Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 2,203
- 5,610
Serikali ya Ecuador imeanza kuichunguza hospitali aliyokuwa akitibiwa bibi mmoja ambaye alitangazwa amekufa lakini aliamka ndani ya jeneza Ijumaa iliyopita.
Bella Montonya (76) ambaye madaktari walithibitisha kifo chake aligundulika yupo hai baada ya mtoto wake kusikia kelele zikitokea kwenye jeneza wakati wa maandalizi ya mazishi.
Bibi huyo alikuwa akigongagonga ndipo walipoenda kutizama na kumkuta akiwa anapumua kwa nguvu, walimtoa na kumkimbiza hospitali huku waombolezaji wakibaki na mshtuko mkubwa.
Kamati maalumu imeundwa kupitia upya mchakato unaofanywa na hospitali za nchini humo mpaka kutoa cheti cha kifo.
Bella Montonya (76) ambaye madaktari walithibitisha kifo chake aligundulika yupo hai baada ya mtoto wake kusikia kelele zikitokea kwenye jeneza wakati wa maandalizi ya mazishi.
Bibi huyo alikuwa akigongagonga ndipo walipoenda kutizama na kumkuta akiwa anapumua kwa nguvu, walimtoa na kumkimbiza hospitali huku waombolezaji wakibaki na mshtuko mkubwa.
Kamati maalumu imeundwa kupitia upya mchakato unaofanywa na hospitali za nchini humo mpaka kutoa cheti cha kifo.