Sodoku
JF-Expert Member
- Feb 3, 2016
- 1,271
- 2,903
Kwanza niseme wazi wazi kabisa huwa sikubaliana na njia za matumizi ya nguvu kwenye maamuzi yoyote yale. Lakini pia wanasema binadamu ukimnyima haki yake mwishowe huamua kuchukua kwa nguvu. Na tuliona huko South Afrika kipindi cha ubaguzi, Msumbiji, Angola n.k lakini sipendelei sana maamuzi ya namna hiyo.
Serikali ishukuru kuwa wanachama wa Simba waliamua kuvunja tu viti, wasiwasi wangu ilikuwa kama wangeamua kuingia ndani ya kiwanjani kuwashughulikia waamuzi nadhani hali ingekuwa mbaya zaidi. Hapo kusingekuwa na malipo ya kutosha ya uhai au viungo vya waamuzi hao.
Hivi ni wangapi wakikasirika hupiga meza? Namfahamu mheshimiwa mmoja ni mtu mkubwa sana, sana kwenye serikali. Alikasirika siku hiyo ofisini kwake akapiga meza ngumi na kusukuma kompyuta iliyokuwa mezani ikaanguka. Waliokuwa pamoja naye waliogopa sana lakini walimsifia kuwa anachukia sana uonevu baada ya kusikia kuwa kuna maskini wameonewa sehemu flani. Niliambiwa aliletewa kompyuta nyingine kesho yake bora kuliko ile ya kwanza.
Nilipomwambia jambo hili mwalimu wangu ambaye ni Dr pia wa saikolojia akanambia ni afadhali alipiga ngumi meza maana angekuwa hajajua namna ya kuhamishia hasira yake basi angepiga mtu na pengine angeua mtu.
Ni wangapi wanaudhiwa ofisini na boss wanakuja kushusha hasira zao kwa paka au mbwa analewalilia miguuni wakiwa nyumbani? Serikali ijitahidi kuwaambia TFF waelewe umuhimu wa michezo na maana yake kwa wanagenzi. Maana kama tusipokuwa makini tukumbuke habari za Escobar aliyekuwa mchezaji wa Colombia baada ya kufungisha goli aliuawa na mtu mwenye hasira kali. Kumbe mtu huyu angepata nafasi akang'oa kiti kimoja au viwili hasira zake zingeisha.
Lakini nasisitiza mashabiki wa team zote tusifanye fujo za namna hii. Wakati mwingine ni bora kushughulika na anayesababisha tatizo kama hilo na si vitu.
List ya matukio ya vurugu uwanjani hapa duniani. List of violent spectator incidents in sports - Wikipedia, the free encyclopedia
Serikali ishukuru kuwa wanachama wa Simba waliamua kuvunja tu viti, wasiwasi wangu ilikuwa kama wangeamua kuingia ndani ya kiwanjani kuwashughulikia waamuzi nadhani hali ingekuwa mbaya zaidi. Hapo kusingekuwa na malipo ya kutosha ya uhai au viungo vya waamuzi hao.
Hivi ni wangapi wakikasirika hupiga meza? Namfahamu mheshimiwa mmoja ni mtu mkubwa sana, sana kwenye serikali. Alikasirika siku hiyo ofisini kwake akapiga meza ngumi na kusukuma kompyuta iliyokuwa mezani ikaanguka. Waliokuwa pamoja naye waliogopa sana lakini walimsifia kuwa anachukia sana uonevu baada ya kusikia kuwa kuna maskini wameonewa sehemu flani. Niliambiwa aliletewa kompyuta nyingine kesho yake bora kuliko ile ya kwanza.
Nilipomwambia jambo hili mwalimu wangu ambaye ni Dr pia wa saikolojia akanambia ni afadhali alipiga ngumi meza maana angekuwa hajajua namna ya kuhamishia hasira yake basi angepiga mtu na pengine angeua mtu.
Ni wangapi wanaudhiwa ofisini na boss wanakuja kushusha hasira zao kwa paka au mbwa analewalilia miguuni wakiwa nyumbani? Serikali ijitahidi kuwaambia TFF waelewe umuhimu wa michezo na maana yake kwa wanagenzi. Maana kama tusipokuwa makini tukumbuke habari za Escobar aliyekuwa mchezaji wa Colombia baada ya kufungisha goli aliuawa na mtu mwenye hasira kali. Kumbe mtu huyu angepata nafasi akang'oa kiti kimoja au viwili hasira zake zingeisha.
Lakini nasisitiza mashabiki wa team zote tusifanye fujo za namna hii. Wakati mwingine ni bora kushughulika na anayesababisha tatizo kama hilo na si vitu.
List ya matukio ya vurugu uwanjani hapa duniani. List of violent spectator incidents in sports - Wikipedia, the free encyclopedia