DOKEZO Serikali itazameni Ofisi ya Msajili wa Hati ya Dar es Salaam

DOKEZO Serikali itazameni Ofisi ya Msajili wa Hati ya Dar es Salaam

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Joined
Oct 29, 2024
Posts
2
Reaction score
2
Serikali inapambana sana kusaidia wananchi wapate HATI zao kwa wakati. Wizara ya Ardhi imekuwa mstari wa mbele sana kuhakikisha kilio cha HATI kinaisha, na tumekuwa mashahidi kwa sasa serikali imeongeza kasi kubwa sana kuhakikisha watu wanapata hati zao. Awamu hii ya sita imekuwa mstari wa mbele sana kutoa Hati kwa wakati, na juzi tumeona Mkuu wa mkoa wa Dar alifanya ziara usiku wizara ya Ardhi na kupokelewa na Katibu Mkuu. Tumeona Hati zinatolewa hadi usiku (usiku wa manane)!

Ila moja ya watu wanaokwamisha juhudi hizi ni MSAJILI. Huu ni mwezi wa nne, hadi sasa tunaangaika na msajili apitishe hati zetu, ila imeshindikana. Kauli anazotoa siyo nzuri; kupitisha file tupate nambari ya malipo (control number) ni kitendo cha muda mfupi, hata dakika moja haifiki, ila ni miezi sasa file limekwama kwa msajili.

Tunamuomba waziri wa wizara husika, sisi ni wale tumekosa ajira, tumejiajiri, tumepambana, tumejenga, tumeingia katika mikopo bank na tunategemea hii mikopo kuendesha maisha. Hadi sasa mikopo yetu haijakamilika, tunasubiri hati ili bank ipitishe mikopo yetu; ni miezi sasa tumekwama. Kauli ya mwisho ya Msajili alisema TUSIMFUNDISHE KAZI, hadi leo hatujui ni lini msajili atapitisha haya mafaili. TEGEMEO LETU LA MWISHO NI HII POST!

SERIKALI TUNAOMBA ANGALIENI HILI SUALA KWA UNYETI SANA OFISI YA MSAJILI HAPO DAR ES SALAAM. Watu wamekwama; moja ya mtu aliekwama ni hawa wanaosubiri msajili apitishe hati zao wakachukue mkopo wampeleke mzazi wao katika matibabu nje! Wote sisi tumekwama; serikali TUNAOMBA SANA MTUSAIDIE KATIKA HILI!

Wizara ya Ardhi

a24f7952-4570-449a-abae-a6de10f563da.jpeg
 
Pole na hongera kwa hatua uliyofikia mimi kuna eneo nilinunua hapajapimwa wakaja watu (kampuni ya urathimishaji) hawa walioletwaga na waziri wa ardhi wakati huo mhe. Lukuvi hao jamaa wakakusanya fedha na hakuna walichofanya na sasa hata hawajulikani walipo na ofisi wamefunga mimi ka eneo kangu ni kakubwa nikawaomba wanitengenezee hati 2 wakikate nusu kwa nusu nikalipa laki 5 ilikuwa hati moja 250000 risiti ya malipo ninayo hivi su naweza kuida wizara ya ardhi manake wao ndio walituletea hao watu
 
Serikali inapambana sana kusaidia wananchi wapate HATI zao kwa wakati. Wizara ya Ardhi imekuwa mstari wa mbele sana kuhakikisha kilio cha HATI kinaisha, na tumekuwa mashahidi kwa sasa serikali imeongeza kasi kubwa sana kuhakikisha watu wanapata hati zao. Awamu hii ya sita imekuwa mstari wa mbele sana kutoa Hati kwa wakati, na juzi tumeona Mkuu wa mkoa wa Dar alifanya ziara usiku wizara ya Ardhi na kupokelewa na Katibu Mkuu. Tumeona Hati zinatolewa hadi usiku (usiku wa manane)!

Ila moja ya watu wanaokwamisha juhudi hizi ni MSAJILI. Huu ni mwezi wa nne, hadi sasa tunaangaika na msajili apitishe hati zetu, ila imeshindikana. Kauli anazotoa siyo nzuri; kupitisha file tupate nambari ya malipo (control number) ni kitendo cha muda mfupi, hata dakika moja haifiki, ila ni miezi sasa file limekwama kwa msajili.

Tunamuomba waziri wa wizara husika, sisi ni wale tumekosa ajira, tumejiajiri, tumepambana, tumejenga, tumeingia katika mikopo bank na tunategemea hii mikopo kuendesha maisha. Hadi sasa mikopo yetu haijakamilika, tunasubiri hati ili bank ipitishe mikopo yetu; ni miezi sasa tumekwama. Kauli ya mwisho ya Msajili alisema TUSIMFUNDISHE KAZI, hadi leo hatujui ni lini msajili atapitisha haya mafaili. TEGEMEO LETU LA MWISHO NI HII POST!

SERIKALI TUNAOMBA ANGALIENI HILI SUALA KWA UNYETI SANA OFISI YA MSAJILI HAPO DAR ES SALAAM. Watu wamekwama; moja ya mtu aliekwama ni hawa wanaosubiri msajili apitishe hati zao wakachukue mkopo wampeleke mzazi wao katika matibabu nje! Wote sisi tumekwama; serikali TUNAOMBA SANA MTUSAIDIE KATIKA HILI!

Wizara ya Ardhi

View attachment 3137981
Kuna mtu kahangaikia kupata hati toka alivokuwa kijana hadi kazeeka na umauti ukamkuta huku hati haijatoka.
 
Back
Top Bottom