma wa Tanzania wenzetu kua kuna watu wachache wanajaribu kupindisha ukweli kua mrembo huyu kadanganya umri kwa sababu anazojua yeye, sasa tunaomba taasisi husika zichukue hatua stahiki ili iwe fundisho kwa watakaofuata.

Neno letu kwa wadhamini Redds kueni na msimamo na msiharibu image yenu nzuri ya product yenu mlioijenga kwa gharama kubwa ili heshima yenu iendelee kuwepo mbele ya jamii, la sivyo tutawaona na nyie mmeshiriki kwa kuandaa na kukubaliana na taarifa za uongo ili kuwahadaa Watanzania wazalendo wenye moyo wa upendo na amani.

Na nyie RITA, inashangaza sana taasisi kubwa na nyeti ya serikali inatoa vyeti bila kufuata taratibu za kisheria zilizowekwa. Tujiulize hivi kuna wakina Sitti wangapi wamepata vyeti vya kuzaliwa vya mipango? Sitti amefoji cheti ili awadanganye Kamati ya Miss Tanzania, Na je hao wengine waliolipa hivyo vyeti unajua lengo Lao?

Mpaka hapa serikali kupitia BASATA mnahitaji ushahidi gani mwingine ili muamini huyo Miss katengenezwa na Lundenga? tunaomba Serikali kupitia wizara yake ya Michezo na Utamaduni,BASATA amkeni onyesheni uhai.

Hizi ni salamu zangu

#bringbackourcrown
 

Attachments

  • 1414123917620.jpg
    1414123917620.jpg
    96.2 KB · Views: 549
  • 1414123930504.jpg
    1414123930504.jpg
    56.9 KB · Views: 507
  • 1414123954074.jpg
    1414123954074.jpg
    60.4 KB · Views: 496
  • 1414123968374.jpg
    1414123968374.jpg
    91.1 KB · Views: 482
Mkuu unatutaftia ugomvi na ehh! Hyo website mbona ina onyo kali sana juu ya kusearch watu ambao hawakuhusu ?? Wanasema kama unataka kupata details za mtu unaemchunguza au vip tuma email usitumie website unavunja kiapo
 
Huyu dada hata haoni aibu? Watu wa uhamiaje wamfate wamuulize alipata wapi passport yenye umri mkubwa kuliko ilivyo kwenye cheti chake cha kuzaliwa
 
Laana za baba ake hizo kwa vilio vya watanzania waishiao uarabuni pesa zote za BMK atamalizia kujisafisha na mwanae.
 
dawa hapa ni kutuma hizi data huko miss world, tupuuzie hii rotten system hakuna haki nchi hii
 
:what::what::what:
 

Attachments

  • 1414146989936.jpg
    1414146989936.jpg
    21.8 KB · Views: 206
Huyu Sitti apunguze mkorogo hadi mashavu yameshaanza kumshuka na bado analilia udogo solution hapo ni kutuma malalamiko miss world nchi hii wasivo fuatilia.malalamiko ya wananchi watabebana kirushwa bora tufungiwe kabisa kushiriki hyo miss world na hapo ukute wana foji pasport nyingine kama waliweza cheti cha kuzaliwa
 
Back
Top Bottom