Serikali kupitia BoT, iruhusu watumishi wa umma wanaolipwa posho za mwezi kukopa kupitia posho zao

Serikali kupitia BoT, iruhusu watumishi wa umma wanaolipwa posho za mwezi kukopa kupitia posho zao

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kwa wale watumishi wa umma ambao taasisi zao huwalipa posho kila mwezi(mfano JWTZ, Polisi, n.k), wakati umefika waruhusiwe kukopa kupitia posho hizo kwa kukatwa sehemu ya posho zao kulipa mikopo watayochukua.

Tofauti na mikopo kupitia mishahara ambayo huwa ni ya muda mrefu (miaka 7 mpaka 8), mikopo kupitia allowance za kila mwezi, inaweza kuwa ni ya muda mfupi (mfano miezi 6 mpaka miaka 2).

Hii ni kwasababu, mishahara serikalini ni midogo na wakati huo huo, watumishi wananabwa na sheria inayowataka wabaki na walau moja ya tatu ya mishahara yao baada ya makato yote yakiwemo makato ya lazima kama Bima na ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Matokeo ya hali hii ni watumishi kupata mikopo midogo isiyolingana na mahitaji yao, na kuwafanya wengi kukimbilia katika microfinance ambazo licha ya kutowapa mikopo mikubwa, bali hutoa mikopo yenye riba kubwa na hata kufanya ile dhana ya mtumishi kubaki na moja ya tatu kuwa ni nadharia tu kwani mtumishi hulazimika kutumia mshahara huo huo kulipa mikopo ya mabenki na ya hizi financial institutions.

Hivyo, kwa wale watumishi wanaoweza kukopa kupitia posho zao za kila mwezi ambazo nazo hulipwa kupitia akaunti zao katika mabenki, wakati umefika waruhusiwe kukopa mikopo ya muda mfupi kupitia allowance zao za kila mwezi.

Tena, kama inawezekan, mtumishi aruhusiwe kutumia mshahara na allowance yake vyote kwa pamoja kupata mkopo na kwenye allowance, mtumishi aruhusiwe hata kukopea allowance yote mradi kaamua mwenyewe.

Mfano, mtumish ana allowance ya shilingi 300,000 kwa mwezi, na kupitia mshahara wake, anaweza pia kutumia shilingi 200,000 kukopea, maana yake mtumishi kama huyu, akiamua, anaweza kutumia shilingi 200,000 ya posho na hiyo 200,000 ya mshahara wke akapata jumla ya shilingi 400,000 kwa mwezi, kiasi anachoweza kwenda Benki na akachukua mkopo wa muda mfupi na akapata hela nzuri tu na akafanya mambo yake?

Jambo hili mimi naamini linawezekana iwapo serikali kupitia BOT, Utumishi na mabenki, watakaa pamoja na kulifanyia kazi wazo hili.

Watumishi wengi kwa sasa hawakopesheki katika mabenki kutona na sheria ya moja ya tatu(tusisahau pia kwa miaka 6 mshahara haijaongezwa) na hata wengi wa wanaokopesheke huishia kuchukua mkopo juu ya mkopo mwingine(top- up) na matokeo ni watu kupata vihela vidogo visivyokidhi mahitaji yao.

Mwisho, sheria ya mtumishi kutakiwa kubaki na moja ya tatu ya mshahara wake, nayo ipitiwe upya kwani haikuzingatia tofauti ya mishahara iliyopo baina ya watumishi na uhuru wa mtumishi kutumia mshahara wake kadri anayotoka.

Pia, kwakuwa mishahara serikalini ni midogo na haikidhi mahitaji, serikali iwaache watumishi kuamua ni namna gani watatumia mishahara yao kuendesha maisha yao.

Kumjali mtumishi sio kwa kumuwekea sheria ya kumlazimisha kubaki na moja ya tatu ya basic salary yake, bali ni kwa kuboresha masilahi yake( mtu miaka 6 mshahara ule ule halafu bado unampangia matumizi?).Haingii akilini.

CC: mwigulu nchemba
 
Ila wewe jamaa unastahili kabisa nushaninya KULALAMIKA.

Wanaoishi na wewe nawapongeza sana.

Unalalamikia kila kitu yaani.

Anyway, kuhusu mtumishi kubaki na 1/3 ya mshahara wake ni muhimu zaidi kwa kwake.

Kwani serikali inapata faida gani kuhakaikisha mtumishi anabakiwa na 1/3 ya mshahara wake??

Kuna kipindi nilienda Tanga mwaka 2014 nilikuta kuna watumishi wamekopa mpaka hawapati mshahara hata 100!!!

Sasa kwa mtu asiyepata mshahara anaishi vipi, na kazi atafanyaje ??

Hapo ndipo maDED wakataka kila mtumishi akitaka kukopa barua yake ipite kwao waone baada ya kukopa watabakiwa na kiasi gani ili kuepusha huo utaahira.

