Ni lazima tupongeze kwa dhati uamuzi wa serikali wa kujenga viwanda. ni maamuzi sahihi na tusipofanya maamuzi kama hayo tujue hakuna miujiza katika kupata maisha bora, maisha bora yanapatikana kwa kufanya maamuzi sahihi na kuyatekeleza kwa wakati.
Swali kuu hapa ni je serikali inatekeleza maamuzi haya kwa usahihi?
binafsi nina wasiwasi mkubwa kutokana na mambo yafuatayo.
kwanza ninajaribu kuangalia taasisi ambazo serikali inazitumia kujenga Viwanda, nikachukua Jeshi la magereza pamoja na mifuko ya hifadhi ya jamii. Ki msingi ukiangalia Jeshi la magereza wanayo miradi mingi kama ufugaji na utengenezaji wa thamani, kiwanda cha viatu na ujenzi wa majengo.
hivi ni mradi gani katika miradi yote iliyoko chini ya jeshi hili inaendeshwa kwa tija kibiashara? mathalani miradi ya ngombe unakuta mbali na kuwa na cheap labour lakini miaka nenda miaka rudi mifugo hii haiongezeki na hawafanyi biashara kusema wanauza kupata faida.
Sitaki kuzungumzia miradi ya kilimo, au ujenzi ambapo mbali na kuwa na wafanyakazi wa bure nyumba zao za kuishi tu wameshindwa kuzikarabati na kuziweka katika hali nzuri angalau kwa kufanya biashara kupata fedha za kununua vifaa na kutumia ufundi wa bure walionao kuweka nyumba za askari katika hali nzuri.
ninachotaka kusema ni kitu gani? hebu jiulize unaweza kumchukua mtu aliyezoea kutembea miguu peku ukamnunulia viatu siku moja na kumlazimisha kuvaa viatu? bila shaka atakuwa akikuona anavaa viatu na ukitoka anavua anatembea peku.
hivi unaweza kumchukua mtoto aliyezoea kwenda kwenye mziki mpaka usiku wa manane, hakuna shoo inayompita umfungie geti eti akae ndani? kimsingi mtoto huyu ataanza kujifunza mbinu mpya za kuruka fensi usiku na kutoroka kwenda kwenye mziki.
hebu watazame mifuko ya hifadhi ya jamii, hivi hawa wanafanya miradi gani yenye tija? kimsingi ni wataalamu wa kujenga majengo lakini ni nani amewahi kufanya tathmini ya gharama halisi inayotumika katika majengo haya kulinganisha na thamani halisi ya majengo yenyewe? tumeona ni mradi gani wa kibiashara wameufanya mifuko hii na wakauendesha kwa faida? sijui kama upo.
tunaweza kujiuliza hivi ni kwa nini huko nyuma tuliingia katika serikali kufanya biashara na tukashibdwa na wenzetu wenye kujua wakatushauri serikali ijitoe kwenye kufanya biashara na iwatengenezee mazingira sekita binafsi? sina uhakika kama tunajiona kuwa na ujuzi kuwashinda waliotushauri au tulielewa sababu zilizofanya watushauri hivyo.
nashindwa kuelewa kama tumeona tumepiga virungu viwili na tukajiamini kuwa tunaouwezo wa kuthibiti "corruption kiasi cha serikali kurudi kwenye biashra? ki msingi ni jambo gumu sana kwa serikali kujenga viwanda na kuviendesha.
1. ni kutokana na taasisi inazozitumia kuwa zimekwisha remaa. Yaani wamezoea kufanya miradi kwa hasara. kitaalamu wanasema ni bora mtu asiyejua anarekebishika lakini mtu anayejua jibu lisililo sahihi ni vigumu kufuta anachokijua na kumfahamisha kingine. Yaani hawa wamezoea mambo ya hovyo hivyo hata uawabane vipi watakachokifanya ni kujifunza mbinu za kiprofesional katika kufanya mambo ya hovyo. yaani kama unavyoona ukimfungia mtoto aliyezoea kwenda disco anaanza kujifunza kuruka ukuta na akaenda na kabla ya kucha akarudi akaruka ukuta hivyo kupiga virungu viwili tusijione tunaweza kudhibiti corruption hivyo tuzidi kuirundukia serikali biashara itaziendesha vizuri.
moja ya sababu ya serikali kujitoa katika biashara ni kudhibiti corruption hivyo mapambano yetu ya corruption yatakuwa na tija iwapo tutazidi kuielekeza serikali katika kujenga mazingira na kusimamia biashara tu.
