Hili suala lisipodhibitiwa basi madhara yake yatakuwa makubwa mno.
Fikiria hiki kizazi kinachokuwa kizazi cha wanafunzi kuanzia primary hadi secondary kinachojiingiza kwenye haya makamari.
Baada ya miaka kumi mbele tutakuwa na kizazi cha aina gani??
Kizazi kisichofikiri kwenye kufanya kazi,nguvu kazi inapotea bure kwa vijana kushinda kwenye mabanda ya kamari bila kuzalisha kitu chochote.
Na tazama baada ya kuona soko la uhakika angalia makampuni ya kamari yalivyoshika hatamu kipindi hiki na yataongezeka zaidi na zaidi.
Unaona hadi viongozi wa serikali wanashiriki kupromote biashara hii kwa kuwakabidhi washindi hundi zao na zawadi mbalimbali.
Wenzetu kamari ni hobby huku kwetu tunataka kugeuza kazi.
Serikali chukueni hili suala kwa umakini mkubwa,kizazi kinakwenda kuangamia,tusisubiri hadi tuangamie ndio tupige marufuku.
Hapa tuamue kati ya kodi(revenue gainsVS society welfare)
Uamuzi ni wetu...!!tuchukue hatua