KERO Serikali ifuatilie Chuo cha Maendeleo ya wananchi Same, hawatoi vyeti kwa wakati

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Great_j

New Member
Joined
Oct 29, 2023
Posts
3
Reaction score
0
Tunaiomba Serikali kupitia Wizara husika ijaribu kufatilia chuo hiki kuna kila dalili za kutokuwajibika kwa watumishi wake na kutokutumia madaraka yao vyema, wapo wanafunzi waliowahi kusoma chuoni hapo mwaka 2020-2021 mpaka hivi sasa hawajapatiwa vyeti vyao na wakiuliza hakuna majibu ya kuridhisha mda mingine hata kupewa maneno yasiyofaa.

Je, tunawaandaaje hawa vijana tunaosema ni wa taifa la kesho wakajiajiri na wasingoje kuajiriwa? Au kulikuwa na umuhimu gani kuwapa mafunzo haya na mwisho kuwanyima vyeti? Au kuna utaratibu umebadilika kupata cheti mpaka utoe pesa?

Vyeti ni haki yao.

 
Hilo suala umeripoti hapo chuoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…