mjasiriamali mdogo
JF-Expert Member
- Mar 15, 2013
- 258
- 110
Watu tumeamua kujiajiri katika kilimo lakini cha kuskitisha hakuna soko la uwakika. Huku songea kipindi cha mavuno serikali ilinunua mahindi kilo kwa tsh 500 kwa muda mfupi ikatangaza kuishiwa fedha na magunia. Mbaya zaidi wakulima mpaka sasa tuna mahindi mengi sana na wanunuzi hakuna na wanaojitokeza kutoka nje ya nchi wanapata vikwazo kibao. Serikali tusaidie kututafutia soko la uwakika la mazao ili tuondolane na umaskin. Nawakaribisha wote mnaotaka kulima huku ardhi ipo kubwa na hakuna shida katika upatikanaji kwa kununua au kukodi. Karibu songea karibu ruvuma.