Serikali kushindwa kulipa malimbikizo ya wafanyakazi ni aibu

Serikali kushindwa kulipa malimbikizo ya wafanyakazi ni aibu

Mtemi mpambalioto

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2015
Posts
3,436
Reaction score
7,955
Imekuwa ni porojo tu utumishi huko na hazina.

Bora tu kaondoka Jenista maana alikuwa gundu watu hawalipwi madai yao!

Hivi Serikali mnawaona wafanyakazi wanyonge au mapoyoyo? Kutwa kujifanya mnaandaa malipo ya malimbikizo na hamlipi?

Je, Rais naye anadanganywa kuhusu hili?
 
Imekuwa ni porojo tu utumishi huko na hazina.

Bora tu kaondoka Jenista maana alikuwa gundu watu hawalipwi madai yao!

Hivi Serikali mnawaona wafanyakazi wanyonge au mapoyoyo? Kutwa kujifanya mnaandaa malipo ya malimbikizo na hamlipi?

Je, Rais naye anadanganywa kuhusu hili?
Kuna rais pale au mwanaseseri
 
Historia ya mageuzi katika dunia ililetwa na wafanyakazi lakini Tanzania ni tofauti kabisa badala ya kupigania haki zao wafanyakazi wa Tanzania ndio machawa no 1 ya viongozi wamebaki kuvaa manguo ya ajabu ajabu siku ya Mei mosi

"Penal colony wa serikali"
kazi ipo kwa kweli
 
Watanzania tuna kawaida moja tu ya unafiki uliotukuka.

Tuna umoja sana wa kulalamikia haki zetu nyuma ya mabwana wakubwa na tunasapotiana kwenye hilo ila ikija kwenye kuonesha misimamo yetu ya dhahiri huwa tunatabia ya kuufyata kwa hofu ya reaction yao dhidi yetu.

Hapo ndipo ubinafsi unapo kick in na kutumaliza. Kila mtu anaangalia tumbo lake kwanza akishiba tu wengine mtajijua wenyewe. Wakubwa wameshajua udhaifu wetu huu na wanautumia kutukandamiza na kutufanya misukule kadri watakavyo. Wakitishia kidogo tu kumwaga ugali watu wanaufyata. Kwa style hii tutaburuzwa hadi kiama.
 
Watanzania tuna kawaida moja tu ya unafiki uliotukuka.

Tuna umoja sana wa kulalamikia haki zetu nyuma ya mabwana wakubwa na tunasapotiana kwenye hilo ila ikija kwenye kuonesha misimamo yetu ya dhahiri huwa tunatabia ya kuufyata kwa hofu ya reaction yao dhidi yetu.

Hapo ndipo ubinafsi unapo kick in na kutumaliza. Kila mtu anaangalia tumbo lake kwanza akishiba tu wengine mtajijua wenyewe. Wakubwa wameshajua udhaifu wetu huu na wanautumia kutukandamiza na kutufanya misukule kadri watakavyo. Wakitishia kidogo tu kumwaga ugali watu wanaufyata. Kwa style hii tutaburuzwa hadi kiama.

Na cycle ya unafiki ilianzia kwa mababu zetu hadi leo, huu uchawa umeanza zamani sema unabadilika jina haukumbuki wale waliitwa makuwadi? Mtu mjamaa hua ni muoga sana kuliko bepari ndio maana china alijibadili itikadi akachukua ujamaa wake akachanganya na ubepari akatembea mbele kwenda kwenda kwenye maendeleo
 
Na cycle ya unafiki ilianzia kwa mababu zetu hadi leo, huu uchawa umeanza zamani sema unabadilika jina haukumbuki wale waliitwa makuwadi? Mtu mjamaa hua ni muoga sana kuliko bepari ndio maana china alijibadili itikadi akachukua ujamaa wake akachanganya na ubepari akatembea mbele kwenda kwenda kwenye maendeleo
Kama ni ujamaa ndio umetufanya hivi basi ujamaa ni wa kuachwa kabisa. Ni aina flani ya utumwa wa kifikra na unadumisha uoga usio na tija.

Tunaposhindwa kuambiana ukweli ulio dhahiri na badala yake tunakuwa watu wa kulalamika tu tunatengeneza kizazi cha ajabu sana. We create unneccesary competition baina yetu wenyewe na ndio maana leo hii badala ya kupigania haki zetu kwa umoja kunakuwa na undumi la kuwili.

