Tetesi: Serikali imeamua kutotenga fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa!

Tetesi: Serikali imeamua kutotenga fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Habari kutoka chanzo kinachoaminika ndani ya serikali zinaonyesha kwamba serikali ya awamu ya tano imeendeleza dhana ya kutokuwa na huruma kwa wahanga wa matukio ya maafa kama matetemeko na mafuriko, kwa kuwa kwa makusudi kabisa imeamua kutotenga fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa nchini. Imesemwa kwamba mfuko huo hauna fedha za kuweza kufanya jambo lolote la maana kwa ajili ya maafa nchini.

Habari znasema kwamba wananchi wanaokumbwa na maafa kama mafuriko yanayoendelea wasitegemee msaada wowote toka serikalini kwa sababu serikali iliamua hata kukitokea maafa ya namna gani wananchi wanapaswa kusimama kwa miguu yao wenyewe, au kusaidiwa na ndugu zao lakini sio serikali. Hili lilionekana kuwa ndio msimamo wa serikali ya awamu ya tano pale wananchi wa Kagera walipokumbwa na maafa ya tetemeko, ambapo Raisi Magufuli aliweka wazi kwamba serikali isingetoa msaada kwa wananchi, na fedha za misaada zingeelekezwa sehemu nyingine sio kuwasaidia wananchi.

IKiwa hili likithibitishwa kuwa kweli, basi ni jambo la kujiuliza ni kwa nini Wabunge hawakuhoji jambo hili Bungeni kwamba kama taifa tunaishi kwa kudura za mwenyezi Mungu bila kuwa na fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa! Ikumbukwe kwamba fedha za mfuko wa maafa si kwa ajili tu ya kuwasiaidia wananchi, bali pia kuendesha kampeni za uokoaji na hata kutoa huduma za dharura kwa wahanga wa maafa. Ni ajabu kwamba serikali haijaona hilo kuwa jambo la muhimu.

Ieleweke kwamba wananchi wanapokumbwa na maafa kama mafuriko, sio tu wanapoteza nyumba zao, bali pia akiba yote ya chakula. Kutarajia kuwa wananchi watajitegemea bila msaada wa serikali katika mazingira kama hayo ni kuwaonea.

upload_2018-5-7_18-5-49.png
 
Huu uzi muda si mrefu utakuwa banned

Kwa ajili ya ukweli kuwa serikali imekataa kutenga fedha za maafa? Labda mtu atuwekee ukweli kulingana na bajeti ya serikali iliyopo.
 
Habari kutoka chanzo kinachoaminika ndani ya serikali zinaonyesha kwamba serikali ya awamu ya tano imeendeleza dhana ya kutokuwa na huruma kwa wahanga wa matukio ya maafa kama matetemeko na mafuriko, kwa kuwa kwa makusudi kabisa imeamua kutotenga fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa nchini. Imesemwa kwamba mfuko huo hauna fedha za kuweza kufanya jambo lolote la maana kwa ajili ya maafa nchini.

Habari znasema kwamba wananchi wanaokumbwa na maafa kama mafuriko yanayoendelea wasitegemee msaada wowote toka serikalini kwa sababu serikali iliamua hata kukitokea maafa ya namna gani wananchi wanapaswa kusimama kwa miguu yao wenyewe, au kusaidiwa na ndugu zao lakini sio serikali. Hili lilionekana kuwa ndio msimamo wa serikali ya awamu ya tano pale wananchi wa Kagera walipokumbwa na maafa ya tetemeko, ambapo Raisi Magufuli aliweka wazi kwamba serikali isingetoa msaada kwa wananchi, na fedha za misaada zingeelekezwa sehemu nyingine sio kuwasaidia wananchi.

IKiwa hili likithibitishwa kuwa kweli, basi ni jambo la kujiuliza ni kwa nini Wabunge hawakuhoji jambo hili Bungeni kwamba kama taifa tunaishi kwa kudura za mwenyezi Mungu bila kuwa na fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa! Ikumbukwe kwamba fedha za mfuko wa maafa si kwa ajili tu ya kuwasiaidia wananchi, bali pia kuendesha kampeni za uokoaji na hata kutoa huduma za dharura kwa wahanga wa maafa. Ni ajabu kwamba serikali haijaona hilo kuwa jambo la muhimu.