2. Moja ya sababu kubwa zinazofanya taasisi za serikali kushindwa kufanya biashara ni watendaji wake kutokuwa na msukumo unaoleta ushindani kwenye biashara. mfano jambo linalosukuma makampuni kufanya vizuri katika biashara ni msukumo wa kutafuta faida unaotoka kwa wawekeza mitaji na kushuka chini hadi kwa wafanyakazi wenyewe. wawekezaji binafsi hawako tayari kupoteza mitaji hivyo kwa huweka usimamizi kuhakikisha mitaji yao inatumika vizuri lakini pia kutafuta motisha za kuwafanya wafanyakzi watimize wajibu wao. motisha hizi zinaweza kuwa adhabu kwa anayefanya vibaya na zawadi kwa anayefanya vizuri.
lakini kwa serikali kwanza wenye mitaji ambao ni wananchi wala hawana habari kama hiyo ni mitaji yao na pili wale wanaokabidhiwa dhamana huwa hawana machungu. matokeo yake hakuna taasisi ya umma inayojisikia vibaya kupoteza mtaji na badala yake hujali mlolongo wa maamuzi na mambo mengine yasiyo na tija ambayo mara nyingi ni chanzo cha upotevu wa mitaji.
kwa kifupi kama tunataka kujenga viwanda kama kujenga viwanda tunaweza kuzitumia taasisi za serikali kujenga viwanda lakini kama tunataka kujenga viwanda kwa kulenga faida. viwanda hivi viendeshwe kibiashara kwa maana vitusaidie kuagiza mashine na si bidhaa, vizalishe ajira kwa watanzania, vizuie fedha zetu kwenda nje kufuata bidhaa, tuzalishe bidhaa zivuke mipaka ziende nje kutuletea fedha za kigeni hatuwezi kuthubu kutumbukia katika kujenga viwanda kwa kutumia taasisi za umma na zenye uzoefu hasi katika kufanya biashra, bora kama wangekuwa na uzoefu sifuri.
nini serikali ingefanya.
serikali mitaji hii iitoe kwa watanzania katika sekita binafsi wazalishe wenyewe. huko nyuma tulikwama katika hili kutokana na corruption, tulivyoandaa mipango kama hii watendaji wa umma waliitumia kuhujumu, waliwapa watu wasio na sifa kwa kigezo cha undungu au rushwa.
tunapokuwa tumeinua rungu kudhibiti haya katika umma basi ni wakati wa mitaji hii tuiundie bank ya kuwakopesha wazalishaji kwa masharati nafuu.
tatizo kubwa la watanzania ni uwezo wa kupata mitaji lakini ujuzi wanao kwani hata hao wageni wanaofanikiwa wanawatumia watanzania hawa hawa. tutengeneze programu zinazowaleta watanzania wataalamu wenye fikra sawa wakopeshwe miundombinu na fedha ya kuanzia na serikai inaweza kumonitor account zao mpaka wanaporudisha mikopo ndio wanakuwa huru.
Swali kuu hapa ni je serikali inatekeleza maamuzi haya kwa usahihi?
binafsi nina wasiwasi mkubwa kutokana na mambo yafuatayo.
kwanza ninajaribu kuangalia taasisi ambazo serikali inazitumia kujenga Viwanda, nikachukua Jeshi la magereza pamoja na mifuko ya hifadhi ya jamii. Ki msingi ukiangalia Jeshi la magereza wanayo miradi mingi kama ufugaji na utengenezaji wa thamani, kiwanda cha viatu na ujenzi wa majengo.
hivi ni mradi gani katika miradi yote iliyoko chini ya jeshi hili inaendeshwa kwa tija kibiashara? mathalani miradi ya ngombe unakuta mbali na kuwa na cheap labour lakini miaka nenda miaka rudi mifugo hii haiongezeki na hawafanyi biashara kusema wanauza kupata faida.
Sitaki kuzungumzia miradi ya kilimo, au ujenzi ambapo mbali na kuwa na wafanyakazi wa bure nyumba zao za kuishi tu wameshindwa kuzikarabati na kuziweka katika hali nzuri angalau kwa kufanya biashara kupata fedha za kununua vifaa na kutumia ufundi wa bure walionao kuweka nyumba za askari katika hali nzuri.
ninachotaka kusema ni kitu gani? hebu jiulize unaweza kumchukua mtu aliyezoea kutembea miguu peku ukamnunulia viatu siku moja na kumlazimisha kuvaa viatu? bila shaka atakuwa akikuona anavaa viatu na ukitoka anavua anatembea peku.
hivi unaweza kumchukua mtoto aliyezoea kwenda kwenye mziki mpaka usiku wa manane, hakuna shoo inayompita umfungie geti eti akae ndani? kimsingi mtoto huyu ataanza kujifunza mbinu mpya za kuruka fensi usiku na kutoroka kwenda kwenye mziki.
hebu watazame mifuko ya hifadhi ya jamii, hivi hawa wanafanya miradi gani yenye tija? kimsingi ni wataalamu wa kujenga majengo lakini ni nani amewahi kufanya tathmini ya gharama halisi inayotumika katika majengo haya kulinganisha na thamani halisi ya majengo yenyewe? tumeona ni mradi gani wa kibiashara wameufanya mifuko hii na wakauendesha kwa faida? sijui kama upo.
