Serikali iheshimu suala nyeti la Katiba

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Naiomba sana Serikali ya chama changu. Iheshimu suala hili nyeti la katiba mpya. Katiba ni moyo wa nchi. Si jambo la kuletewa mzaha na maigizo. Nimesikitishwa sana na nilichoshuhudia kuhusu nakala za Katiba Inayopendekezwa. Kimeniuma sana. Nimelia kuililia nchi yangu inayoelekea shimoni.

Nimeshuhudia nakala za katiba zikiwafikia wananchi. Nimeshuhudia wananchi wakisoma kwa zamu,kwa saa chache,halafu nakala hiyohiyo kuhamishwa kwenda nyumba nyingine. Nimeshuhudia Katiba Inayopendekezwa ikisomwa kama gazeti. Nikalia sana.

Nimesikitishwa na mtazamo wa Serikali kuwa wananchi wanatakiwa kuiona na kuisoma tu Katiba Inayopendekezwa. Si kuielewa ili kuchagua upande sahihi kwenye kura ya maoni. Huu ni mtazamo hasi na wenye ukakasi. Ni mtazamo wa kiutani,kisanii na kimaigizo. Katiba ni nyaraka ya kisheria. Hata wasomi wenyewe waweza kuisoma na wasielewe. Seuse wananchi wa kawaida?

Serikali,tafadhalini,muwe makini. Kucheza na Katiba ni kuchezea moyo wa Tanzania. Tujirekebishe na tustopishe hima!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Hivyo ndivyo serikali ilivyokusudia tangu mwanzo...waananchi wasiisome, na hata kama wakiisoma wasielewe. Kuna picha moja inazunguka humu jamvini inaonyesha mtu anasoma hiyo katiba huku ameigeuza. Picha hiyo inaeleza yote kuhusu uelewaji wa wananchi kuhusu katiba hii. Wananchi wanatakiwa/wanalazimishwa waipigie kura ya ndio, watake wasitake. Hata humu jamvini wamemiminwa vijana tele kuipigia debe debe katiba hiyo. Ila ukiandika kuikataa katiba hiyo utatukanwa wewe! Sasa sijui kwa matusi makubwa hivyo watanishawishi vipi kuipigia hiyo katiba kura ya ndio!
 
Wananchi hawatakiwi kuielewa. We unadhani wakiielewa wataipigia kura ya ndiyo? Kinachofanyika ni maigizo ya kuwaridhisha waangalizi wa kimataifa. Wananchi wengi hata kutafsiri biblia (msahafu) hawawezi sembuse lugha ya kisheria. Watawala wanajua walichokusudia hivyo wako tayari ipite hata kwa mtutu wa bunduki.
 
.....karibuni mwaka 1998 nilimsikia waziri mmoja akisema katiba ni nyaraka ya serikali haichezewi!.....nchi hii ina maigizo.Waswahili wengi!.
 
hii nchi inakosa mwelekeo kutokana na uwingi wa viongozi wasio na matamanio yakutatua hoja na kubaki ktk ulafi wa madaraka
 
hii nchi inakosa mwelekeo kutokana na uwingi wa viongozi wasio na matamanio yakutatua hoja na kubaki ktk ulafi wa madaraka

so what? Soma katiba inayopendekezwa sura ya nne, ibara ya 28-31 utaona inavyozungumzia mambo mbalimbali ya maadili na miiko ya uongozi, hivyo katiba hii ndo itakayotatua matatizo haya yote!!
 

Mapambano Yetu! Wewe naamini ni kati ya watu wachache wenye maoni hasi na hatima ya nchi yako. Hivi kweli unaweza kulinganisha maisha yako na maigizo? Usiwatukane Watanzania nakuwafananisha na kuwaita kwamba wao ni miongoni mwaWananchi wengi ambao hata kutafsiri biblia (msahafu) hawawezi. Kwanini unawalazimisha kuwa hawawezi kuelewa? Hayo ni matusi kwa wananchi na dharau kubwa sana.


Waheshimu Watanzania wao ni wazalendo kwa nchi yao ndiyo maana wamnasema “KWA KUWA,sisi wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayoheshimu na kuzingatia misingi ya utu na udugu, uhuru, kujitegemea, haki, usawa, amani na utulivu, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu” Ni wenye mapenzi mema tu na nchi yao ndiyo wanajali kupiga hatua mbele na siyo kurudi nyuma kama wewe unavyotaka kuwa kikwazo cha nchi yako kupiga hatua. Nawasihi Watanzania wasibezwe kwa namna yeyote na watu ambao naamini hawana nia ya dhati kujenga Tanzania kwa maslahi wengi.
 


Sio suala la kuiomba Serikali soma katiba pendekezwa, elewa subiri hamasisha ndugu zako kupiga kula nyingi kelele za nini?
 
hii nchi inakosa mwelekeo kutokana na uwingi wa viongozi wasio na matamanio yakutatua hoja na kubaki ktk ulafi wa madaraka


Uwiii kweli umekata tamaa wewe mwenyewe afu unasema nchi imekosa mwelekeo wakati wewe ndio umekosa mwelekeo na hujui unachokifanya humu, ngoja nikuonee huruma nikusaidie; Ni rahisi tu isome katiba pendekezwa uielewe afu ukaipigie kura ya NDIYO utarudi kwenye reli tu.
 


Naona account yako umeianzisha maalum kwaajili ya kutetea upumbavu unaofanywa na serikali. Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu asiyeelewa wingi wa watanzania wasiokuwa na uwezo wa kuielewa katiba kulinganisha na wenye uwezo huo. Kama Kinana aliwauliza maji na katiba wanataka nini wakasema maji, sasa kuna uelewa hapo?
 


chama chako kipi kama wewe ni mzalendo na hauna hila wala unafiki ndani yako ungekitaja na ungekua mkweli kuliko kupotosha umma unatushawishi na kutuona hatuna akilini ya kupambanua, eti tumetakiwa kuiona na kuisoma then what? Acha uongo watanzania tuna akilini na tuko timamu wewe na tunajua kusoma na kupambanua acha kulazimisha hoja!!
 


haikuhusu jenga hoja tukutane,afu nakushangaa utafikiri unaishi somalia unashindwa kuelewa unabaki kupinga kila kitu kinachopita mbele yako, usitafute huruma kwa watanzania kwa taarifa yako watanzania wanaelewa sana kuliko unavyofikiri wewe na ndio maana tuko hapa, tena wana fikiri sawasawa na wanamaamuzi sahihi kwa nchi yao kama huna hoja bora upishe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…