Serikali isiyohusika na ajira inapozuia watu kujiajiri

Serikali isiyohusika na ajira inapozuia watu kujiajiri

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Pana magari almaarufu usiku kwa usiku. Haya ni haramu kwa mujibu wa sheria japo abiria wanaoyahitaji wapo, tena wengi tu.

Pana magari Hiace yanazuiliwa kusafiri umbali zaidi ya km 100. Haieleweki ni kwa mujibu wa kigezo kipi, japo abiria wenye kuyahitaji wapo na aliyeyatengeneza hana ufahamu wa mantiki ya restriction hiyo.

Pana magari Hiace, boda boda na bajaaj kuzuiliwa kuingia mijini kati kwa mujibu wa sheria, japo wenye uhitaji wake wapo.

Kuna magari mapya kwenda nchi jirani (IT) yanazuiliwa kubeba abiria kwa mujibu wa sheria, japo abiria wenye kuyahitaji wapo.

Ni mwendo wa sheria na vizingiti right, left and center kutoka serikalini.

Cha kujiuliza: ni je, kwa nini uwepo wa uhitaji wa huduma kama hizi usionekane kuwa kama fursa? Badala ya kukimbizana na watu hawa kama ilivyokuwa mapema kwa machinga, kusiwepo utaratibu mzuri wa kulipa kodi mahsusi tu?

Kuruhusu fursa kama hizi zisingekuwa na faida kama hizi?

1. Kutoa ajira.
2. Kuongeza mapato kwa serikali.
3. Kuongeza wigo wa Kodi.
4. Kuongeza wigo wa walipa Kodi.
5. Kuondoa chuki inayojipalia serikali pasipo na umuhimu.
6. Nauli za usafiri kupungua.
7. Watu kusafiri kulingana na mahitaji yao.
8. Nk, nk.

Ni mantiki ipi inayo halalisha serikali yenye kuthubutu kutamka kuwa haihusiki kuzalisha ajira kuzizuia fursa za ajira kama hizo na kwa mujibu wa sheria zake tu?

--------

Serikali isiyo na wajibu wa kutengeneza ajira ni ya nini?
 
serikali isiyo na wajibu wa kutengeneza ajira, haifai

Staajabu ya Mussa:

IMG_20230115_092933_511.jpg
 
Wapinzani wachukue hii waende nayo kwenye mikutano ya siasa iliyoruhusiwa, wakati wa kuiamsha serikali umefika..
 
Wapinzani wachukue hii waende nayo kwenye mikutano ya siasa iliyoruhusiwa, wakati wa kuiamsha serikali umefika..

Chawa wametumwa kuja na majibu wasiyokuwa nayo:

Mikutano ya siasa wamebana, wameachia

Serikali madarakani hawana ridhaa yetu. Wana sheria zao ambazo ni mwiba kwa wananchi.

Wapinzani wayaelewe maeneo wananchi wa walks mbalimbali wanayokwazwa na serikali. Wawaunganishe kudai haki zao sasa.

Watu na makasiriko yao ni Kila Mahali.
 
Mtu alie ajiliwa akamwambia asie na ajira ajiajiri kabla hajajiajiri unakutana na vikwazo toka kwake tena
 
Mtu alie ajiliwa akamwambia asie na ajira ajiajiri kabla hajajiajiri unakutana na vikwazo toka kwake tena

Kwa hakika serikali hii haieleweki inataka nini zaidi ya kuwadidimiza watu kwenye lindi la umaskini.

Wanasema umaskini wetu ni mtaji mkubwa wao mkuu wa kubakia madarakani. Hawana huruma wala nia njema nasi.
 
Back
Top Bottom