SoC01 Serikali inavyoweza kuzuia wimbi la vijana kuhama vijijini, kuhamia mijini na kuondoa umaskini katika jamii kwa kufanya haya...

SoC01 Serikali inavyoweza kuzuia wimbi la vijana kuhama vijijini, kuhamia mijini na kuondoa umaskini katika jamii kwa kufanya haya...

Stories of Change - 2021 Competition

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari,

Kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili vijana huamua kuhamia mijini kujaribu kutatua changamoto hizo.
Lakini pamoja na wimbi hili la vijana ambao ni nguvu kazi kuhamia mijini lakini bado jamii zinaendelea kukumbwa na changamoto zaidi.

Umaskini, ujinga(kukosa elimu), na maradhi bado ni mtego kwa mamilioni ya Watanzania.

SERIKALI NA JAMII KWA UJUMLA IFANYE MAMBO TAFUATAYO KUPUNGUZA WIMBI LA VIJANA KUHAMA VIJIJINI NA KUHAMIA MIJINI ILI KUKUZA UCHUMI WA NCHI NA VIJANA KWA UJUMLA.

1. Kuanzisha miradi ya kikanda.
Hapa serikali inapaswa kuanzisha miradi mikubwa kikanda kulingana na uoto wa sehemu husika au kulingana na shughuli kuu za sehemu husika.

Mfano

1: Serikali itatakiwa kuanzisha mashamba makubwa ya mikorosho mikoa ya Lindi na Mtwara, vijana wataingizwa kwenye miradi kama sehemu ya wamiliki washiriki (wanahisa) kwakuwa ndio watakuwa nguvu kazi. Serikali itawajibika kutafuta wataalamu, kuwekeza vifaa vya kisasa vya kazi na kufadhili mradi kwa ujumla.

Mfano
2: Serikali itatakiwa kuanzisha vitalu vya uvuvi ziwa Victoria, ziwa Tanganyika na ziwa Nyasa. Hapa serikali itawajibika kutafuta wataalamu na kufadhili mradi.

Sehemu ya mavuno itakapouzwa serikali itapata fedha na vijana watapata fedha pia. Hivyo fursa zitakuwa zimewafuata vijana waliko huko vijijini hali itakayopelekea kupungua kasi ya vijana kuhama vijijini kuhamia mijini (Rural to urban migration).

2. Kujenga vyuo vya ufundi kila kata na kufadhili masomo ya muda mfupi kwa vijana wa maeneo husika.
Kama serikali ilivyoweza kujenga sekondari kila kata vivyo hivyo serikali inapaswa kujenga vyuo vya ufundi kila kata ili kuwapa ujuzi na stadi za maisha vijana waliomaliza darasa la saba na kidato cha nne lakini wamekosa fursa zingine za kielimu na kibiashara.

3. Kutoa mikopo rahisi ya vitendea kazi kwa vijana wenye taaluma ya ufundi.
Wapo vijana wenye ufundi ama ujuzi walioupata VETA na vyuo vingine vya ufunfi, na wengine wamepata ujuzi mitaani. Hawa wakipatiwa mikopo rahisi ya vitendea kazi kama granding machine, air compressor n.k wanaweza kuanzisha viwanda vidogovidogo mahali waliko na wasione tena haja ya kwenda mijini huku wasijue wanakwenda kufanya nini hukojini. Hivyo jamii itaneemeka na umaskini utaondoka kabisa. Hapatakuwa na haja tena kwa vijana kwenda mijini kutafuta ajira au kufanya ujasiriamali ambao hauna tija kubwa kwa taifa(ujasiriamali wa kuuza bidhaa kutoka nje ya nchi).

Asanteni.
 
Upvote 1
Kwa mfano Mwanza kunapatikana zaidi samaki,chuo cha uvuvi kingejengwa huko,Tanga matunda zaidi yanapatikana huko, kiwanda cha kusindika matunda kingesaidia ku create ajira Tanga na kuzuia vijana kuhama, sehemu kama Tabora asali inapatikana zaidi huko kungekuwa na kiwanda cha ku rina asali...vyuo na viwanda vingejengwa kimkakati ku explore kitu gani kinapatikana mkoa husika kungezuia vijana kuhama..nimeipenda topic yako, you have my vote mkuu... 👍 👍 👍 👍
 
Kwa mfano Mwanza kunapatikana zaidi samaki,chuo cha uvuvi kingejengwa huko,Tanga matunda zaidi yanapatikana huko, kiwanda cha kusindika matunda kingesaidia ku create ajira Tanga na kuzuia vijana kuhama, sehemu kama Tabora asali inapatikana zaidi huko kungekuwa na kiwanda cha ku rina asali...vyuo na viwanda vingejengwa kimkakati ku explore kitu gani kinapatikana mkoa husika kungezuia vijana kuhama..nimeipenda topic yako, you have my vote mkuu... 👍 👍 👍 👍
Asante
 
Ndani ya miaka 3 jinsi ya kuleta maendeleo na kumaliza tatizo la ajira nchini.

1.Ondoa futa kodi zote za kuingiza magari ya mizigo na abiria nchini kodi yake utaipata mara mbili yake kupitia indirect tax.Kwenye mafuta,leseni za udereva,fine za traffic, parking fee,ushuru wa stand,spare za magari,leseni na vibali mbalimbali.Gari moja uajiri si chini ya vijana 3.

2.Toa ruzuku kwenye viwanda vya kuzalisha matrekta wazalishe matreka mengi waje watuuzie wakulima kwa robo bei trekta moja uajiri zaidi ya watu wanne.

3.Jenga schemes za umwagaliaji KILA kijiji upitapo mto pande zote mbili watu walime mwaka mzima ni aibu sana kwa maji ya mito kumwaga maji yake baharini badala ya mashambani.Soko la mazao nje ya nchi lipo tele

4.Jenga vyuo vya ujuzi kila kata kopesha vijana ujuzi baada ya kumaliza darasa la saba wakapate ujuzi wautakao.

Kukopesha vijana waende chuo kikuu kisha warudi mtaani kuendesha bodaboda na kuwa machinga ni upotevu Mkubwa Sana wa kodi zetu na kuongeza idadi ya masikini nchini.

5.Fungua mipaka watu wauze watakapo nje ya nchi kuna masoko tele.Legeza masharti ya vibali Ili export ikue.

Ni sekta mbili tu zingine takataka hazifikii kilimo na madini kwa kuajiri vijana wote nchini na kuongeza pato la taifa bila kutegemea kukopa na kukamua kodi wananchi.

6.Peleka KILA kijiji mashine za kutengeneza interlocking block na vigae Ili watz wote wajenge nyumba bora kwa gharama nafuu kabisa

Mjerumani kwa miaka 15 alituletea maendeleo makubwa Sana ccm imeshindwa nini.
 
Sekta ya kilimo na madini pekee ndo huweza ajiri vijana wote nchini
 
Back
Top Bottom