Serikali: Hatuna mfumo wa ukaguzi wa madereva wa mabasi ya shule

Serikali: Hatuna mfumo wa ukaguzi wa madereva wa mabasi ya shule

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo amesema wizara walitoa mwongozo wa mabasi ya shule na kwamba waliviachia vyombo vingine vya Serikali kuendelea na ukaguzi wa madereva hao kama wanavyofanya kwa madereva wengine na hawakuwahi kuwa na mfumo.

“Baada ya uzoefu huu tutatafakari, namna gani nzuri tutaangalia dereva yupi atafaa kubeba watoto ni suala ambalo sasa tulifikirie kwa umbali zaidi kama Serikali tunapaswa kufanya nini katika suala hili.

“Katika mifumo ya kiserikai tayari dereva awe amekidhi vigezo lakini sasa utahitajika ukaguzi zaidi kwa madereva wa watoto, kulitafakari kwa pamoja na vyombo vingine na kulitolea msimamo. Kama kutakua na uhitaji wa kuongeza sifa za ziada kupitia mifumo ya serikali,” amesema Profesa Nombo.

Miongoni mwa ajali hizo ambazo inadaiwa imesababishwa na uzembe wa dereva ni ya gari Toyota Hiace la Shule ya Msingi Ghati Memorial, kuangukia kwenye korongo lililojaa maji eneo la Dampo mkoani Arusha.

Katika maelezo yake, Profesa Nombo amesisitiza ili dereva aweze kukabidhiwa gari la wanafunzi lazima awe na vigezo na kazi ya trafiki ni kuwakagua kama wana vigezo na kupitia mchakato wa kuwa dereva.

“Madereva wanaobeba watoto wa shule, wanapaswa wawe makini zaidi tunategemea aliyekabidhiwa jukumu hilo, atazingatia kulinda uhai wa wale anaowabeba,” amesema.

Mwongozo

Waraka wa Elimu Na. 01 wa mwaka 2023 kuhusu uboreshaji wa huduma ya magari au mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi, ulioanza kutumika Machi Mosi 2023 ulielekeza umakini kwa wamiliki wa shule kwa kuwa kuwa thamani ya rasilimali watoto ni kubwa kuliko thamani ya rasilimali yoyote ambayo nchi imejaliwa kuwa nayo.

Waraka huo uliolenga kuboresha utoaji wa huduma ya usafiri wa magari na mabasi kwa wanafrunzi uliwataka kuzingatia kutokuwepo kwa viashiria vyovyote vya ukatili dhidi ya wanafunzi ikiwemo ubakaji na ulawiti na tabia zenye viashiria vya mmomonyoko wa maadili.

“Tabia hizi zinaleta mmomonyoko wa maadili, kuathiri ukuaji, ujifunzaji na kuhatarisha ustawi wa watoto kwa ujumla. Haitakiwi kuwa na wahudumu jinsi moja ya wanaume pekee, kuweka miziki au nyimbo au picha za video zisizozingatia maadili, mila na destrui na tamaduni, kuwafanyia vitendo vya ukatili,” ulielekeza.

Mwongozo huo uliosainiwa na Kamishna wa Elimu, Dk Lyabwene Mtahabwa ulielekeza shule kuwa na ratiba rafiki za safari ili wanafunzi hususani watoto wadogo wapate muda wa kutosha kupumzika kwa ajili ya ukuaji wao.

Pia, uliekeza kuwa na mabasi yenye vioo angavu, wamiliki kuhakikisha wanaowaajiri wawe waaminifu, wenye weledi na maadili.

“Endapo mhudumu yeyote ataenda kinyuma na maadili au kuhatarisha usalama wa wanafunzi, mmiliki wa shule achukue hatua mara moja dhidi ya mtumishi husika.”

PIA, SOMA:
 
Nashauri madereva wote wa school bus wawe "matured" na wawe na familia. Hawa masela mavi ndio shida hawajui uchungu wa mtoto.
 
School inapita unakuta imefunguliwa miziki amapiano na singeli watoto ndani wanaimbishwa, watoto wanaruka wanaimba huku hawana habari.

Ova
 
Hakuna kazi ya ovyo kama hii!! Dereva anaamshwa saa 11 alfajiri, hana posho wala nini mwisho wa mwezi ndo apewa laki 2 au 3!! Just imagine!!!
 
