Serikali kudhibiti Madaktari wanaofanya kazi kwenye Kituo zaidi ya kimoja

Serikali kudhibiti Madaktari wanaofanya kazi kwenye Kituo zaidi ya kimoja

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

View: https://www.youtube.com/watch?v=7xmj6NSToGE


Kutokana na kuwapo idadi kubwa ya madaktari vijiweni, Serikali imesema ipo katika mchakato wa ufumbuzi wa tatizo hilo, ikigusia kuwa itaanza kudhibiti wale wanaofanya kazi hospitali zaidi ya moja na vituo vya afya binafsi.

Zaidi ya madaktari 5,000 waliohitimu na kuwa na sifa za kuajiriwa, bado wanaendelea kusota mtaani kwa kukosa ajira rasmi, wanaokadiriwa kutumia zaidi ya Sh450 bilioni kusomea fani hiyo.

Hayo yamesemwa leo Jumanne, Julai 30, 2024 na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu katika Kongamano la Kumbukizi ya Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, hayati Benjamini Mkapa linalofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Waziri Ummy amesema madaktari wameruhusiwa kuanzisha hospitali zao baada ya muda wa kazi, lakini kinachoonekana sasa daktari mmoja anafanya kazi zaidi ya vituo viwili, hivyo kuminya ajira za madaktari wengine waliopo mtaani.

“Kama kwenye mpira wachezaji wa nje wasizidi kadhaa, inakuja na kwenye sekta ya afya kama una hospitali tutakupa maelekezo, asilimia kadhaa ya unaowaajiri wasiwe kwenye ajira za kudumu, mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sasa tunafanya uchambuzi tutakuja kwako baada ya kuwa tumemaliza huu uchambuzi,” amesema Waziri Ummy akimfahamisha Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa.

Chanzo: Mwananchi
 
Wawaongezee maslahi watatulia.ukiona mtu anahangaika na party time from main job ujue maslahi ni kidogo.

Nani anapenda ku overwork. Yaani utoke kazini badala ya kupumziki unaingiq viniwenu,labda ukiacha wale Madokta wenye vituo vyao vye afya
 
Waziri anaongea kitu ambacho hakiwezekani. Waziri apige kelele kwenye kuboresha maslahi ya Drs kwanza. Nadhani hakuna Dr ambaye anapenda kufanya kijiwe kama analipwa stahiki zake vizuri.
 
Madaktari ni wajinga tu acha wafanywefanywe.
 
Back
Top Bottom