Leo umekopa mshahara umeisha unataka eti kukopea mpaka posho, hii ni akili timamu kweli ??

Kwanza kwa taratibu za wanajeshi, hakuna posho tu.

Hakuna just posho tu. Watu wqnapewa pesa kwaajili ya vinywaji. Suala la wewe kuinadilishia matumizi ni wewe sasa unataka Jeshi wao ndio wabadilishe matumizi ?

Suala la pesa ya vinywaji siyo mshahara na wanaweza kuamua pia kuitoa kwa njia nyingine kama ilivyowahi kutolewa huko nyuma.

Yaani mtu, umeokopea mshahara umemaliza, hakuna ulichofanya, umekopa salary advance umemaliza. Umechukua ATM kadi umeweka bond umekopa mtaani umemaliza na saa unataka kukopea posho umalize.

Baada ya hapo uanze kulaumu serikali.

Aiseee. Binadamuuu

FB_IMG_1637482991302.jpg
 
Ila wewe jamaa unastahili kabisa nushaninya KULALAMIKA.

Wanaoishi na wewe nawapongeza sana.

Unalalamikia kila kitu yaani.

Anyway, kuhusu mtumishi kubaki na 1/3 ya mshahara wake ni muhimu zaidi kwa kwake.

Kwani serikali inapata faida gani kuhakaikisha mtumishi anabakiwa na 1/3 ya mshahara wake??

Kuna kipindi nilienda Tanga mwaka 2014 nilikuta kuna watumishi wamekopa mpaka hawapati mshahara hata 100!!!

Sasa kwa mtu asiyepata mshahara anaishi vipi, na kazi atafanyaje ??

Hapo ndipo maDED wakataka kila mtumishi akitaka kukopa barua yake ipite kwao waone baada ya kukopa watabakiwa na kiasi gani ili kuepusha huo utaahira.

Leo umekopa mshahara umeisha unataka eti kukopea mpaka posho, hii ni akili timamu kweli ??

Kwanza kwa taratibu za wanajeshi, hakuna posho tu.

Hakuna just posho tu. Watu wqnapewa pesa kwaajili ya vinywaji. Suala la wewe kuinadilishia matumizi ni wewe sasa unataka Jeshi wao ndio wabadilishe matumizi ?

Suala la pesa ya vinywaji siyo mshahara na wanaweza kuamua pia kuitoa kwa njia nyingine kama ilivyowahi kutolewa huko nyuma.

Yaani mtu, umeokopea mshahara umemaliza, hakuna ulichofanya, umekopa salary advance umemaliza. Umechukua ATM kadi umeweka bond umekopa mtaani umemaliza na saa unataka kukopea posho umalize.

Baada ya hapo uanze kulaumu serikali.

Aiseee. Binadamuuu
Hiyo moja ya tatu mnayoihubiri unafikiri ina uhalisia? Mtu ana take home ya 300,000 au 200,000 unafikiri hiyo habari ya moja ya tatu itawezekana? Mtu huyo atalazimika kukopa mitaani tena sometimes kwa riba kuwa tu na mshahara ukitoka anaishia kulipa madeni.

Halafu mtu mwenye basic salary ya mfano shilingi 1,500,000 na mtu mwenye basic salary ya shilingi 300,000, au hata 500,000 ,kwanini wote uwabane wabaki na moja ya tatu baada ya makato yote ili hali wana gap kubwa kiasi hicho?
 
Hiyo mikopo mbona ipo CRDB toka muda sana lkn, kikubwa mwajiri wako aaainishe aina ya posho unazolipwa kila mwezi na kiasi chake na mshahara wako sharti upitie ktk benki husika. Mkopo unaenda 85-150Mil, wale wenye wajomba zet watumishi tunapata mteremko kupitia mikopo yao ya aina hii. Kikubwa ni uaminifu tu maisha yanasonga
 
Hiyo mikopo mbona ipo CRDB toka muda sana lkn, kikubwa mwajiri wako aaainishe aina ya posho unazolipwa kila mwezi na kiasi chake na mshahara wako sharti upitie ktk benki husika. Mkopo unaenda 85-150Mil, wale wenye wajomba zet watumishi tunapata mteremko kupitia mikopo yao ya aina hii. Kikubwa ni uaminifu tu maisha yanasonga
Labda kwa wafanyakazi wa sekta binafsi lakini sio serikalini. Na kama ni serikalini, basi sio kwa wizara na idara zote.


Ubunifu ni tatizo kubwa sana nchi hii hasa kwa wenye dhamana na mamlaka mbalimbali na ndio maana mpaka leo tuna mgao wa umeme.