tunaweza kujiuliza hivi ni kwa nini huko nyuma tuliingia katika serikali kufanya biashara na tukashibdwa na wenzetu wenye kujua wakatushauri serikali ijitoe kwenye kufanya biashara na iwatengenezee mazingira sekita binafsi? sina uhakika kama tunajiona kuwa na ujuzi kuwashinda waliotushauri au tulielewa sababu zilizofanya watushauri hivyo.
nashindwa kuelewa kama tumeona tumepiga virungu viwili na tukajiamini kuwa tunaouwezo wa kuthibiti "corruption kiasi cha serikali kurudi kwenye biashra? ki msingi ni jambo gumu sana kwa serikali kujenga viwanda na kuviendesha.
1. ni kutokana na taasisi inazozitumia kuwa zimekwisha remaa. Yaani wamezoea kufanya miradi kwa hasara. kitaalamu wanasema ni bora mtu asiyejua anarekebishika lakini mtu anayejua jibu lisililo sahihi ni vigumu kufuta anachokijua na kumfahamisha kingine. Yaani hawa wamezoea mambo ya hovyo hivyo hata uawabane vipi watakachokifanya ni kujifunza mbinu za kiprofesional katika kufanya mambo ya hovyo. yaani kama unavyoona ukimfungia mtoto aliyezoea kwenda disco anaanza kujifunza kuruka ukuta na akaenda na kabla ya kucha akarudi akaruka ukuta hivyo kupiga virungu viwili tusijione tunaweza kudhibiti corruption hivyo tuzidi kuirundukia serikali biashara itaziendesha vizuri.
moja ya sababu ya serikali kujitoa katika biashara ni kudhibiti corruption hivyo mapambano yetu ya corruption yatakuwa na tija iwapo tutazidi kuielekeza serikali katika kujenga mazingira na kusimamia biashara tu.
2. Moja ya sababu kubwa zinazofanya taasisi za serikali kushindwa kufanya biashara ni watendaji wake kutokuwa na msukumo unaoleta ushindani kwenye biashara. mfano jambo linalosukuma makampuni kufanya vizuri katika biashara ni msukumo wa kutafuta faida unaotoka kwa wawekeza mitaji na kushuka chini hadi kwa wafanyakazi wenyewe. wawekezaji binafsi hawako tayari kupoteza mitaji hivyo kwa huweka usimamizi kuhakikisha mitaji yao inatumika vizuri lakini pia kutafuta motisha za kuwafanya wafanyakzi watimize wajibu wao. motisha hizi zinaweza kuwa adhabu kwa anayefanya vibaya na zawadi kwa anayefanya vizuri.
lakini kwa serikali kwanza wenye mitaji ambao ni wananchi wala hawana habari kama hiyo ni mitaji yao na pili wale wanaokabidhiwa dhamana huwa hawana machungu. matokeo yake hakuna taasisi ya umma inayojisikia vibaya kupoteza mtaji na badala yake hujali mlolongo wa maamuzi na mambo mengine yasiyo na tija ambayo mara nyingi ni chanzo cha upotevu wa mitaji.
kwa kifupi kama tunataka kujenga viwanda kama kujenga viwanda tunaweza kuzitumia taasisi za serikali kujenga viwanda lakini kama tunataka kujenga viwanda kwa kulenga faida. viwanda hivi viendeshwe kibiashara kwa maana vitusaidie kuagiza mashine na si bidhaa, vizalishe ajira kwa watanzania, vizuie fedha zetu kwenda nje kufuata bidhaa, tuzalishe bidhaa zivuke mipaka ziende nje kutuletea fedha za kigeni hatuwezi kuthubu kutumbukia katika kujenga viwanda kwa kutumia taasisi za umma na zenye uzoefu hasi katika kufanya biashra, bora kama wangekuwa na uzoefu sifuri.
nini serikali ingefanya.
serikali mitaji hii iitoe kwa watanzania katika sekita binafsi wazalishe wenyewe. huko nyuma tulikwama katika hili kutokana na corruption, tulivyoandaa mipango kama hii watendaji wa umma waliitumia kuhujumu, waliwapa watu wasio na sifa kwa kigezo cha undungu au rushwa.
tunapokuwa tumeinua rungu kudhibiti haya katika umma basi ni wakati wa mitaji hii tuiundie bank ya kuwakopesha wazalishaji kwa masharati nafuu.
tatizo kubwa la watanzania ni uwezo wa kupata mitaji lakini ujuzi wanao kwani hata hao wageni wanaofanikiwa wanawatumia watanzania hawa hawa. tutengeneze programu zinazowaleta watanzania wataalamu wenye fikra sawa wakopeshwe miundombinu na fedha ya kuanzia na serikai inaweza kumonitor account zao mpaka wanaporudisha mikopo ndio wanakuwa huru.