Pre GE2025 Serikali kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuijenga upya kwa Trilioni 1.2

Pre GE2025 Serikali kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuijenga upya kwa Trilioni 1.2

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Serikali imedhamiria kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuijenga upya, ili kuwezesha huduma zote kutolewa ndani ya jengo moja litakalokuwa na vitanda 1,757 kutoka 1,435 vya sasa ambapo mradi huo utagharimu USD .468 Mil (takribani TZS. 1.2 Trilioni), ambapo kati ya fedha hizo USD.364 Mil zitatoka Korea Kusini na Serikali ya Tanzania itachangia USD. 104 Mil.

Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji Dkt. Rachel Mhaville kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH wakati akitoa taarifa kwa umma juu ya mafanikio ya kipindi cha miaka minne chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa kwa sasa upembuzi yakinifu wa mradi huo umekamilika hivyo hatua mbalimbali za kusaini mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Korea zinaendelea vizuri.

Soma pia: Pre GE2025 Miradi kuelekea Uchaguzi Mkuu: Mhandisi Kundo akagua mradi wa maji unaonufaisha zaidi ya wakazi 200,000 Chalinze

Hospitali ya Taifa Muhimbili yenye kampasi mbili ni Hospitali ya Rufaa ya Kitaifa na kubwa kuliko zote nchini ina vitanda 2,043 ambapo Upanga kuna vitanda 1,435 na Mloganzila vipo 608.Katika kampasi zote mbili wagonjwa 4,000 wanaonwa kwa siku.
1741255400462.png


 

Attachments

  • 1741255382362.png
    1741255382362.png
    229.7 KB · Views: 1
Serikali imedhamiria kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuijenga upya, ili kuwezesha huduma zote kutolewa ndani ya jengo moja litakalokuwa na vitanda 1,757 kutoka 1,435 vya sasa ambapo mradi huo utagharimu USD .468 Mil (takribani TZS. 1.2 Trilioni), ambapo kati ya fedha hizo USD.364 Mil zitatoka Korea Kusini na Serikali ya Tanzania itachangia USD. 104 Mil.

Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji Dkt. Rachel Mhaville kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH wakati akitoa taarifa kwa umma juu ya mafanikio ya kipindi cha miaka minne chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa kwa sasa upembuzi yakinifu wa mradi huo umekamilika hivyo hatua mbalimbali za kusaini mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Korea zinaendelea vizuri.

Hospitali ya Taifa Muhimbili yenye kampasi mbili ni Hospitali ya Rufaa ya Kitaifa na kubwa kuliko zote nchini ina vitanda 2,043 ambapo Upanga kuna vitanda 1,435 na Mloganzila vipo 608.Katika kampasi zote mbili wagonjwa 4,000 wanaonwa kwa siku.View attachment 3261100
Afadhali huduma zote zipatikane sehemu moja maana unaweza kutoka maabara kwenda wodini safari kama ya kimara hadi manzese
 
Watuambie kwanza kuna uhitaji huo?Je vitanda vilivyopo havitoshi?na Je hatuwezi Hospitali nyingine kubwa ili kuipunguzia mzigo Muhimbili?
 
Serikali imedhamiria kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuijenga upya, ili kuwezesha huduma zote kutolewa ndani ya jengo moja litakalokuwa na vitanda 1,757 kutoka 1,435 vya sasa ambapo mradi huo utagharimu USD .468 Mil (takribani TZS. 1.2 Trilioni), ambapo kati ya fedha hizo USD.364 Mil zitatoka Korea Kusini na Serikali ya Tanzania itachangia USD. 104 Mil.
Kwanini isijengwe nyingine mahali pengine ndani ya Dsm na hiyo ikabakia kama hospitali ya kawaida
 
Duh ni pesa mingi ambapo ingejenga tu mpya hospital mikoani mfano Lindi na songea na masasi na tabora na manyara
Kufanya hivyo itakuwa ni kupoteza pesa, huko lindi songea hakuna pesa ya kuihudumia hospitali yenye ukubwa wa muhimbili.

Kumbuka hospitali hizi kwa asilimia zote zinatakiwa zijiendeshe zenyewe.
Na nikupitia mapato ya fees za wagonjwa.
 
Kwa muhimbili ilivyojengwa kama slums ni bora ijengwe upya kubadilisha mandhari ya mjini hapo, ila ingeleta tija sana kama wangeongeza brand new hosp nje ya mji kupunguza congestion maana hayo mafoleni yataongezeka balaa!
 
Mkopo mwingine huo,
Sipati picha muchemba anavyofurahi huko
wapigaji hawakosekani hapo
 
Badala ya kujenga hospitali moja kubwa sehemu moja ni afadhari wakajenga mbili sehemu tofauti. Moja iwe Dodoma na nyingine Dar zenye thamani ya pesa hiyo.
 
Kwa nini hiyo pesa isitumike kuboresha huduma na maslahi ya wahudumu wa afya? Kuikarabati hospital kwa trillion 1.2 ni sawa na kukarabati gari bovu T253 AAA huku ukiendelea kutumia oil chafu kwenye gari hiyo hiyo baada ya ukarabati. Bata wahed!
 
Serikali imedhamiria kuboresha Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kuijenga upya, ili kuwezesha huduma zote kutolewa ndani ya jengo moja litakalokuwa na vitanda 1,757 kutoka 1,435 vya sasa ambapo mradi huo utagharimu USD .468 Mil (takribani TZS. 1.2 Trilioni), ambapo kati ya fedha hizo USD.364 Mil zitatoka Korea Kusini na Serikali ya Tanzania itachangia USD. 104 Mil.

Hayo yameelezwa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji Dkt. Rachel Mhaville kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa MNH wakati akitoa taarifa kwa umma juu ya mafanikio ya kipindi cha miaka minne chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa kwa sasa upembuzi yakinifu wa mradi huo umekamilika hivyo hatua mbalimbali za kusaini mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Korea zinaendelea vizuri.

Hospitali ya Taifa Muhimbili yenye kampasi mbili ni Hospitali ya Rufaa ya Kitaifa na kubwa kuliko zote nchini ina vitanda 2,043 ambapo Upanga kuna vitanda 1,435 na Mloganzila vipo 608.Katika kampasi zote mbili wagonjwa 4,000 wanaonwa kwa siku.View attachment 3261100
Kuna harufu kubwa ya ufisadi kwenye mradi huu
 
Ingependeza kama ingejengwa hospital nyingine mpya nje ya mji kama bagamoyo huko
 
Back
Top Bottom