Serikali itoe taarifa kuhusu hali ya usalama ya wanajeshi wa Tanzania waliopo DRC

Serikali itoe taarifa kuhusu hali ya usalama ya wanajeshi wa Tanzania waliopo DRC

ACT Wazalendo

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2014
Posts
631
Reaction score
1,577
Chama cha ACT Wazalendo inaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa taarifa rasmi kuhusu hali ya usalama ya wanajeshi wetu walioko katika operesheni za kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Hii inafuatia taarifa za hivi karibuni za kuongezeka kwa mashambulizi ya waasi wa M23, ambao wameingia na kudhibiti mji wa Goma na mashariki mwa DRC.

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali, mapigano haya yamesababisha vifo na majeruhi kwa mamia ya raia na baadhi ya wanajeshi kutoka vikosi vya kulinda amani kupitia Umoja wa Mataifa (MONUSCO) na SADC (SAMIDRC). Nchi kama vile Afrika Kusini imeweka wazi wanajeshi wake waliopoteza maisha wamefikia 9, Malawi 3, Botswana 5 na vingine.
Hali hii imezua wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa vikosi vyetu vilivyoko katika maeneo hayo yenye machafuko.

Tunatambua na kuthamini mchango wa wanajeshi wetu katika kudumisha amani na usalama barani Afrika. Hata hivyo, tunashangazwa na ukimya wa Serikali ya Tanzania kuwajulisha wananchi juu ya hali ya usalama ya wanajeshi wetu na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha usalama wao katika mazingira haya hatarishi.

ACT Wazalendo tunaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukua hatua zifuatazo;

i. Kuwajulisha wananchi kuhusu hali ya usalama ya wanajeshi wetu walioko DRC na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha usalama wao.
ii. Kuhakikisha kuwa wanajeshi wetu wanapata vifaa na msaada unaohitajika ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na usalama.
iii. Kufanya kazi kwa karibu na Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa ili kuhakikisha kuwa amani inarejeshwa haraka katika maeneo yaliyoathirika na machafuko

Mwisho, ni wakati wa Tanzania kutathmini upya msimamo wake wa kushiriki kutuma vikosi ambavyo haviondoi mzizi wa mzozo huu. Vita hivi vinasababishwa na maslahi ya kiuchumi na unyonyaji wa rasilimali za Kongo unaofanywa na makundi ya maslahi na mataifa ya kibepari. Tunapaswa kuweka msisitizo katika kulinda utu na kusimamia haki za watu wa Kongo badala ya kuwa sehemu ya mzunguko huu wa machafuko yanayonufaisha wachache.

Imetolewa na;
Ndg. John Patrick Mbozu
Waziri Kivuli wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Januari 28, 2025
 
Chama cha ACT Wazalendo inaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa taarifa rasmi kuhusu hali ya usalama ya wanajeshi wetu walioko katika operesheni za kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Hii inafuatia taarifa za hivi karibuni za kuongezeka kwa mashambulizi ya waasi wa M23, ambao wameingia na kudhibiti mji wa Goma na mashariki mwa DRC.

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali, mapigano haya yamesababisha vifo na majeruhi kwa mamia ya raia na baadhi ya wanajeshi kutoka vikosi vya kulinda amani kupitia Umoja wa Mataifa (MONUSCO) na SADC (SAMIDRC). Nchi kama vile Afrika Kusini imeweka wazi wanajeshi wake waliopoteza maisha wamefikia 9, Malawi 3, Botswana 5 na vingine.
Hali hii imezua wasiwasi mkubwa kuhusu usalama wa vikosi vyetu vilivyoko katika maeneo hayo yenye machafuko.

Tunatambua na kuthamini mchango wa wanajeshi wetu katika kudumisha amani na usalama barani Afrika. Hata hivyo, tunashangazwa na ukimya wa Serikali ya Tanzania kuwajulisha wananchi juu ya hali ya usalama ya wanajeshi wetu na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha usalama wao katika mazingira haya hatarishi.

ACT Wazalendo tunaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuchukua hatua zifuatazo;

i. Kuwajulisha wananchi kuhusu hali ya usalama ya wanajeshi wetu walioko DRC na hatua zinazochukuliwa kuhakikisha usalama wao.
ii. Kuhakikisha kuwa wanajeshi wetu wanapata vifaa na msaada unaohitajika ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na usalama.
iii. Kufanya kazi kwa karibu na Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa ili kuhakikisha kuwa amani inarejeshwa haraka katika maeneo yaliyoathirika na machafuko

Mwisho, ni wakati wa Tanzania kutathmini upya msimamo wake wa kushiriki kutuma vikosi ambavyo haviondoi mzizi wa mzozo huu. Vita hivi vinasababishwa na maslahi ya kiuchumi na unyonyaji wa rasilimali za Kongo unaofanywa na makundi ya maslahi na mataifa ya kibepari. Tunapaswa kuweka msisitizo katika kulinda utu na kusimamia haki za watu wa Kongo badala ya kuwa sehemu ya mzunguko huu wa machafuko yanayonufaisha wachache.

Imetolewa na;
Ndg. John Patrick Mbozu
Waziri Kivuli wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Januari 28, 2025
Msitarajie serikali dhalimu ya CCM kwamba itaweka takwimu sahihi. Jiandaeni kuipokea miili ya wapendwa wenu.

kagame yuko deadly serious na kuchukua nchi ya DR Congo
 
Daah! DR Congo,kwasasa kunatisha sana,huwa ni furaha mtu akichaguliwa kwenda huko,wengine kwasababu ya maokoto, lakini naona kunakaribia kua kama Somalia.Hela ya huko inaanza kua chungu.
 
Daah! DR Congo,kwasasa kunatisha sana,huwa ni furaha mtu akichaguliwa kwenda huko,wengine kwasababu ya maokoto, lakini naona kunakaribia kua kama Somalia.Hela ya huko inaanza kua chungu.
Kuna mjenda mmoja alifurahi kwenda Kongo na akawa anajitapa kwamba walichanga na wenzie wakakata mpunga ili wapate hiyo nafasi, bahati mbaya alirudi akiwa na mguu mmoja baada ya bomu la kutupwa kumlipukia
 
Kuna mjenda mmoja alifurahi kwenda Kongo na akawa anajitapa kwamba walichanga na wenzie wakakata mpunga ili wapate hiyo nafasi, bahati mbaya alirudi akiwa na mguu mmoja baada ya bomu la kutupwa kumlipukia
Duh
 
Huko ni machinjioni kwasasa, serikali ya CCM inaficha tu.
 
Sasa Serikali yetu ya Chichi emu si inajeshi imara walipeleke😁😁 au wamejaa upepo
 
Kwahiyo nchi zote hizo wamewashindwa M23... Hii sasa dharau.
 
Back
Top Bottom