Serikali inapanga kuchakachua matokeo kidato cha pili

the muter

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2012
Posts
1,347
Reaction score
1,828
Katika kile kinachoonekana hali tete serikali imeshindwa kutoa matokeo ya kidato cha pili kwani wanafunzi wamefeli sana.kama wastani utabaki ule ule wa 30 kuna shule zitafaulisha wanafunzi chini ya kumi.Serikali inataka kupunguza wastani kama walivyofanya darasa la saba waliposhusha wastani mpaka 70.ikumbukwe pia kama serikali yetu ni ya quantity na sio quality ndio maana hata Rais kwenye hotuba yake alijisifia kupeleka wanafunzi wengi sekondari mwaka huu bila kujali ubora wa wanafunzi walioenda sekondari
 

Mlipokua mnauza maandazi darasan badala ya kufundisha hamkujua hayo ya watoto kufeli zaidi?
 
Uhusiano wa mada na hoja yako haupo nani kakwambia mleta mada ni mwalimu? Na je ni shule zote wanauza maanazi kwa mujibu wako? Kazi ipo
 
Mimi wasiwasi mkubwa ni kuwa hii mitaihani ipo chini ya mkaguzi mkuu wa Elimu Kanda, na hawa huwa wanashindana ni yupi kafaulisha sana ni yupi kafelisha sana hivyo itakuwa ni rahisi sana kwao kuanza kuchakachua matokeo kwani kila mmoja hatotaka kuwa nyuma ya mwenzake.
Hivyo nitoe ushauri wangu wa dhati wa Waziri mwenye dhamana na elimu ndani ya Nchi, kuwa kama kweli ana nia njema na Taifa hili hii mitihani airudishe kwenye chombo amabacho mimi kama mimi nina imani nacho sana kiitwacho Baraza la Mitihani la Taifa a.k.a NECTA, hapo ndipo suluhu ya elimu itafahamika ndani ya Taifa letuuuu!!!
 
Wadau mambo yako hadharani, je yaliyotangazwa ni ya kweli au kuna uchakachuaji?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…