Wafanyakazi badala kutetea maslahi yao, wanamteua mwakilishi ambaye anaenda ku side na serikali ili kuwadhibiti wasisikike na pengine kuwaziba midomo ikiwa anapewa maslahi flani.
 
Kama ni ujamaa ndio umetufanya hivi basi ujamaa ni wa kuachwa kabisa. Ni aina flani ya utumwa wa kifikra na unadumisha uoga usio na tija.

Tunaposhindwa kuambiana ukweli ulio dhahiri na badala yake tunakuwa watu wa kulalamika tu tunatengeneza kizazi cha ajabu sana. We create unneccesary competition baina yetu wenyewe na ndio maana leo hii badala ya kupigania haki zetu kwa umoja kunakuwa na undumi la kuwili.

Wafanyakazi badala kutetea maslahi yao, wanamteua mwakilishi ambaye anaenda ku side na serikali ili kuwadhibiti wasisikike na pengine kuwaziba midomo ikiwa anapewa maslahi flani.

Ndio Ujamaa ndio ulifanya watanganyika wawe hawana msimamo kabisa, hata wachache wenye mafanikio wana itikadi za kibepari vichwani mwao walishaachana na ujamaa kabisa, hao watumishi wanadai mapesa mengi lakini wakipewa kazi ya sensa au uchaguzi na wakavishwa matishet wanachekelea jino hadi la mwisho, wanashindwa kudai sio madeni tu lakini haki zao za msingi kama posho ya usafiri, posho ya mawasiliano, posho ya nyumba, posho ya muda wa ziada, posho ya mazingira magumu, hapo kila dai wakipewa 20k tu kwa kada za watumishi wengi unaona kabisa kuna laki hivi itawasogeza sehemu
 
Watanzania tuna kawaida moja tu ya unafiki uliotukuka.

Tuna umoja sana wa kulalamikia haki zetu nyuma ya mabwana wakubwa na tunasapotiana kwenye hilo ila ikija kwenye kuonesha misimamo yetu ya dhahiri huwa tunatabia ya kuufyata kwa hofu ya reaction yao dhidi yetu.

Hapo ndipo ubinafsi unapo kick in na kutumaliza. Kila mtu anaangalia tumbo lake kwanza akishiba tu wengine mtajijua wenyewe. Wakubwa wameshajua udhaifu wetu huu na wanautumia kutukandamiza na kutufanya misukule kadri watakavyo. Wakitishia kidogo tu kumwaga ugali watu wanaufyata. Kwa style hii tutaburuzwa hadi kiama.
Ukweli huu mkuu ,uoga uliotawaliwa na uzuzu, wapi mafao ya wafanyakazi wa EAC?wanasiasa walafi wa nchi hii wamedhulumu ile fedha,na wazee wale wanakufa mmoja baada ya mwingine bila kupata haki zao,inahudhunisha mno
 
Ndio Ujamaa ndio ulifanya watanganyika wawe hawana msimamo kabisa, hata wachache wenye mafanikio wana itikadi za kibepari vichwani mwao walishaachana na ujamaa kabisa, hao watumishi wanadai mapesa mengi lakini wakipewa kazi ya sensa au uchaguzi na wakavishwa matishet wanachekelea jino hadi la mwisho, wanashindwa kudai sio madeni tu lakini haki zao za msingi kama posho ya usafiri, posho ya mawasiliano, posho ya nyumba, posho ya muda wa ziada, posho ya mazingira magumu, hapo kila dai wakipewa 20k tu kwa kada za watumishi wengi unaona kabisa kuna laki hivi itawasogeza sehemu
Inaonesha kwenye itikadi za ujamaa kudai haki ni sign ya kiherehere na malipo yake huwa ni elimination. Fear of unknown ndio silaha ya watawala.
 
Serikali hii inadharau sana watumishi wake kwani kuna watumishi wanadai hizo arrears kwa miaka mingi wengine tangu mwaka 2015 na 2017 wanachokifanya wanavuta miezi kadha ndani ya mwaka wa fedha wanaweza kulipa watu wachache sana huku wakichagua wenye madai madogo wanaodai vihela vingi kidogo mfano milioni mbili na kuendelea ni kama madai yao hayaonekani kwenye mfumo kumbe usanii.Lipeni madai ya watumishi wote waliohakikiwa miaka na miaka ili hao maafisa ugani wetu ,manesi wetu na walimu wetu waweze kufanya kazi kwa moyo mkunjufu ili serikali iweze kufikia malengo yake ya kuwapa huduma bora kwa wananchi wake.

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom