Serikali kumlipa Mshahara kocha wa Taifa Stars

Serikali kumlipa Mshahara kocha wa Taifa Stars

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Waziri wa Utamaduni, Sana na Michezo Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuendeleza mchezo wa Soka nchini itamlipa mshahara mwalimu wa Timu ya Taifa (Taifa Stars), Adel Amrouche ambaye ni raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria.

Hayo yamebainishwa wakati wa kumtambulisha Kocha huyo, Machi 07, 2023 Mtumba jijini Dodoma na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo ambapo Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali inaamini Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limejiridhisha kuwa ni Kocha Bora atakayekuza soka la Tanzania.

Dkt. Chana ameongeza kuwa, Serikali inaendelea kuangalia uwezekano wa kupata Wataalamu katika michezo mingine ambapo ameeleza kuwa Wizara inaendelea kuimarisha Wataalamu wa michezo kupitia Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kilichopo wilayani Kwimba mkoani Mwanza.

Kwa upande wake Kocha Amrouche ameahidi kuwanoa wachezaji vyema ili kuiweka juu zaidi Tanzania katika ulimwengu wa Soka , huku akisisitiza ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali katika kufanikisha kazi yake.

WhatsApp Image 2023-03-07 at 12.58.40.jpeg
 
Ni muendelezo tu ule ule wa kuzichezea hela za walipa kodi. Hakuna tija yoyote ile itakayoletwa na huyo kocha kwenye mpira wa miguu nchini.
 
Kwani mwanzo alikuwa nani analipa mishahara ila siasa kweli ni kitu cha ajabu.
 
Waziri wa Utamaduni, Sana na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuendeleza mchezo wa Soka nchini itamlipa mshahara mwalimu wa Timu ya Taifa (Taifa Stars), Adel Amrouche ambaye ni raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria .

Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa hafla ya kumtambulisha Kocha huyo, Machi 07, 2023 Mtumba jijini Dodoma, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema Serikali inaamini Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limejiridhisha kuwa ni Kocha Bora atakayekuza soka la Tanzania.

"Ukitazama wasifu wa Kocha Adel utabaini uzoefu mkubwa alionao sio tuu katika kufundisha soka uwanjani, bali pia katika kuandaa Wataalamu wengine wa Soka, hivyo tumtumie vizuri ili asaidie timu yetu kufanya vizuri ndani na nje ya nchi"

Ameongeza kuwa, Serikali inaendelea kuangalia uwezekano wa kupata Wataalamu katika michezo mingine ambapo ameeleza kuwa Wizara inaendelea kuimarisha Wataalamu wa michezo kupitia Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya kilichoko wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Kwa upande wake Kocha Amrouche ameahidi kuwanoa wachezaji vyema ili kuiweka juu zaidi Tanzania katika ulimwengu wa Soka, huku akisisitiza ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali katika kufanikisha kazi yake.View attachment 2541141View attachment 2541142View attachment 2541143View attachment 2541144View attachment 2541145View attachment 2541147View attachment 2541146
IMG-20230307-WA0121.jpg
 
Kwahiyo 10 percent atakuwa anatoa TFF au WIZARANII?
 
Ni muendelezo tu ule ule wa kuzichezea hela za walipa kodi. Hakuna tija yoyote ile itakayoletwa na huyo kocha kwenye mpira wa miguu nchini.
Mambo Yale Yale ya Kikwete,Ina maana Hadi Leo tff haijawa na uwezo wa kumlipa kocha!Je,itawezaje kugharimia Kambi za timu na posho za wachezaji?
 
Back
Top Bottom