Serikali imeondoa gharama za vipimo kwa wajawazito

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Serikali chini ya Rais Samia Suluhu imetangaza kuwa vipimo vya awali kwa wajawazito ambavyo vitahusisha kupima wingi wa damu, mkojo ili kuangalia wingi wa protin, Shinikizo la damu pamoja na kusikiliza mapigo ya moyo ya mtotozitatolewa bure Lengo la Serikali ya Rais Samia Suluhu ni kupunguza vifo vya mama na mtoto pamoja na kifafa cha mimba vilivyokua vinatokana na kutopata huduma za awali kwa wajawazito.

Lakini pia Rais Samia Suluhu alipoingia madarakani aliahidi kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa kuboresha huduma sasa amefanikiwa kwa kujenga majengo ya huduma ya mama na mtoto hadi vijijini sasa huduma zinapatikana karibu na makazi ya wananchi vile vifo vilivyokua vinatokana na umbali wa huduma hiyo vinaendelea kupungua.

 
Tengeneza tatizo halafu litatue ili usifiwe CCM bhana?
 
Kwani vilikua vinalipiwa? Bei gani?
 
Waweke huduma za kukifungua na ujauzito iwe Bure kabisa serikali tuthamini basi wanawake pia jengeni ward kubwa za wamama sio wanalala watatu wa tatu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…