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo amesema wizara walitoa mwongozo wa mabasi ya shule na kwamba waliviachia vyombo vingine vya Serikali kuendelea na ukaguzi wa madereva hao kama wanavyofanya kwa madereva wengine na hawakuwahi kuwa na mfumo.

“Baada ya uzoefu huu tutatafakari, namna gani nzuri tutaangalia dereva yupi atafaa kubeba watoto ni suala ambalo sasa tulifikirie kwa umbali zaidi kama Serikali tunapaswa kufanya nini katika suala hili.

“Katika mifumo ya kiserikai tayari dereva awe amekidhi vigezo lakini sasa utahitajika ukaguzi zaidi kwa madereva wa watoto, kulitafakari kwa pamoja na vyombo vingine na kulitolea msimamo. Kama kutakua na uhitaji wa kuongeza sifa za ziada kupitia mifumo ya serikali,” amesema Profesa Nombo.

Miongoni mwa ajali hizo ambazo inadaiwa imesababishwa na uzembe wa dereva ni ya gari Toyota Hiace la Shule ya Msingi Ghati Memorial, kuangukia kwenye korongo lililojaa maji eneo la Dampo mkoani Arusha.

Katika maelezo yake, Profesa Nombo amesisitiza ili dereva aweze kukabidhiwa gari la wanafunzi lazima awe na vigezo na kazi ya trafiki ni kuwakagua kama wana vigezo na kupitia mchakato wa kuwa dereva.

“Madereva wanaobeba watoto wa shule, wanapaswa wawe makini zaidi tunategemea aliyekabidhiwa jukumu hilo, atazingatia kulinda uhai wa wale anaowabeba,” amesema.

Mwongozo

Waraka wa Elimu Na. 01 wa mwaka 2023 kuhusu uboreshaji wa huduma ya magari au mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi, ulioanza kutumika Machi Mosi 2023 ulielekeza umakini kwa wamiliki wa shule kwa kuwa kuwa thamani ya rasilimali watoto ni kubwa kuliko thamani ya rasilimali yoyote ambayo nchi imejaliwa kuwa nayo.

Waraka huo uliolenga kuboresha utoaji wa huduma ya usafiri wa magari na mabasi kwa wanafrunzi uliwataka kuzingatia kutokuwepo kwa viashiria vyovyote vya ukatili dhidi ya wanafunzi ikiwemo ubakaji na ulawiti na tabia zenye viashiria vya mmomonyoko wa maadili.

“Tabia hizi zinaleta mmomonyoko wa maadili, kuathiri ukuaji, ujifunzaji na kuhatarisha ustawi wa watoto kwa ujumla. Haitakiwi kuwa na wahudumu jinsi moja ya wanaume pekee, kuweka miziki au nyimbo au picha za video zisizozingatia maadili, mila na destrui na tamaduni, kuwafanyia vitendo vya ukatili,” ulielekeza.

Mwongozo huo uliosainiwa na Kamishna wa Elimu, Dk Lyabwene Mtahabwa ulielekeza shule kuwa na ratiba rafiki za safari ili wanafunzi hususani watoto wadogo wapate muda wa kutosha kupumzika kwa ajili ya ukuaji wao.

Pia, uliekeza kuwa na mabasi yenye vioo angavu, wamiliki kuhakikisha wanaowaajiri wawe waaminifu, wenye weledi na maadili.

“Endapo mhudumu yeyote ataenda kinyuma na maadili au kuhatarisha usalama wa wanafunzi, mmiliki wa shule achukue hatua mara moja dhidi ya mtumishi husika.”

PIA, SOMA:
 
Hakuna kazi ya ovyo kama hii!! Dereva anaamshwa saa 11 alfajiri, hana posho wala nini mwisho wa mwezi ndo apewa laki 2 au 3!! Just imagine!!!
Asili ya mwanadamu ni kutolingana.
Wenzio hiyo laki 2-3 wanatunza familia zao.
 
Hii ajali kwa kweli LATRA wanatakiwa kutoa tamko, sio kubaki ofisni tu.
 
