Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Serikali imepanga kuchanja watu milioni 10 kufikia mwishoni mwa mwaka huu.Takwimu za wizara ya Afya zinaonyesha kuwa jumla ya watu 5,029,901 wamepewa chanjo. Kati yao, 3,545,060 wamepata dozi moja huku 1,484,841 wakiwa wamepata dozi zote mbili.
Watu 1,012,457 wamepata dozi ya kwanza ya chanjo ya corona jijini Nairobi huku 511,615 wakiwa wamepata dozi zote mbili. Serikali inalenga kuchanja watu milioni 3 wa kuanzia umri wa miaka 18 na zaidi jijini Nairobi.
Watu 139,943 na 322,519 wamepata dozi mbili na moja mtawalia katika Kaunti ya Kiambu.Kaunti ya Nyeri imechanja asilimia 14.7 ya watu wanaolengwa, Kiambu (asilimia 8.6), Uasin Gishu (asilimia 7.7), Nyandarua (asilimia 7.4), Kisumu (asilimia 6.9) na Mombasa (asilimia 6.5).
Katika eneo la Pwani, Kaunti ya Mombasa inaongoza kwa idadi ya watu waliochanjwa dozi zote mbili. Watu 52,379 wamechanjwa dozi mbili jijini Mombasa, Kilifi (15,506) na Taita Taveta (14,679).Kaunti za kaskazini mashariki mwa nchi na sehemu za Bonde la Ufa, hata hivyo, zinajikokota katika utoaji wa Chanjo ya Corona.
Ripoti ya wizara ya Afya iliyotolewa jana inaonyesha kuwa Kaunti za Pokot Magharibi, Mandera, Wajir, Garissa na Marsabit zimechanja chini ya asilimia moja. Kenya imepokea jumla ya dozi 8,006,820 za aina mbalimbali za chanjo ya corona, ikiwemo AstraZeneca, Johnson & Johnson, Moderna, Pfizer na Sinopharm iliyotengenezwa China.
Hiyo inamaanisha kuwa Kenya imesalia na takribani dozi milioni 3.Kenya inatarajia kupokea sehemu ya dozi milioni 50 za chanjo ya Moderna ambazo Amerika ilitangaza jana kuuzia Umoja wa Afrika (AU).
Watu 1,012,457 wamepata dozi ya kwanza ya chanjo ya corona jijini Nairobi huku 511,615 wakiwa wamepata dozi zote mbili. Serikali inalenga kuchanja watu milioni 3 wa kuanzia umri wa miaka 18 na zaidi jijini Nairobi.
Watu 139,943 na 322,519 wamepata dozi mbili na moja mtawalia katika Kaunti ya Kiambu.Kaunti ya Nyeri imechanja asilimia 14.7 ya watu wanaolengwa, Kiambu (asilimia 8.6), Uasin Gishu (asilimia 7.7), Nyandarua (asilimia 7.4), Kisumu (asilimia 6.9) na Mombasa (asilimia 6.5).
Katika eneo la Pwani, Kaunti ya Mombasa inaongoza kwa idadi ya watu waliochanjwa dozi zote mbili. Watu 52,379 wamechanjwa dozi mbili jijini Mombasa, Kilifi (15,506) na Taita Taveta (14,679).Kaunti za kaskazini mashariki mwa nchi na sehemu za Bonde la Ufa, hata hivyo, zinajikokota katika utoaji wa Chanjo ya Corona.
Ripoti ya wizara ya Afya iliyotolewa jana inaonyesha kuwa Kaunti za Pokot Magharibi, Mandera, Wajir, Garissa na Marsabit zimechanja chini ya asilimia moja. Kenya imepokea jumla ya dozi 8,006,820 za aina mbalimbali za chanjo ya corona, ikiwemo AstraZeneca, Johnson & Johnson, Moderna, Pfizer na Sinopharm iliyotengenezwa China.
Hiyo inamaanisha kuwa Kenya imesalia na takribani dozi milioni 3.Kenya inatarajia kupokea sehemu ya dozi milioni 50 za chanjo ya Moderna ambazo Amerika ilitangaza jana kuuzia Umoja wa Afrika (AU).