Serikali imedanganya umma? Bei elekezi za Barakoa na Sukari zashindikana

Serikali imedanganya umma? Bei elekezi za Barakoa na Sukari zashindikana

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Bei ya jumla ya Sukari ni Tsh 2800/= kwa kilo moja, hii ni kwa DSM, lakini katika hali ya kushangaza serikali inawataka wafanyabiashara wa reja reja waiuze kwa Tsh 2600/= kwa kilo moja, hili jambo halitawezekana hata kwa mtutu wa bunduki, hivi sasa sukari madukani imefichwa na wafanyabiashara ili kuepuka hasara ya kijinga.

Hali hii imejitokeza kwenye biashara ya Barakoa, serikali iliacha box lenye barakoa 50 (surgical mask) kupanda kutoka 8500/= hadi 120, 000/= halafu leo inatangaza barakoa moja iuzwe kwa Tsh 1500/=, hili jambo halitawezekana kamwe kwa sababu hakujawahi kutokea bidhaa iliyonunuliwa kwa laki na 20 iuzwe elfu 75, hii ni biashara kichaa, vinginevyo na hizo barakoa nazo zitatoweka mubaki kuvaa barakoa za vitenge kama alivyoshauri RC wa DSM Makonda.

Kwa ufupi sana ni kwamba Wizara ya viwanda na biashara ni kama haina Waziri, ni heri enzi za Mwijage kuliko sasa.

PIA SOMA:
Serikali yatangaza bei ya kikomo ya Sukari; ipo kati ya Tsh. 2,600 na Tsh. 3,200 kwa kilo kutegemea na Mkoa - JamiiForums
 
Yaani bado unaisubiri Serikali kwenye hili suala. Mawaziri wanashauri Watu waachwe wanaopata wapate wasiopata korona Basi heri yao ila shughuli ziendelee Kama kawaida. By Kigwangalla
 
Erythrocyte,
Usanii mtu!
Utawekaje bei elekezi wakati you dont control neither demand nor supply.
Bwana mdogo Bashu azalishe mwenyewe sukari na kuuza kwa hiyo bei, haoni wenziwe wakihangaika na Fosi akaunti?
 
Kwa ufupi sana ni kwamba Wizara ya viwanda na biashara ni kama haina Waziri, ni heri enzi za Mwijage kuliko sasa.
Badala ya kulia mtandaoni ungekuja na majina ya walanguzi ili tuwashughulikie
 
Hii kazi ya kuagiza sukari wangewapa wafanyabiashara kwa kuwashindanisha bila hivyo bei haitashuka wala haya makampuni hatataongeza uzalishaji
 
Back
Top Bottom