Serikali imesahau kabisa kama kuna shule za hivi jamani..

Down To Earth

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
21,940
Reaction score
16,643
hawa watoto nao wana ndoto zao maishani!

wengine watataka kuwa mawaziri, wengine wafanyabiashara, wengine waalimu, mwingine atataka awe rais n.k

sasa je kwa mazingira kama haya, ndoto zao zitatimilika kweli?



serikali yetu bado haijawa serious kabisa katika kutoa elimu sawa kwa wote.

kwa uchunguzi wa haraka, kuna watoto wengine hata wanafikia hatua ya kumaliza shule ya msingi, licha ya kutojua kusoma na kuandika, lugha yenyewe ya kiswahili hawazwezi kuizungumza vizuri.

Tanzania inarudishwa nyuma na vwananchi wake wenyewe!

endapo tukiamua kuwaamsha viongozi, hakika maendeleo yataonekana!
 
mkuu unazungumzia serikali ipi, Zanzibar au Tanganyika???? kama ni ya Tanganyika wataanza kujali siku, "cdm" itakapopotea kwenye medani za siasa. kwa sasa nguvu na pesa zimeelekezwa dhidi ya huko. via Stephano Wassira.
 
Hakuna serikali iliyofanikiwa 100% kusomesha watoto wake wote bure, tafakari chukua hatua, siasa zitatuua!
 
mbona nmesikia samwel luhanga anaanxa kutoa tablet kwenye primary schools.... cc MSALANI
 
Last edited by a moderator:
Tumesoma kwa kukaa kwenye matofari ,hakuna jipya hapo.
 
Mkuu suala la kujali malezi ya mtoto,kiafya kielimu, lianzie nyumbani kwa maana mbali na mtoto kuwa wa jamhuri ana wazazi pia. Muhimu ni serikali kuinua level ya maisha ya watu wa hali ya chini ili kupunguza umasikini,hilo liishakufanikiwa nadhani hakuna mzazi mwenye mawazo endelevu ambaye angependa kuona mwanae akisoma katika mazingira kama haya sema uwezo wa kumudu mazingira tofauti unashindikana kutokana na maisha kubana!
 
Huna hata chembe ya huruma umewapaka vumbi hao watoto ili utimize lengo lako la kupata picha za kijinga ili uje utulingishie hapa, acha kutumika, watanzania wa siku hizi wanaakili walishawajua nia na hila zenu chafu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…