Hakuna kazi ya ovyo kama hii!! Dereva anaamshwa saa 11 alfajiri, hana posho wala nini mwisho wa mwezi ndo apewa laki 2 au 3!! Just imagine!!!
Kwani ukiwa na boda au taxi huwezi kupiga kazi baada ya kuwapeleka watoto?
Mda wa kuwachukua ukifika unawaendea au haliwezekani
 
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Carolyne Nombo amesema wizara walitoa mwongozo wa mabasi ya shule na kwamba waliviachia vyombo vingine vya Serikali kuendelea na ukaguzi wa madereva hao kama wanavyofanya kwa madereva wengine na hawakuwahi kuwa na mfumo.

“Baada ya uzoefu huu tutatafakari, namna gani nzuri tutaangalia dereva yupi atafaa kubeba watoto ni suala ambalo sasa tulifikirie kwa umbali zaidi kama Serikali tunapaswa kufanya nini katika suala hili.

“Katika mifumo ya kiserikai tayari dereva awe amekidhi vigezo lakini sasa utahitajika ukaguzi zaidi kwa madereva wa watoto, kulitafakari kwa pamoja na vyombo vingine na kulitolea msimamo. Kama kutakua na uhitaji wa kuongeza sifa za ziada kupitia mifumo ya serikali,” amesema Profesa Nombo.

Miongoni mwa ajali hizo ambazo inadaiwa imesababishwa na uzembe wa dereva ni ya gari Toyota Hiace la Shule ya Msingi Ghati Memorial, kuangukia kwenye korongo lililojaa maji eneo la Dampo mkoani Arusha.

Katika maelezo yake, Profesa Nombo amesisitiza ili dereva aweze kukabidhiwa gari la wanafunzi lazima awe na vigezo na kazi ya trafiki ni kuwakagua kama wana vigezo na kupitia mchakato wa kuwa dereva.

“Madereva wanaobeba watoto wa shule, wanapaswa wawe makini zaidi tunategemea aliyekabidhiwa jukumu hilo, atazingatia kulinda uhai wa wale anaowabeba,” amesema.

Mwongozo

Waraka wa Elimu Na. 01 wa mwaka 2023 kuhusu uboreshaji wa huduma ya magari au mabasi yanayotumika kusafirisha wanafunzi, ulioanza kutumika Machi Mosi 2023 ulielekeza umakini kwa wamiliki wa shule kwa kuwa kuwa thamani ya rasilimali watoto ni kubwa kuliko thamani ya rasilimali yoyote ambayo nchi imejaliwa kuwa nayo.

Waraka huo uliolenga kuboresha utoaji wa huduma ya usafiri wa magari na mabasi kwa wanafrunzi uliwataka kuzingatia kutokuwepo kwa viashiria vyovyote vya ukatili dhidi ya wanafunzi ikiwemo ubakaji na ulawiti na tabia zenye viashiria vya mmomonyoko wa maadili.

“Tabia hizi zinaleta mmomonyoko wa maadili, kuathiri ukuaji, ujifunzaji na kuhatarisha ustawi wa watoto kwa ujumla. Haitakiwi kuwa na wahudumu jinsi moja ya wanaume pekee, kuweka miziki au nyimbo au picha za video zisizozingatia maadili, mila na destrui na tamaduni, kuwafanyia vitendo vya ukatili,” ulielekeza.

Mwongozo huo uliosainiwa na Kamishna wa Elimu, Dk Lyabwene Mtahabwa ulielekeza shule kuwa na ratiba rafiki za safari ili wanafunzi hususani watoto wadogo wapate muda wa kutosha kupumzika kwa ajili ya ukuaji wao.

Pia, uliekeza kuwa na mabasi yenye vioo angavu, wamiliki kuhakikisha wanaowaajiri wawe waaminifu, wenye weledi na maadili.

“Endapo mhudumu yeyote ataenda kinyuma na maadili au kuhatarisha usalama wa wanafunzi, mmiliki wa shule achukue hatua mara moja dhidi ya mtumishi husika.”

PIA, SOMA:
Waanze na vibali vya shule kumiliki usafiri kulingana na idadi ya wanafunzi.


Shule ina hiace moja yenye uwezo wa kubeba watu 15 mfano, halafu ina wanafunzi 200 wanaotegemea kuitumia kila siku asubuhi na jioni.

1. Lazima wabanane ili kusave mafuta
2. Lazima dereva aende mwendo kasi ili kuokoa muda na wanafunzi kuwahi shule.

Ajali nyingi za shule hutokea asubuhi na sio jioni
 
Back
Top Bottom