Serikali itoe tamko au waraka kupunguza adhabu ya fimbo mashuleni;watoto watavunjwa nyonga

Serikali itoe tamko au waraka kupunguza adhabu ya fimbo mashuleni;watoto watavunjwa nyonga

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Bila jitihada za serikali kuweka msisitizo wa kuzuia au kupunguza adhabu ya viboko mashuleni; kuna uwezekano mkubwa wa kuzalisha taifa lenye walemavu wengi!

Binafsi niliwahi kuchapwa enzi hizo nikiwa sekondari kwa kosa la jumla (darasa zima) na walimu karibu 10 kwa wakati mmoja. Nilipata maumivu ya kidole ambayo hadi leo hii kuna wakati kidole hicho huuma!

Hapa miaka ya katikati (wakati wa JK) Adhabu ya viboko ilipungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kampeni ya 'shule rafiki'

Kwa sasa adhabu hii imeshika kasi sana. Wanafunzi wanachapwa kuliko idadi inayotakiwa. Sababu zipo nyingi (kwa mtazamo wangu) ambazo zianweza kuwa:-
•Idadi kubwa ya wanafunzi isiyoendana na idadi ya walimu husika.
•Maslahi duni ya walimu.
•Uwezo mdogo wa kitaaluma/kitaalam kwa baadhi ya walimu na hivyo wanaona viboko ndio njia pekee ya kumfanya mwanafunzi aelewe.
•Majukumu mengi kwa walimu (kuamua kesi za wanafunzi za kupigana, kuibiana nk, kuwa washauri nasaha, kudhibiti nidhamu nk nk)
•mmonyoko mkubwa wa maadili katika jamii. Watoto wengi wanajilea wenyewe kutokana na baadhi ya wazazi kuwa 'busy' kutafuta kipato au kulelewa na wasaidizi wa kazi za nyumbani na hivyo kusababisha kukosa maadili stahiki.

Kuna uwezekano mkubwa walimu wengi hawako sawa kisaikolojia. Kwasababu binadamu aliye sawa hawezi kumuadhibu binadamu mwenzako kiasi cha kumjeruhi. Serikali iingilie kati. Wanafunzi watazidi kuwa wakatili kutokana na ukatili wanaofanyiwa wao katika umri mdogo!
 
Mbona miongozo ipogo tu siku zote

Sema baadhi ya waalimu wanakuwa kama wamevurugwa siku hizi asee. Zamani ilikuwa poa tu mwanafunzi kupigwa kama ng'ombe ila siku hizi waalimu wawe makini sana.

Kuna watu tulipigwa kuliko kupigwa kwenyewe. Waliosoma Tabora Boys wanaelewa maana ya GATUNDU. Ule ni uuwaji na wala sio sifa
 
Bila jitihada za serikali kuweka msisitizo wa kuzuia au kupunguza adhabu ya viboko mashuleni; kuna uwezekano mkubwa wa kuzalisha taifa lenye walemavu wengi!

Binafsi niliwahi kuchapwa enzi hizo nikiwa sekondari kwa kosa la jumla (darasa zima) na walimu karibu 10 kwa wakati mmoja. Nilipata maumivu ya kidole ambayo hadi leo hii kuna wakati kidole hicho huuma!

Hapa miaka ya katikati (wakati wa JK) Adhabu ya viboko ilipungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kampeni ya 'shule rafiki'

Kwa sasa adhabu hii imeshika kasi sana. Wanafunzi wanachapwa kuliko idadi inayotakiwa. Sababu zipo nyingi (kwa mtazamo wangu) ambazo zianweza kuwa:-
•Idadi kubwa ya wanafunzi isiyoendana na idadi ya walimu husika.
•Maslahi duni ya walimu.
•Uwezo mdogo wa kitaaluma/kitaalam kwa baadhi ya walimu na hivyo wanaona viboko ndio njia pekee ya kumfanya mwanafunzi aelewe.
•Majukumu mengi kwa walimu (kuamua kesi za wanafunzi za kupigana, kuibiana nk, kuwa washauri nasaha, kudhibiti nidhamu nk nk)
•mmonyoko mkubwa wa maadili katika jamii. Watoto wengi wanajilea wenyewe kutokana na baadhi ya wazazi kuwa 'busy' kutafuta kipato au kulelewa na wasaidizi wa kazi za nyumbani na hivyo kusababisha kukosa maadili stahiki.

Kuna uwezekano mkubwa walimu wengi hawako sawa kisaikolojia. Kwasababu binadamu aliye sawa hawezi kumuadhibu binadamu mwenzako kiasi cha kumjeruhi. Serikali iingilie kati. Wanafunzi watazidi kuwa wakatili kutokana na ukatili wanaofanyiwa wao katika umri mdogo!
Sahihi ila waangalie namna adhabu zinavyotokewa za viboko. NB; viboko ni muhimu Ila kwa utaratib maalum!!
 
Mbona miongozo ipogo tu siku zote

Sema baadhi ya waalimu wanakuwa kama wamevurugwa siku hizi asee. Zamani ilikuwa poa tu mwanafunzi kupigwa kama ng'ombe ila siku hizi waalimu wawe makini sana.

Kuna watu tulipigwa kuliko kupigwa kwenyewe. Waliosoma Tabora Boys wanaelewa maana ya KATUNDU. Ule ni uuwaji na wala sio sifa
I see!
Na ujue ukatili unaanzia katika umri mdogo
 
Walimu pigeni kadiri muwezavyo?tena nashauri ktk vyuo vya ualimu wafundishwe judo!viboko havitoshi!maana madogo wa sikuhizi wanajifanya wamepinda.
 
Walimu pigeni kadiri muwezavyo?tena nashauri ktk vyuo vya ualimu wafundishwe judo!viboko havitoshi!maana madogo wa sikuhizi wanajifanya wamepinda.
Na wanapigika kwelikweli!
 
Walimu wana mafrastruation + mastress+madipression
Hasira zao za maisha wanazihamishia
Kwa wanafunzi
Walimu mtaishiaaa sana jelaaaaa

Ova
 
Walimu wana mafrastruation + mastress+madipression
Hasira zao za maisha wanazihamishia
Kwa wanafunzi
Walimu mtaishiaaa sana jelaaaaa

Ova
Wanaoenda jela ni wale wanaobainika. Na wasiobainika je?
Ambao ni wengi kuliko waendao jela
 
Unaweza ukatumia ukali ama upendo na bado ukatibu tatizo.
Kwa Nini walimu wasitoe adhabu constructive like kusafisha vyoo,mazingira ama kufagia darasa mwezi mzima so wengine Wana relax.

Ama mwalimu ampe mwanafunzi maswali kibao ya hesabu ama fizikia ayafanye na baadaye majibu yake afanye presentation mbele ya darasa Zima.
Yaani hata upendo huwa Ni silaha tosha ndio nayotumia.
Mana Kama unaishi vizuri kabisa na watu kiupendo nakuhakikishia wevi na wachawi nyumba yako watairuka na hawataigusa Mana hata maandiko yanatuhaidi hivyo kabisa.


Mie Nina wito na ualimu sema Ile maslahi huwa yananikataga ngebe kusema ukweli.

Pia walimu wanatakiwa wafundishwe emotions intelligence otherwise hasira zao za mek ama wakubwa zake anahamishia kwa watoto wa watu.

Mktaba Ni umfundishe nidhamu yenyewe mwalimu inamshinda kuwa nayo ama watoto wake mwenyewe wanamshindwa kuwaonyoosha ujue so why uhangaike na mtt usiyejua asili ya Koo yake. Kikubwa andika recommendation kwa mzazi wake ili ajue how to deal him or her Basi kwani akipinda wewe una hasara gani.

Hao akina jk si walifundishwa na akina Mandela ama nyerere lakini nidhamu iko wapi cheki viongozi wanavyotuibia Mali zetu , wengine wanaziweka rehani kuokoa maisha ya watt wao.


So nidhamu ama heshima Ni innate character Kuna watt wazazi wao Ni mashekhe ama mapadri ama wachungaji Ila utakuta wanaiba wanavuta bangi Ni Malaya na Ni wavivu was kufanya kazi . So Hawa walikosa malezi ama
 
Bila jitihada za serikali kuweka msisitizo wa kuzuia au kupunguza adhabu ya viboko mashuleni; kuna uwezekano mkubwa wa kuzalisha taifa lenye walemavu wengi!

Binafsi niliwahi kuchapwa enzi hizo nikiwa sekondari kwa kosa la jumla (darasa zima) na walimu karibu 10 kwa wakati mmoja. Nilipata maumivu ya kidole ambayo hadi leo hii kuna wakati kidole hicho huuma!