Ieleweke kwamba wananchi wanapokumbwa na maafa kama mafuriko, sio tu wanapoteza nyumba zao, bali pia akiba yote ya chakula. Kutarajia kuwa wananchi watajitegemea bila msaada wa serikali katika mazingira kama hayo ni kuwaonea.

View attachment 769271
Tuwafanyaje?,mkiambiwa muondoke maeneo hatarishi hamtaki,"prevention is better than cure"
 
Habari kutoka chanzo kinachoaminika ndani ya serikali zinaonyesha kwamba serikali ya awamu ya tano imeendeleza dhana ya kutokuwa na huruma kwa wahanga wa matukio ya maafa kama matetemeko na mafuriko, kwa kuwa kwa makusudi kabisa imeamua kutotenga fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa nchini. Imesemwa kwamba mfuko huo hauna fedha za kuweza kufanya jambo lolote la maana kwa ajili ya maafa nchini.

Habari znasema kwamba wananchi wanaokumbwa na maafa kama mafuriko yanayoendelea wasitegemee msaada wowote toka serikalini kwa sababu serikali iliamua hata kukitokea maafa ya namna gani wananchi wanapaswa kusimama kwa miguu yao wenyewe, au kusaidiwa na ndugu zao lakini sio serikali. Hili lilionekana kuwa ndio msimamo wa serikali ya awamu ya tano pale wananchi wa Kagera walipokumbwa na maafa ya tetemeko, ambapo Raisi Magufuli aliweka wazi kwamba serikali isingetoa msaada kwa wananchi, na fedha za misaada zingeelekezwa sehemu nyingine sio kuwasaidia wananchi.

IKiwa hili likithibitishwa kuwa kweli, basi ni jambo la kujiuliza ni kwa nini Wabunge hawakuhoji jambo hili Bungeni kwamba kama taifa tunaishi kwa kudura za mwenyezi Mungu bila kuwa na fedha kwa ajili ya mfuko wa maafa! Ikumbukwe kwamba fedha za mfuko wa maafa si kwa ajili tu ya kuwasiaidia wananchi, bali pia kuendesha kampeni za uokoaji na hata kutoa huduma za dharura kwa wahanga wa maafa. Ni ajabu kwamba serikali haijaona hilo kuwa jambo la muhimu.

Ieleweke kwamba wananchi wanapokumbwa na maafa kama mafuriko, sio tu wanapoteza nyumba zao, bali pia akiba yote ya chakula. Kutarajia kuwa wananchi watajitegemea bila msaada wa serikali katika mazingira kama hayo ni kuwaonea.

View attachment 769271
Sio tu elimu ya uokoaji shughuli kama kuipa uwezo jamii uwezo wa namna ya kujikinga, kujiandaa na namna ya kukabiliana na maafa ni sehemu ambayo nchi nyingi zinawekeza ili kuwapatia wananchi wake uwezo wa kuhimili majanga yanapotokea! Iwapo ni kweli hii tetesi basi hata wabunge hawana uelewa juu ya mzingo wa maafa!
 
Kwa hiyo yule mkurugenzi bwana Bashiri Taratibu, anaekaimu ile idara ya maafa pale ofisi ya waziri mkuu atakua anafanya nini?
 
Tetesi za kibarudhuli hizi...ninavyofahamu serikali imepitia Sera ya maafa na kuiboresha.
Kwa sasa Sera sio kutoa msaada wa majanga tu bali kuzuia,kufuatilia na kukabiliana na majanga.

Kajifunze kitu kinaitwa One health approach...hii ni sehemu ya mkakati huo
 
Kwa bajeti ya ofisi ya waziri mkuu imesemaje yeye ndio mwenyekiti wa kamati ya maafa,acheni kulishana matango pori
 
Sawa Mungu wetu haamini katika ajali. Nyie wenye mapepo ndio mnaleta maafa
 
Back
Top Bottom