Hata vitu kama salary advance bila shaka ni ubunifu wa watu kutoka nje(tumeiga) na mtu angetoa wazo la salary advanve humu nchinii, si ajabu asingepata watu wa kumuunga mkono mpaka mambo yaanzie kwa wenzetu ndio tuige.
 
Hiyo moja ya tatu mnayoihubiri unafikiri ina uhalisia? Mtu ana take home ya 300,000 au 200,000 unafikiri hiyo habari ya moja ya tatu itawezekana? Mtu huyo atalazimika kukopa mitaani tena sometimes kwa riba kuwa tu na mshahara ukitoka anaishia kulipa madeni.

Halafu mtu mwenye basic salary ya mfano shilingi 1,500,000 na mtu mwenye basic salary ya shilingi 300,000, au hata 500,000 ,kwanini wote uwabane wabaki na moja ya tatu baada ya makato yote ili hali wana gap kubwa kiasi hicho?
Lengo ni kuhakikisha mtu hakopi pesa yote.

Sasa unataka kykopa pesa yote halafu utaishi vipi ???

Kwa kuomba omba ??

Kwani ukikopa mtaani pesanyoyenukaenda kulip maadeni, unakuwa unamkomoa nani ??

Mtu mzima na akili zake, kama ameahindwa kulinda maisha yake ya kipato unataka apelekwe polisi kwa kuomba omba ??
 
Lengo ni kuhakikisha mtu hakopi pesa yote.

Sasa unataka kykopa pesa yote halafu utaishi vipi ???

Kwa kuomba omba ??

Kwani ukikopa mtaani pesanyoyenukaenda kulip maadeni, unakuwa unamkomoa nani ??

Mtu mzima na akili zake, kama ameahindwa kulinda maisha yake ya kipato unataka apelekwe polisi kwa kuomba omba ??
Hivi mishahara serikalini unaijua wewe?

Mtu ana take home ya shilingi 300,000 huku nauli ya kwenda kazini,chakula pamoja na maji kwa siku akijibana sana katumia shilingi 5,000 ambayo ni 150,000 kwa mwezi. Sasa mtu kama huyu unadhani hiyo sheria ya moja ya tatu inamlinda kivipi?
 
Mleta mada hujielewi kabisa mkopo Ni Kati ya mkopaji na mkopeshaji tu hakuna mtu wa tatu

Mwajiri au Benki kuu hawawezi kuingilia hiyo process

Kwa ulivyoandika unaonyesha umelenewa na madeni pesa unapeleka wapi? Unafanyia Nini Cha maana?
 
Mleta mada hujielewi kabisa mkopo Ni Kati ya mkopaji na mkopeshaji tu hakuna mtu wa tatu

Mwajiri au Benki kuu hawawezi kuingilia hiyo process

Kwa ulivyoandika unaonyesha umelenewa na madeni pesa unapeleka wapi? Unafanyia Nini Cha maana?
Kama jambo hulijui, ni bora kukaa kimya.

Watanzania , hasa viongozi wa CCM, ubunifu ni jambo ambalo limetushinda. Asilimia kubwa ya mijadala yetu ni kuhusu matukio na kujadili kauli na vitendo vya watu maarufu kama wanasiasa na wasanii lskimi sio ubunifu


Wewe mawazo yako ni kuelrmewa na madeni tu na huwezi zaidi ya hapo.

No wonder mmeona suluhu ya kumlinda mtumishi ni kumuwekea hiyo sheria ambayo in real life, haifanyi kazi.
 
Kama jambo hulijui, ni bora kukaa kimya.

Watanzania , hasa viongozi wa CCM, ubunifu ni jambo ambalo limetushinda.
Waje kukubunia ukopaje? Kichwa chako kimegota hujui hata uongezeje mkopo serikali ije ikuwazie kwa niaba yako!!! Ubunifu wa kuongeza kipato chako mwenyewe kwa njia mbalimbali huna unataka serikali ikubunie hivi kichwani zimo kweli?
 
Kwa wale watumishi wa umma ambao taasisi zao huwalipa posho kila mwezi(mfano JWTZ, Polisi, n.k), wakati umefika waruhusiwe kukopa kupitia posho hizo kwa kukatwa sehemu ya posho zao kulipa mikopo watayochukua.

Tofauti na mikopo kupitia mishahara ambayo huwa ni ya muda mrefu (miaka 7 mpaka 8), mikopo kupitia allowance za kila mwezi, inaweza kuwa ni ya muda mfupi (mfano miezi 6 mpaka miaka 2).

Hii ni kwasababu, mishahara serikalini ni midogo na wakati huo huo, watumishi wananabwa na sheria inayowataka wabaki na walau moja ya tatu ya mishahara yao baada ya makato yote yakiwemo makato ya lazima kama Bima na ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Matokeo ya hali hii ni watumishi kupata mikopo midogo isiyolingana na mahitaji yao, na kuwafanya wengi kukimbilia katika microfinance ambazo licha ya kutowapa mikopo mikubwa, bali hutoa mikopo yenye riba kubwa na hata kufanya ile dhana ya mtumishi kubaki na moja ya tatu kuwa ni nadharia tu kwani mtumishi hulazimika kutumia mshahara huo huo kulipa mikopo ya mabenki na ya hizi financial institutions.

