Serikali Kushirikiana na Sekta Binafsi Katika Utekelezaji wa Miradi

Serikali Kushirikiana na Sekta Binafsi Katika Utekelezaji wa Miradi

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI.

Wizara ya Ujenzi imeanza utaratibu wa kushirikisha sekta binafsi kwa utaratibu wa ubia (PPP)katika kutekeleza miradi ya miundombinu.

Haya yamebainishwa na Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa wakati wa kuwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2024/25, Bungeni jijini Dodoma leo, Mei 29, 2024

Amesema ni katika kuipunguzia Serikali gharama kubwa za utekelezaji wa miradi ya miundombinu hasa barabara na madaraja ambayo Serikali imekuwa ikitumia kiasi kikubwa cha fedha.

“Lengo la kutumia utaratibu huu ni kujenga miundombinu na kuitekeleza kwa wakati.”

Aliitaja iradi inayotekelezwa kwa utaratibu huo kuwa ujenzi wa barabara ya Kibaha-Chalinze-Morogoro-Dodoma (Expressway) yenye urefu wa kilometa 423.8 kwa mfumo wa kulipia.

MWISHO
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.36.jpeg
    WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.36.jpeg
    314.1 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.37.jpeg
    WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.37.jpeg
    294.9 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.42(1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.42(1).jpeg
    342.5 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.40.jpeg
    WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.40.jpeg
    305 KB · Views: 2
  • WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.39.jpeg
    WhatsApp Image 2024-05-29 at 10.58.39.jpeg
    349.6 KB · Views: 3
Back
Top Bottom