Serikali iongeze mwekezaji kwenye barabara ya mwendokasi ili kukuza ushindani

Serikali iongeze mwekezaji kwenye barabara ya mwendokasi ili kukuza ushindani

gstar

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2011
Posts
790
Reaction score
1,373
Kutokana na uendeshaji wa shirika la DART kusuasua, na kwamba zaidi ya magari 70 kufikia kuwekwa pembeni kutokana na ubovu na madereva kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kutokutoa huduma zinazo ridhisha, ni wakati sasa kwa serikali kuongeza mwekezaji mwengine kwenye njia hiyo ili kukuza ushindani.

Pamoja na hayo, barabara ya Mbagala tangu izinduliwe haikuwahi tena kufanya kazi ya kupitisha mabasi ya mwendokasi jambo ambalo lingepunguza adha ya usafiri kwa abiria, ili kuifanya DART kufanya kazi kwa ufanisi, ninapendekeza ziongezwe kampuni mbili zaidi kila mmoja iwe na mabasi yake na zote zipewe haki ya kutumia barabara ya mwendo kasi.

Serikali iwekeze kwenye usimamizi na kukusanya mapato yake.
 
Maboresho yanayotakiwa kufanyika katika mradi wa mabasi yaendayo haraka Bus rapid transit (BRT) jijini Dar es Salaam.
Nimebaini changamoto kadhaa zinazotakiwa kutatuliwa katika mradi huu.

Hivyo nimemshauri juu ya maboresho yanayotakiwa kufanywa katika mradi huu. Pitia katika link hii kusoma ushauri wote: Kwako Mkurugenzi mpya wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART): Katatue changamoto zifuatazo….

Pia michango mbalimbali imetolewa na wadau wengine na wameshauri jinsi ambavyo mfumo wa uendeshaji wa haya mabasi unapaswa kuwa ili kwendana na ukuaji wa teknolojia:

Ushauri wote tumeuandika hapa: Kwako Mkurugenzi mpya wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART): Katatue changamoto zifuatazo….
 
Back
Top Bottom