Hivyo, kwa wale watumishi wanaoweza kukopa kupitia posho zao za kila mwezi ambazo nazo hulipwa kupitia akaunti zao katika mabenki, wakati umefika waruhusiwe kukopa mikopo ya muda mfupi kupitia allowance zao za kila mwezi.

Tena, kama inawezekan, mtumishi aruhusiwe kutumia mshahara na allowance yake vyote kwa pamoja kupata mkopo na kwenye allowance, mtumishi aruhusiwe hata kukopea allowance yote mradi kaamua mwenyewe.

Mfano, mtumish ana allowance ya shilingi 300,000 kwa mwezi, na kupitia mshahara wake, anaweza pia kutumia shilingi 200,000 kukopea, maana yake mtumishi kama huyu, akiamua, anaweza kutumia shilingi 200,000 ya posho na hiyo 200,000 ya mshahara wke akapata jumla ya shilingi 400,000 kwa mwezi, kiasi anachoweza kwenda Benki na akachukua mkopo wa muda mfupi na akapata hela nzuri tu na akafanya mambo yake?

Jambo hili mimi naamini linawezekana iwapo serikali kupitia BOT, Utumishi na mabenki, watakaa pamoja na kulifanyia kazi wazo hili.

Watumishi wengi kwa sasa hawakopesheki katika mabenki kutona na sheria ya moja ya tatu(tusisahau pia kwa miaka 6 mshahara haijaongezwa) na hata wengi wa wanaokopesheke huishia kuchukua mkopo juu ya mkopo mwingine(top- up) na matokeo ni watu kupata vihela vidogo visivyokidhi mahitaji yao.

Mwisho, sheria ya mtumishi kutakiwa kubaki na moja ya tatu ya mshahara wake, nayo ipitiwe upya kwani haikuzingatia tofauti ya mishahara iliyopo baina ya watumishi na uhuru wa mtumishi kutumia mshahara wake kadri anayotoka.

Pia, kwakuwa mishahara serikalini ni midogo na haikidhi mahitaji, serikali iwaache watumishi kuamua ni namna gani watatumia mishahara yao kuendesha maisha yao.

Kumjali mtumishi sio kwa kumuwekea sheria ya kumlazimisha kubaki na moja ya tatu ya basic salary yake, bali ni kwa kuboresha masilahi yake( mtu miaka 6 mshahara ule ule halafu bado unampangia matumizi?).Haingii akilini.

CC: mwigulu nchemba
Allowances hazilipwi moja kwa moja kutoka hazina, zinapitia kwenye Taasisi husika.
Na zipo kwa mlengo maalum wa kumfanya Mfanyakazi kukidhi baadhi ya mahitaji muhimu hasa anapokuwa katika mafunzo ya baada ya kuajiriwa (posho ya chakula anapokuwa mafunzoni).
 
Hivi mishahara serikalini unaijua wewe?

Mtu ana take home ya shilingi 300,000 huku nauli ya kwenda kazini,chakula pamoja na maji kwa siku akijibana sana katumia shilingi 5,000 ambayo ni 150,000 kwa mwezi. Sasa mtu kama huyu unadhani hiyo sheria ya moja ya tatu inamlinda kivipi?
Sasa ukikopa ndio hiyo pesa itaongezeka ???

Sana sana ukikopa maana yake umeongeza matumizi ya hiyo pesa wakati bado ni ndogo.
 
Allowances hazilipwi moja kwa moja kutoka hazina, zinapitia kwenye Taasisi husika.
Na zipo kwa mlengo maalum wa kumfanya Mfanyakazi kukidhi baadhi ya mahitaji muhimu hasa anapokuwa katika mafunzo ya baada ya kuajiriwa (posho ya chakula anapokuwa mafunzoni).
Ndio tatizo letu hili.Kwani hizi allowance si zinapita katika benki unayopokelea mshahara?
 
Hapo ndio akili yenu inapoishia.

Na kama hujui ni namna gani mikopo hii ukitumia vizuri unaweza kupiga hatua,mada kama hii huwezi kuelewa.
Ungekuwa unajua kutumia vizuri hiyo mikopo uliyokopa ingeshakutoa usingehitaji Tena kuwa posho nazo ziingizwe ukakopee .Wewe inanyesha mshahara wote unaishia kulipa madeni.Kwani ulizokopa ulifanyia Nini ambacho hakizalishi ujikwamue kwenye Lindi la madeni
 
Back
Top Bottom