Serikali inatengeneza Ajira 40,000 Kwenye Kilimo

Serikali inatengeneza Ajira 40,000 Kwenye Kilimo

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Rais Samia Suluhu amemaliza Ziara yake leo mkoani Manyara kwa kukagua Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Manyara. Baada ya ukaguzi huo alikutana na kuzungumza na wananchi. Kabla ya Rais Samia kuzungumza. Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alipata nafasi ya kuzungumza na kuongelea jinsi Serikali ilivyojipanga kuzalisha ajira kupitia kilimo na kupunguza tatizo la ajira nchini.

Serikali imeanzisha mashamba ya pamoja zaidi ya hekari 188,000 ambazo zitagaiwa na kumilikishwa kwa vijana. Aidha mradi huo utagharimu Shs. Bilioni 200 na kutengeneza ajira 40,000 ndani ya miaka 3. Pamoja na hayo Serikali imeongeza bajeti ya kilimo ili kujenga mabwawa ya umwagiliaji yatakayosaidia kuachana na kilimo cha kutegemea mvua.

"Hukutaka kuwalaumu vijana kwa kutokufanya kazi uliamua kuweka fedha ili vijana wa kitanzania kuingia mashambani"-Mhe. Waziri Hussein Bashe
 
Kilimo kipi hicho? Hiki hiki cha jembe la mkono na mvua zisizo tabirika?

Na hata hayo mabwawa mnayojifanya mnaenda kujenga, mwisho wake utakuwa ni upigaji tu! Na hakuna cha maana kitakachofanyika.
 
Kilimo kipi hicho? Hiki hiki cha jembe la mkono na mvua zisizo tabirika?

Na hata hayo mabwawa mnayojifanya mnaenda kujenga, mwisho wake utakuwa ni upigaji tu! Na hakuna cha maana kitakachofanyika.
Nenda site kaone miradi inayoendelea huwezi kujifungua ndani alafu ukalalamika ni upigaji
 
Nenda site kaone miradi inayoendelea huwezi kujifungua ndani alafu ukalalamika ni upigaji
Mabwawa kibao yamejengwa chini ya kiwango! Mfano kule Igurusi Mbeya. Mingine wajanja walipiga hela juu kwa juu!

Kuna jipya lipi kwenye serikali inayo ongozwa na wapigaji wa ccm?
 
Back
Top Bottom