Hapa miaka ya katikati (wakati wa JK) Adhabu ya viboko ilipungua kwa kiasi kikubwa kutokana na kampeni ya 'shule rafiki'

Kwa sasa adhabu hii imeshika kasi sana. Wanafunzi wanachapwa kuliko idadi inayotakiwa. Sababu zipo nyingi (kwa mtazamo wangu) ambazo zianweza kuwa:-
•Idadi kubwa ya wanafunzi isiyoendana na idadi ya walimu husika.
•Maslahi duni ya walimu.
•Uwezo mdogo wa kitaaluma/kitaalam kwa baadhi ya walimu na hivyo wanaona viboko ndio njia pekee ya kumfanya mwanafunzi aelewe.
•Majukumu mengi kwa walimu (kuamua kesi za wanafunzi za kupigana, kuibiana nk, kuwa washauri nasaha, kudhibiti nidhamu nk nk)
•mmonyoko mkubwa wa maadili katika jamii. Watoto wengi wanajilea wenyewe kutokana na baadhi ya wazazi kuwa 'busy' kutafuta kipato au kulelewa na wasaidizi wa kazi za nyumbani na hivyo kusababisha kukosa maadili stahiki.

Kuna uwezekano mkubwa walimu wengi hawako sawa kisaikolojia. Kwasababu binadamu aliye sawa hawezi kumuadhibu binadamu mwenzako kiasi cha kumjeruhi. Serikali iingilie kati. Wanafunzi watazidi kuwa wakatili kutokana na ukatili wanaofanyiwa wao katika umri mdogo!
Hatari sana
 
Ujinga mtupu tembelea vituo vya polisi uone watuhumiwa wanavyotesa au nenda segerea ukawacheki mahabusu wenye miaka 10 mpk 15 wakuambie...

Nyie wanaharakati Uchwara mliosomea kwenye shule za magari ya njano wengi Wenu hamna kitu kabisa...

Waacheni walimu wapige kazi wanamiongozo yao .

..
 
Ujinga mtupu tembelea vituo vya polisi uone watuhumiwa wanavyotesa au nenda segerea ukawacheki mahabusu wenye miaka 10 mpk 15 wakuambie...

Nyie wanaharakati Uchwara mliosomea kwenye shule za magari ya njano wengi Wenu hamna kitu kabisa...

Waacheni walimu wapige kazi wanamiongozo yao .

..
Kumbuka wanafunzi sii wafungwa wa uhalifu japo hata hao wafungwa wana haki zao.
 
Mimi ni ticha na Huwa sichapi na Kwa jina la Mungu nachukia mno maticha washamba wanaochapa na ninajua sana jinsi wanafunzi wanavyoudhi na kuchokoza maticha ila denti akikosea kosa kubwa na akalirudia basi naongea nae sana masaa matatu namsimulia stori zangu zote Kila nilikopita niliona Nini nikafaidi Nini ukorofi una madhara gani mifano ya wakorofi Dunia nzima na kilichowatokea basi nitaongea mimi ticha tu mpaka denti itamboa kinoma mi nimo tu adhabu ya kuongea ikiisha denti anaenda , nakwambia harudii tena Hilo kosa na hata akiniona Kwa mbali tu anakata Kona Kwa kujiona mshamba tu. Denti Anajua last time tulikaa 3 hours akirudia kosa tunaweza kukaa the whole day nikijisifia tu!!!!

Kumchapa Mtoto ni kuthibitisha uwezo mdogo wa kiakili na kisaikolojia wa ticha kushindwa kutambua na kutumia adhabu mbadala ambazo ziko kibao! Kuchimba shimo, kugonga kengele Kila kipindi, kufyeka nyasi, kupokea wageni getini siku nzima nk

Unamchapaje mtu anaejitambua na kupata akili zote kutoka social media Kwa mfano? Mtu Yuko insta mda wote, kajaza picha tik tok, ana page YouTube na Facebook. Huyu ni WA kumkalisha na kimuelewesha tu sio kumchapa.
 
Adhabu ya viboko mashuleni ifutwe maana kuna walimu wanajiona wanataka kubadili tabia na mienendo mibovu ya wanafunzi kwa nia njema ndio hao baadae serikali na jamii inawachukia. Walimu acheni adhabu ya viboko wapeni watoto adhabu angalau ya ya kunakili kitabu cha ngoswe penzi kitovu cha uzembe au mabala the farmer, over
 
kapuyasekondari ilioko wilayani Kaliua waalimu hujipanga kuchapa viboko wakiongozwa na mkuu washule. mwanadunzi akiingizwa ofisini ndio kiama chake
 
Back
Top Bottom